DOKEZO Maji ya kuoshea maiti yanayo lalamikiwa kutumika kuhifadhia samaki yanauzwa kwenye maduka ya dawa za asili, Serikali imulike huko

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,283
3,274
Salaam,

Tafiti zinaonesha kwamba wagonjwa wengi wa Saratani wamekuwa wakitokea Kanda ya Ziwa jambo ambalo linapelekea Serikali kuhangaika kutafuta sababu kwanini Kanda ya Ziwa?

Jana nimeona Mh Makamu wa Rais akiwa hospitali ya Bugando ameeleza moja ya sababu inayopelekea takwimu za saratani kuwa juu Kanda ya Ziwa ni watu wanaotumia maji ya kuoshea maiti kuhifadhia samaki.

Nimeona niijulishe Serikali kwamba moja ya wateja wakubwa wa maji haya ni waganga wa kienyeji na maji haya yanauzwa kwenye maduka ya dawa asili.

Ili Serikali ifanikiwe kudhibiti usambaaji wa biashara hii nashauri wahakikishe masoko yote pamoja na mochwari ambapo ndipo yanapotoka wanadhibiti vinginevyo tatizo hili litaendelea.

Asante.
---

Kauli Makamu wa Rais kuhusu maji ya kuoshea maiti Kusababisha kansa

1663145803022.png

Picha: Sehemu ya gazeti iliyoandika habari hii

Baada ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK. Phillip Mpango amesema ongezeko kubwa la ugonjwa wa saratani katika mikoa ya kanda ya ziwa unatokana na baadhi ya watu kutumia maji ya yanayotumika kuoshea maiti pamoja na dawa aina ya Cloroform inayotumika kuhifadhi samaki.

DK. Mpango alizungumza hayo wakati wa uzinduzi wa jengo la wagonjwa wa saratani katika huspitali ya rufani ya kanda Bugando jijini Mwanza, jengo ambalo limejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 5.6.

Baada ya kauli hiyo, inadaiwa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza, Jana jioni ilianza kugawa fedha kwa waandishi wa habari kuzuia stori hiyo isitoke kwenye vyombo vya habari.

Taarifa kutoka ndani ya ofisi ya mkuu wa mkoa zinadai, fedha hizo zilikuwa zikitolewa na Katibu wa mkuu wa mkoa, bwana Matia Levi.

Inaelezwa zaidi ya waandishi 20 walipokea mshiko huo ili habari hiyo isiandikwe, lakini waandishi walipokea na kutoa habari hiyo.

Hata hivyo Leo mchana, Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mwanza kitazungumza na vyombo vya habari kuhusu taarifa hiyo na inaelezwa wamesikitishwa na kauli ya Makamu wa Rais.
 
Salaam,

Tafiti zinaonesha kwamba wagonjwa wengi wa saratani wamekuwa wakitokea kanda ya ziwa jambo ambalo linapelekea serikali kuhangaika kutafuta sababu kwanini kanda ya ziwa...
Formaline? au maji yapi tena , niliwai sikia hutumia Formaline, ambayo wanasema inasaidia fukuza inzi, but all in all Kama ni kweli basi Hawa ni wauwaji Kama wauwaji wengine,
 
Formaline? au maji yapi tena , niliwai sikia hutumia Formaline, ambayo wanasema inasaidia fukuza inzi, but all in all Kama ni kweli basi Hawa ni wauwaji Kama wauwaji wengine,
Mwanza sili tena samaki zenu 😆🤣
 
This is a very cheap argument, maji ya kuoshea maiti yana uhusiano gani na kutokea saratani.......do you have any mechanism behind.

Labda tuseme unamaanisha kemikali inayotumika kuhifadhi maiti, mfano formali, .hivi inaingia akilini utumie formalin kwenye samaki na isilete usumbufu kwa watu wanaohusika na wateja kwa kupiga chafya au kuwashwa machoni? Hizo kemikali are very pungent ukiifungua kidogo tu hapawezi kukalika.

Kama swala ni saratani inasabbishwa na hivyo vitu kutumika kuhifadhia samaki, logic inaonyesha kwamba case za saratani zingekuwa nyingi mikoa ya mbali na Mwanza maana ndo watatumia zaidi samaki waliohifadhiwa kuliko Mwanza ambako tutategemea watu wengi wanatumia samaki fresh ambao hawajahifadjiwa na kitu chochote.
Hawa watu wanajaribu kupotosha kiini cha saratani kuwa juu huko Mwanza sijui kwa maslahi ya nani. Wafanye utafiti wenye mashiko, tatizo la saratani kuwa juu kanda ya ziwa ni kutokana na kemikali za migodini zinazoelekezwa kwenye vyanzo vya maji ikiwemo mito na kuishia ziwani. Haya ndo yaleyale ya tume ya Manyere kwamba samaki wa mto Mara walikufa kutokana na kuzidiwa na kinyesi na mikojo ya ng'ombe. Pathetic!!
 
Salaam,
Tafiti zinaonesha kwamba wagonjwa wengi wa saratani wamekuwa wakitokea kanda ya ziwa jambo ambalo linapelekea serikali kuhangaika kutafuta sababu kwanini kanda ya ziwa?
...
Inawezekana kuna ka- Ukweli ndani yake. Lakini nawasihi wataalamu wetu wa saratani wazidi kufanya utafiti wa chanzo cha saratani kanda ya ziwa. Kuna sababu zaidi ya hiyo. Sababu haingii akilini mtu wa Kyerwa, Muleba, Kanyigo.

Murugwanza, ana pata saratani Eti sababu amekulia samaki waliooshewa maji ya maiti. Wakati watu wa Muleba, Kanyigo wanapata samaki flesh toka ziwa I (Victoria).

Sababu zipo zaidi ya hiyo fanyeni utafiti wa kina. Please, don't easily jump to the conclusion. Cancer imekuwepo kwa wingi kanda hiyo kabla hizi Zebaki na dawa za kuhifadhi maiti haijawa 'common'.
 
Back
Top Bottom