Serikali liangalieni hili la mashabiki kusafiri na Stars kwenda Cape Verde

Habari za asubuhi watu wa JF,

Leo nimesikia Serikali imetoa ndege kwa lengo la kuipeleka Taifa Stars ktk visiwa vya Cape Verde, kwa jambo hilo kwanza naipongeza Serikali yetu saaaaana.

Lakini napenda kutoa wazo katika hilo juu ya bei ya abiria ambao watapenda kwenda na timu huko Cape Verde ili kuishangilia timu yetu hii pendwa ya taifa.

Serikali imetangaza shabiki yeyote atakayetaka kwenda na timu atalipia kiasi cha 1,500 USD Ambayo ni zaidi ya Shilingi 3,000,000,/= (milioni tatu). Kwa kiasi hiki kuna watu watashindwa kulipia japo wana moyo. Mimi naomba liangaliwe upya hili swala la washingiliaji ama bei ipungue au isiwepo kabisa ili kuhakikisha idadi kubwa ya mashabiki kuhudhuria.

Asanteni.
Unajaribu kusema au kuomba nini ndugu! Kuwa kama ''wana moyo wa kwenda'' basi wapunguziwe gharama ili waende? Kwani umeshambiwa kuwa kuna upungufu wa watu wenye moyo wa kusafiri na timu? Kama unataka kwenda basi tafuta hizo fedha! Katika maisha ya kila siku moyo huwa unapenda kufanya mengi lakini uwezo ndiyo unatuzuia.
 
Mimi sikubaliani kabisa kwa Tanzania kuanza kuingiza tena siasa katika biashara. Nchi yetu kiuchumi bado tunachangamoto nyingi na si kipaumbele kwasasa na si sahihi kuingilia uendeshaji wa mashirika ya Umma kama ATC na kutoa ndege ambayo ni ya kibiashara kulet/kuingiza mambo ya michezo. Hiyo ndege ingekodishwa kwa terms za kibiashara either na wadau wa mpira/wafadhili au kama ni Serikali basi ilipe shirika la ndege ATC gharama halisi kwa rate ya market/soko ili ATC iweze kujiendesha kibiashara

Nani aliyekuambia kwamba iko kibiashara?
 
Habari za asubuhi watu wa JF,

Leo nimesikia Serikali imetoa ndege kwa lengo la kuipeleka Taifa Stars ktk visiwa vya Cape Verde, kwa jambo hilo kwanza naipongeza Serikali yetu saaaaana.

Lakini napenda kutoa wazo katika hilo juu ya bei ya abiria ambao watapenda kwenda na timu huko Cape Verde ili kuishangilia timu yetu hii pendwa ya taifa.

Serikali imetangaza shabiki yeyote atakayetaka kwenda na timu atalipia kiasi cha 1,500 USD Ambayo ni zaidi ya Shilingi 3,000,000,/= (milioni tatu). Kwa kiasi hiki kuna watu watashindwa kulipia japo wana moyo. Mimi naomba liangaliwe upya hili swala la washingiliaji ama bei ipungue au isiwepo kabisa ili kuhakikisha idadi kubwa ya mashabiki kuhudhuria.

Asanteni.
Usichanganye Biashara na ushabiki wa mpira bei ibakie hiyo hiyo.
 
Habari za asubuhi watu wa JF,

Leo nimesikia Serikali imetoa ndege kwa lengo la kuipeleka Taifa Stars ktk visiwa vya Cape Verde, kwa jambo hilo kwanza naipongeza Serikali yetu saaaaana.

Lakini napenda kutoa wazo katika hilo juu ya bei ya abiria ambao watapenda kwenda na timu huko Cape Verde ili kuishangilia timu yetu hii pendwa ya taifa.

Serikali imetangaza shabiki yeyote atakayetaka kwenda na timu atalipia kiasi cha 1,500 USD Ambayo ni zaidi ya Shilingi 3,000,000,/= (milioni tatu). Kwa kiasi hiki kuna watu watashindwa kulipia japo wana moyo. Mimi naomba liangaliwe upya hili swala la washingiliaji ama bei ipungue au isiwepo kabisa ili kuhakikisha idadi kubwa ya mashabiki kuhudhuria.

Asanteni.
We kama huna pesa waache wenye uwezo waende
 
Nimemsikiliza waziri mwenye dhamana na michezo akiwa na mrari kubwa sana na yawezekana ndio kasababisha mpaka ndege ya serikali ilatolewa, mimi nina ushauri ufautao kama yumo humu ama kuna watu wanaofahamiana naye wampelekee habari

1.Mtanzania mwenye uwezo wa kulipa nauli ya 3,000,000/= huyo si SHABIKI bali ni MWEKEZAJI,huyu hata hawezi kubeba na kupuliza vuvuzela ili kuwapa morari wachezaji

2.Watafute wale washangiliaji bora na maarufu kwa kila timu kama wale wa Yanga na Simba wanaova MAVITAMBI ya bandia, Yule wa mbao anayevua shati na kucheza na chungu kinachowaka moto mwanzo mwisho, wawatafutie mavazi yenye rangi za taifa na kujipaka marangi ya bendera yetu ndio wawasafirishe kwa garama za serikali ama hata sisi wengine tuwachangie, kama Yanga inachangiwa na sasa inafanya vizuri tutashindwa nini kwa washabiki wanaokwenda kuitangaza nchi yetu ugenini?

3. Waziri amesema anataka washabiki wanaoshangilia kistarabu ila sikumwelewa, ninachokataa ni kama kile walichokifanya washabiki wa timu moja hapa bongo kungoa viti, lakini kupiga kelele, kuimba nyimbo,na kupiga matarumbeta hilo sii kosa, lazima wachezaji wakiwa wanacheza wasikie sauti za watu wao zikiwapa morari. Misri iliwahi kuja kucheza na stars taifa wakiwa na mashabiki wasiozidi 20 lakini waliwasha mienge ,kuvua mashati na kuimba byimbo zao na kufanikiwa kutunyamazisha wengine tuliojaa uwanja mzima na walishinda mechi ile ugenini.

4.Watafute kikundi kimoja maafufu cha matarumbeta kinachojua kupiga nyimbo za hamasa nacho kilipiwe

5. Watafutwe warembo bomba kabisa , hasa wale wanaojiita ma Tanzania sweat heart, wavalie Tshirts na vidani vyenye rangi za TAIFA, Tena wale wenye tukunyema itakuwa vyema zaidi ili wakitua tuu pale kwenye airport yao waanza kuchanganyikiwa

6. Ma captain wote wa timu za Taifa wa vijana na wanawake wawe sehemu ya msafara kama mashabiki lakini , wawe wameenda kama shule kuangalia wenzao wanafanya nini na wao wajifunze kitu
Safi sana. Naamini wewe ni mpenzi wa soka na pia "tukunyema".
 
Safi sana. Naamini wewe ni mpenzi wa soka na pia "tukunyema".
Hapana ni mzalendo tuu, na ninatoa ushauri maana ni pamoja na kuitangaza nchi yetu ugenini kwani kuna baadhi ya nchi hazitujui na wala hawajawahi kuiskia nchi yetu. Sasa tunapopata nafasi ya kuwatembelea ni kuivamia katika kila idara, hapo utaona kila mtu anatamani kuja kuitembelea Tanzania. Tukipeleka midume mitupu haipendezi, wewe huwa huwaoni akinadada mashabiki wa timu za soka hapa bongo wanavyotokelezea wakivaa sare za timu zao,huku ma wigi yakiwaninginia wanavyovutia, sasa mfano uwachague walio bora kabisa wavae rangi za taifa, na amasuruali matatata wakitua ugenini itakuwaje?
 
Hapana ni mzalendo tuu, na ninatoa ushauri maana ni pamoja na kuitangaza nchi yetu ugenini kwani kuna baadhi ya nchi hazitujui na wala hawajawahi kuiskia nchi yetu. Sasa tunapopata nafasi ya kuwatembelea ni kuivamia katika kila idara, hapo utaona kila mtu anatamani kuja kuitembelea Tanzania. Tukipeleka midume mitupu haipendezi, wewe huwa huwaoni akinadada mashabiki wa timu za soka hapa bongo wanavyotokelezea wakivaa sare za timu zao,huku ma wigi yakiwaninginia wanavyovutia, sasa mfano uwachague walio bora kabisa wavae rangi za taifa, na amasuruali matatata wakitua ugenini itakuwaje?
Kweli kabisa mzee wa tukunyema.:D
 
Nimemsikiliza waziri mwenye dhamana na michezo akiwa na mrari kubwa sana na yawezekana ndio kasababisha mpaka ndege ya serikali ilatolewa, mimi nina ushauri ufautao kama yumo humu ama kuna watu wanaofahamiana naye wampelekee habari

1.Mtanzania mwenye uwezo wa kulipa nauli ya 3,000,000/= huyo si SHABIKI bali ni MWEKEZAJI,huyu hata hawezi kubeba na kupuliza vuvuzela ili kuwapa morari wachezaji

2.Watafute wale washangiliaji bora na maarufu kwa kila timu kama wale wa Yanga na Simba wanaova MAVITAMBI ya bandia, Yule wa mbao anayevua shati na kucheza na chungu kinachowaka moto mwanzo mwisho, wawatafutie mavazi yenye rangi za taifa na kujipaka marangi ya bendera yetu ndio wawasafirishe kwa garama za serikali ama hata sisi wengine tuwachangie, kama Yanga inachangiwa na sasa inafanya vizuri tutashindwa nini kwa washabiki wanaokwenda kuitangaza nchi yetu ugenini?

3. Waziri amesema anataka washabiki wanaoshangilia kistarabu ila sikumwelewa, ninachokataa ni kama kile walichokifanya washabiki wa timu moja hapa bongo kungoa viti, lakini kupiga kelele, kuimba nyimbo,na kupiga matarumbeta hilo sii kosa, lazima wachezaji wakiwa wanacheza wasikie sauti za watu wao zikiwapa morari. Misri iliwahi kuja kucheza na stars taifa wakiwa na mashabiki wasiozidi 20 lakini waliwasha mienge ,kuvua mashati na kuimba byimbo zao na kufanikiwa kutunyamazisha wengine tuliojaa uwanja mzima na walishinda mechi ile ugenini.

4.Watafute kikundi kimoja maafufu cha matarumbeta kinachojua kupiga nyimbo za hamasa nacho kilipiwe

5. Watafutwe warembo bomba kabisa , hasa wale wanaojiita ma Tanzania sweat heart, wavalie Tshirts na vidani vyenye rangi za TAIFA, Tena wale wenye tukunyema itakuwa vyema zaidi ili wakitua tuu pale kwenye airport yao waanza kuchanganyikiwa

6. Ma captain wote wa timu za Taifa wa vijana na wanawake wawe sehemu ya msafara kama mashabiki lakini , wawe wameenda kama shule kuangalia wenzao wanafanya nini na wao wajifunze kitu
Umeongea kitu cha msingi sana ,Mkuu
 
Hiyo Nauli n Sawa was was Wang Sizan Kama wataenda wale mashabik vichaa wanaojua kuamsha morali
 
Habari za asubuhi watu wa JF,

Leo nimesikia Serikali imetoa ndege kwa lengo la kuipeleka Taifa Stars ktk visiwa vya Cape Verde, kwa jambo hilo kwanza naipongeza Serikali yetu saaaaana.

Lakini napenda kutoa wazo katika hilo juu ya bei ya abiria ambao watapenda kwenda na timu huko Cape Verde ili kuishangilia timu yetu hii pendwa ya taifa.

Serikali imetangaza shabiki yeyote atakayetaka kwenda na timu atalipia kiasi cha 1,500 USD Ambayo ni zaidi ya Shilingi 3,000,000,/= (milioni tatu). Kwa kiasi hiki kuna watu watashindwa kulipia japo wana moyo. Mimi naomba liangaliwe upya hili swala la washingiliaji ama bei ipungue au isiwepo kabisa ili kuhakikisha idadi kubwa ya mashabiki kuhudhuria.

Asanteni.
Hivi kwan bei ya kwenda na kurudi huko kepu vede huwa ni shngap, ili tulinganishe na bei ya serikali.
Isije ikawa serikali ndo imetumia fursa hahahahhaahhah
 
Back
Top Bottom