Serikali kwanini mnalishusha hadhi sana jiji la Mwanza?

Mmekuwa mkituimbia ka wimbo ka tunataka kuifanya Mwanza kuwa kitovu cha biashara cha maziwa makuu kwa kuimarisha miundombinu na miundomsingi.

Hatukatai kuwa juhudi zenu baadhi zinaonekana kama ujenzi wa meli, daraja, masoko, stendi za magari,reli, uwanja wa ndege n.k kwa hapa niwapongeze kwa nia yenu ya dhati kabisaa mliyonayo kwa jiji letu pendwa la sato.

Kinachonikera mimi si kingine bali naona kama nyie SERIKALI ndiyo kikwazo cha ukuaji chanya wa mji wetu wa Mwanza, mnauzorotesha na wala hamuupi kipaumbele unachostahili kama jiji la pili hapa Tanzania nayakwamba ni taswira ya pili ya nchi yetu ikitoka hiyo Dar mnayoangaika kuiboresha kila uchao.

Leo hii jiji kubwa kama Mwanza halina taa hata moja ya barabarani kuanzia usagara mpaka unafika mjini na tokea mjini mpaka kisesa ni giza tupu, mabatini ilivyokuwa ikijulikana kwa kuchangamka nyakati za usiku pale gengeni leo hii kweli nipakukutana na ulinzi shirikishi highway saa 3 wamebebelea mapanga kisa wanaimarisha ulinzi eti mitaa ina giza hivyo vibaka na wezi ni tishio.

Bila aibu mmewaachia kazi yenu wanamwanza waishio milimani ndo wawashe taa za majumbani mwao ndo waupe mji mwangaza kisa magari yenu yanataa hivyo haina haja ya kuweka taa za kumulika barabara, eti Mwanza na fahari yake yote inabakia kuwa jiji la taa moja tena ya kuongozea magari pale buzuruga junction, Are we serious?

Jiji la Mwanza linakabiliwa na uhaba mkubwa mno wa mtandao wa barabara za LAMI kuanzia zile kuu mpaka za mitaani ni vumbi tupu, tunawazeeshea watu magari yao utadhani wanafanya biashara kijijini, Vituo vya daladala ndo sasa usiseme ni full vumbi na makorongo.

Hivi inawapendeza sana waheshimiwa mkipita na magari yenu ya kifahari na ving'ora kwenye highway ya lanes mbili na tatu ambazo hamna hata mpango wa kuzitanua at least ziwe 6,8 au 12 kuondoa misongamano na overtakes zisizo na ulazima katika majiji yetu au mnawaona watanzania kama vile wapo usingizini na wala miji yao haiwaumi ikipitwa kwenye suala la miundombinu na vimiji vidogo vidogo kwenye nchi za jirani.

Hivi kwanini suala la ring roads, barabara pana, fly overs,taa za barabarani, n.k kwa miji yetu yote hata kama mkiamua kuanza na ile mikubwa hamuipi kipaumbele na wala hamuonekani kujishtukia kuwa kama nchi mnadumaza ukuaji mzuri wa miji na majiji pia mnatuchelewesha kimaendeleo, mnatufanya tuonekane hatuna maana mbele ya vinchi vichanga tudharaulike na kuonekana watanzania ni washamba na miji yao miundombinu yake haiendani na karne ya 21.

Ifikie wakati kama nchi masula ya miundombinu bora katika majiji yetu uwe ni ushindani wa kawaida na majiji yaliyoendelea zaidi duniani natuchukulie ni jambo la kawaida na siyo ufahari au kuhisi watanzania sote hatuna exposure,

hivyo inapotokea mkijenga kitu kidogo kama kidaraja cha juu cha waendao kwa miguu matangazo yanakuwa mengi na bado mnategemea tuwasifiwe kana kwamba hatukupaswa kuwa navyo ila kwa hisani mmeamua kutuzawadia vitu ambavyo si level zetu sijuhi huwa mnatuonaje.

Mlikuwa na mpango mzuri kabisa wa kuondoa vipanya(hiace) katika mzunguko wa jiji nabadala yake zitumike basi kubwa au coaster kama daladala na wananchi wa Mwanza walivyo wapenda maendeleo mwitikio ulikuwa mkubwa,

watu wakaanza kuingiza barabarani magari yao cha ajabu ruti zote mpaka leo zimebakia kusomeka nyashishi au airport no otherwise kwingineko miundombinu majanga nani ajitose kupeleka gari kwenye vumbi,milima na majabari akagongeshe gari kwenye mashimo na kudondosha vioo vya gari lake au kukata shock ups zake.

Hivi hata kutenga maeneo kadhaa ya wazi nakupanda miti,nyasi, kuweka mabenchi, swimming, sanamu, sinema au mabembea kuufanya mji uwe na bustani kadhaa za kupumzikia kuanzia CBD hadi mitaani
kupendezesha jiji pia ni mpaka mkumbushwe nyie mnaojihita mamlaka ya jiji.

Kuna ufahari gani kutembea ukiona maghorofa lakini huna pa kupumzikia matokeo yake tunajazana tukikaa kwenye msingi mbele ya geti la pamba sekondari utafikiri omba omba kumbe hatuna namna.

Leo hii unashuhudia kati kati ya jiji la Mwanza (CBD) mtu bado anapewa kibali na anafanya ujenzi wa nyumba ya chini(isiyo ya ghorofa) kwa ajili ya kuishi yeye na wapangaji wake tena around main roads sehemu ambazo ni promising sana na anaruhusiwa kuendelea na ujenzi wake bila bughudha vitu vinavyopelekea mwonekano mbovu wa sura ya jiji, hapo pembeni utashuhudia jumba la ghorofa 8 pembeni(chini yake) vibanda kama sita vyenye bati za kutu zimezingira.

Kuna maeneo kadhaa bado miundombinu ya maji ni shida na miundombinu mingi ya maji inajengwa kwa mwendo wa kuchechemea mno.

Itoshe kusema kuwa changamoto ni nyingi katika jiji hili ila chanzo kikuu ni SERIKALI naomba BADILIKENI.
Umeandika huu uzi ukidhani utawashawishi wanamwanza waichukie CCM. Umejidanganya sana. Tafuta kazi ya kufanya.
 
1. Sio kweli kwamba jiji la mwanza ni buzuruga tu ndio kuna mataa ya kuongozea magari.je wajua kwa sasa hadi kisesa kuna mataa ya kuongozea magari na watu pale njia panda ya kwenda kwenye makumbusho ya wasukuma bujora... pia igoma karibia na njia panda ya kishiri bila kusahau national changamoto ni bado hayajaanza kufanya kazi.

Mataa ya kuongozea magari na watu yaliyo maarufu zaidi ni

1. Mataa ya lumumba hapa zinakutana barabara tano
2.Mataa ya buzuruga hapa zinakutana barabara tatu
3.Mataa ya Ghana (kona ya bwiru) naweza Sema haya ndio mataa ya kisasa zaidi maana yanaonesha mpaka dakika
4.mataa ya pansiasi barabara ya airport+mjin na nyasaka inaenda kuunga kiloleni haya nayo ni mataa ya kisesa yanayoonyesha hadi dakika

Mpaka hapo nimeshakuonyesha ni jinsi gani umepotosha wananchi wa jf
emoji38.png
kiujumla mataa ya kuongozea magarina watu kwa jiji la mwanza yanafika 20+ ila ndio hivyo mengi hayajaanza kufanya kazi na mengine yanafanyakazi usongelea taa za kusaidia mwanga narabarani siyo taa za kuongozea magari...
Anaongelea taa za kusaidia mwanga barabarani...haongelei traffic lights..
 
Mmekuwa mkituimbia ka wimbo ka tunataka kuifanya Mwanza kuwa kitovu cha biashara cha maziwa makuu kwa kuimarisha miundombinu na miundomsingi.

Hatukatai kuwa juhudi zenu baadhi zinaonekana kama ujenzi wa meli, daraja, masoko, stendi za magari,reli, uwanja wa ndege n.k kwa hapa niwapongeze kwa nia yenu ya dhati kabisaa mliyonayo kwa jiji letu pendwa la sato.

Kinachonikera mimi si kingine bali naona kama nyie SERIKALI ndiyo kikwazo cha ukuaji chanya wa mji wetu wa Mwanza, mnauzorotesha na wala hamuupi kipaumbele unachostahili kama jiji la pili hapa Tanzania nayakwamba ni taswira ya pili ya nchi yetu ikitoka hiyo Dar mnayoangaika kuiboresha kila uchao.

Leo hii jiji kubwa kama Mwanza halina taa hata moja ya barabarani kuanzia usagara mpaka unafika mjini na tokea mjini mpaka kisesa ni giza tupu, mabatini ilivyokuwa ikijulikana kwa kuchangamka nyakati za usiku pale gengeni leo hii kweli nipakukutana na ulinzi shirikishi highway saa 3 wamebebelea mapanga kisa wanaimarisha ulinzi eti mitaa ina giza hivyo vibaka na wezi ni tishio.

Bila aibu mmewaachia kazi yenu wanamwanza waishio milimani ndo wawashe taa za majumbani mwao ndo waupe mji mwangaza kisa magari yenu yanataa hivyo haina haja ya kuweka taa za kumulika barabara, eti Mwanza na fahari yake yote inabakia kuwa jiji la taa moja tena ya kuongozea magari pale buzuruga junction, Are we serious?

Jiji la Mwanza linakabiliwa na uhaba mkubwa mno wa mtandao wa barabara za LAMI kuanzia zile kuu mpaka za mitaani ni vumbi tupu, tunawazeeshea watu magari yao utadhani wanafanya biashara kijijini, Vituo vya daladala ndo sasa usiseme ni full vumbi na makorongo.

Hivi inawapendeza sana waheshimiwa mkipita na magari yenu ya kifahari na ving'ora kwenye highway ya lanes mbili na tatu ambazo hamna hata mpango wa kuzitanua at least ziwe 6,8 au 12 kuondoa misongamano na overtakes zisizo na ulazima katika majiji yetu au mnawaona watanzania kama vile wapo usingizini na wala miji yao haiwaumi ikipitwa kwenye suala la miundombinu na vimiji vidogo vidogo kwenye nchi za jirani.

Hivi kwanini suala la ring roads, barabara pana, fly overs,taa za barabarani, n.k kwa miji yetu yote hata kama mkiamua kuanza na ile mikubwa hamuipi kipaumbele na wala hamuonekani kujishtukia kuwa kama nchi mnadumaza ukuaji mzuri wa miji na majiji pia mnatuchelewesha kimaendeleo, mnatufanya tuonekane hatuna maana mbele ya vinchi vichanga tudharaulike na kuonekana watanzania ni washamba na miji yao miundombinu yake haiendani na karne ya 21.

Ifikie wakati kama nchi masula ya miundombinu bora katika majiji yetu uwe ni ushindani wa kawaida na majiji yaliyoendelea zaidi duniani natuchukulie ni jambo la kawaida na siyo ufahari au kuhisi watanzania sote hatuna exposure,

hivyo inapotokea mkijenga kitu kidogo kama kidaraja cha juu cha waendao kwa miguu matangazo yanakuwa mengi na bado mnategemea tuwasifiwe kana kwamba hatukupaswa kuwa navyo ila kwa hisani mmeamua kutuzawadia vitu ambavyo si level zetu sijuhi huwa mnatuonaje.

Mlikuwa na mpango mzuri kabisa wa kuondoa vipanya(hiace) katika mzunguko wa jiji nabadala yake zitumike basi kubwa au coaster kama daladala na wananchi wa Mwanza walivyo wapenda maendeleo mwitikio ulikuwa mkubwa,

watu wakaanza kuingiza barabarani magari yao cha ajabu ruti zote mpaka leo zimebakia kusomeka nyashishi au airport no otherwise kwingineko miundombinu majanga nani ajitose kupeleka gari kwenye vumbi,milima na majabari akagongeshe gari kwenye mashimo na kudondosha vioo vya gari lake au kukata shock ups zake.

Hivi hata kutenga maeneo kadhaa ya wazi nakupanda miti,nyasi, kuweka mabenchi, swimming, sanamu, sinema au mabembea kuufanya mji uwe na bustani kadhaa za kupumzikia kuanzia CBD hadi mitaani
kupendezesha jiji pia ni mpaka mkumbushwe nyie mnaojihita mamlaka ya jiji.

Kuna ufahari gani kutembea ukiona maghorofa lakini huna pa kupumzikia matokeo yake tunajazana tukikaa kwenye msingi mbele ya geti la pamba sekondari utafikiri omba omba kumbe hatuna namna.

Leo hii unashuhudia kati kati ya jiji la Mwanza (CBD) mtu bado anapewa kibali na anafanya ujenzi wa nyumba ya chini(isiyo ya ghorofa) kwa ajili ya kuishi yeye na wapangaji wake tena around main roads sehemu ambazo ni promising sana na anaruhusiwa kuendelea na ujenzi wake bila bughudha vitu vinavyopelekea mwonekano mbovu wa sura ya jiji, hapo pembeni utashuhudia jumba la ghorofa 8 pembeni(chini yake) vibanda kama sita vyenye bati za kutu zimezingira.

Kuna maeneo kadhaa bado miundombinu ya maji ni shida na miundombinu mingi ya maji inajengwa kwa mwendo wa kuchechemea mno.

Itoshe kusema kuwa changamoto ni nyingi katika jiji hili ila chanzo kikuu ni SERIKALI naomba BADILIKENI.
JIJI LA MWANZA LINAUNDWA NA WILAYA NGAPI?
 
1. Sio kweli kwamba jiji la mwanza ni buzuruga tu ndio kuna mataa ya kuongozea magari.je wajua kwa sasa hadi kisesa kuna mataa ya kuongozea magari na watu pale njia panda ya kwenda kwenye makumbusho ya wasukuma bujora... pia igoma karibia na njia panda ya kishiri bila kusahau national changamoto ni bado hayajaanza kufanya kazi.

Mataa ya kuongozea magari na watu yaliyo maarufu zaidi ni

1. Mataa ya lumumba hapa zinakutana barabara tano
2.Mataa ya buzuruga hapa zinakutana barabara tatu
3.Mataa ya Ghana (kona ya bwiru) naweza Sema haya ndio mataa ya kisasa zaidi maana yanaonesha mpaka dakika
4.mataa ya pansiasi barabara ya airport+mjin na nyasaka inaenda kuunga kiloleni haya nayo ni mataa ya kisesa yanayoonyesha hadi dakika

Mpaka hapo nimeshakuonyesha ni jinsi gani umepotosha wananchi wa jf kiujumla mataa ya kuongozea magarina watu kwa jiji la mwanza yanafika 20+ ila ndio hivyo mengi hayajaanza kufanya kazi na mengine yanafanyakazi usiku tu
Nadhani alimaanisha taa za kuangaza majira ya giza ili mji uwe na nuru usiku
 
Kwa kwel ni jambo la aibu sanaa....ila yote yanasababishwa na mbunge wao mabulaa...yaan yeye hana muda na miundombinu...alikuja na issue ya taa za barabaran za kutumia solaa...cha ajabu nguzo za taa zimekaa muda mrefu hadi wananch wakaona zimesahaulika wakaamua kung'oa na kwenda kupma kweny vyma chakavu...nyingine zimekuwa ndo chanzo cha ajali barabarani kwan nyakat za usiku magari yanazigonga.,.hapa nmechukulia tu sehm ndogo ya igoma
Huyo mbunge wao, hata hajui kazi za mbunge ni nini, yapo yupo tu
 
Kwa kwel ni jambo la aibu sanaa....ila yote yanasababishwa na mbunge wao mabulaa...yaan yeye hana muda na miundombinu...alikuja na issue ya taa za barabaran za kutumia solaa...cha ajabu nguzo za taa zimekaa muda mrefu hadi wananch wakaona zimesahaulika wakaamua kung'oa na kwenda kupma kweny vyma chakavu...nyingine zimekuwa ndo chanzo cha ajali barabarani kwan nyakat za usiku magari yanazigonga.,.hapa nmechukulia tu sehm ndogo ya igoma
Huyo mbunge wao, hata hajui kazi za mbunge ni nini, yapo yupo tu
 
Jifunze kutofautisha maana ya neno slums na makazi ya kawaida yanayochukuliwa kuwa yakimasikini, bila kuelewa hilo kwanza sina haja ya kubishana tena,

hata hiyo dar pia hamna hizo slums kile tunachokiita uswazi kama manzese,mwananyamala,buguruni, kwa mnyamani n.k ni matokeo ya nyumba zilizojengwa katika mpangilio usio mzuri ila ni nyumba nzuri tu kwa kuishi mwanadamu na humo ndani yake watu wana fenicha kali tu, milo mitatu inapatikana na wanaishi poa.
Wewe ndio nyumba unakoishi au? Kwako hizo sio slums? Walioandika slums hawajui ila wewe..

Kwa hiyo hayo mabanda kwa sababu yamejengwa na tofari basi sio slums? Pole Sana.
 
Huyo mbunge wao, hata hajui kazi za mbunge ni nini, yapo yupo tu
Kanda ya ziwa hasa Mwanza ina wapigakura wapumbavu sana. Wabunge wa uko wengi shule ndogo ilimradi wawe na ng'ombe wengi na pesa. Kina Musukuma, yule wa Kahama na wengine wengi ni hopeless kichwani. Uganga mwingi, uwezo hafifu
 
Nadhani alimaanisha taa za kuangaza majira ya giza ili mji uwe na nuru usiku
Hapana soma vizuri... amesema mwanza inamataa ya kuongozea magari sehem moja tu pale kwenye junction ya buzuruga kitu ambacho sio kweli hata kidogo pia kuhusu mataa ya barabarani ni kweli kuanzia buhongwa had kisesa taa haziwaki ila taa za kuanzia busweru,kiseke,airport,buzuruga shule kupita nyasaka,maduka tisa,kiloleni,kilimahewa panda had mji mwema,isamilo shuka had nyakabungo hiii barabara ni mpya mkeka mtam sana bila kusahau njia ya kiloleni shuka kama unaenda msumbiji nyooka hadi pansiasi nk

Tatizo hii thread mhusika ameenda likizo sijui katembezwa wapi na wapi kaona jiji analijua kaanzisha na uzi ila wacha nimuache watu wa mwanza hatupendi kubishana hua tunawazoom tu wanavyopotosha uma
 
Umeandika huu uzi ukidhani utawashawishi wanamwanza waichukie CCM. Umejidanganya sana. Tafuta kazi ya kufanya.
Sawa kada mpuuzi nimekusikia, usilete pigo za kishamba zilizokosa uzalendo kwa Tanzania yetu, hapa tunazungumzia ni namna gani Mwanza itapiga hatua kimaendeleo, ukiona mmeguswa pabaya na yakwamba CCM ndo chanzo basi wazodoe hao wenzio mrekebishe mnapokosea siyo kuleta mikwara uchwara hapa.
 
Umeandika huu uzi ukidhani utawashawishi wanamwanza waichukie CCM. Umejidanganya sana. Tafuta kazi ya kufanya.
Jina lenyewe linasadifu kilichopo no matter tukizungumzia modernization ya jiji inakuuma, Kwanza kabla sijatafuta hiyo kazi, nikuulize wewe unayo? Kutwa ku-leak viatu vya mbweha wa kijani kibichi..kweli nzi ni nzi tu.
 
"kuhusu mataa ya barabarani ni kweli kuanzia buhongwa had kisesa taa haziwaki"
Hapana soma vizuri... amesema mwanza inamataa ya kuongozea magari sehem moja tu pale kwenye junction ya buzuruga kitu ambacho sio kweli hata kidogo pia kuhusu mataa ya barabarani ni kweli kuanzia buhongwa had kisesa taa haziwaki ila taa za kuanzia busweru,kiseke,airport,buzuruga shule kupita nyasaka,maduka tisa,kiloleni,kilimahewa panda had mji mwema,isamilo shuka had nyakabungo hiii barabara ni mpya mkeka mtam sana bila kusahau njia ya kiloleni shuka kama unaenda msumbiji nyooka hadi pansiasi nk

Tatizo hii thread mhusika ameenda likizo sijui katembezwa wapi na wapi kaona jiji analijua kaanzisha na uzi ila wacha nimuache watu wa mwanza hatupendi kubishana hua tunawazoom tu wanavyopotosha uma
Nimetumia maneno yako mwenyewe umekiri kuwa taa haziwaki huku mimi nashindilia kabisa siyo haziwaki tu bali hazipo,

hivi unaposemea barabara kuu au lango kuu la mji linalofungua mji kutoka na kuingia ambapo panapaswa kuwavutia watu na kuondoka na picha nzuri ya mandhari ya mwanza utaachaje kuitaja barabara ya nyegezi na ile ya buzuruga tu kisesa?

Nilifikiri ni mzalendo utatetea angalau barabara hii isiishie tu kuwekewa taa za barabarani bali itanuliwe kwa njia 4 mpaka 6 tokea usagara,buhongwa mpka mjini vivyo hivyo mpaka buzuruga na hatimaye kisesa kuondosha kabisa kero za misongamano na taswira mbaya ya jiji kulishwa na barabara ndogo ndogo kama kijijini,

hivyo njia hizi 4 au 6 ziende ziishie pale makutano ya bypass huku katikati wakiacha nafasi ya kujenga mbeleni BRT, instead unatetea uzembe hili wenye vitambi vyao wazidi tafuna kodi zetu bila kuzifanyia kazi.
 
Bora umemwelewesha maana anajiondoa ufahamu hili kuendelea kutetea uozo
"Bila aibu mmewaachia kazi yenu wanamwanza waishio milimani ndo wawashe taa za majumbani mwao ndo waupe mji mwangaza kisa magari yenu yanataa hivyo haina haja ya kuweka taa za kumulika barabara, eti Mwanza na fahari yake yote inabakia kuwa jiji la taa moja tena ya kuongozea magari pale buzuruga junction, Are we serious?"

hata aibu huoni chief? Soma hio paragraph vizuri mwanza ulienda kwa shangazi au mjomba eti jiji la taa moja ya kuongozea magari. Nipo hapa kuwanyoosha wapotoshaji kama wewe
 
Naomba ufungue hiyo link hapo chini uangalie kipindi ukiongozwa na akili na siyo tumbo ulikuwa ukilalamikia nini
Umeandika huu uzi ukidhani utawashawishi wanamwanza waichukie CCM. Umejidanganya sana. Tafuta kazi ya kufanya.
 
"Bila aibu mmewaachia kazi yenu wanamwanza waishio milimani ndo wawashe taa za majumbani mwao ndo waupe mji mwangaza kisa magari yenu yanataa hivyo haina haja ya kuweka taa za kumulika barabara, eti Mwanza na fahari yake yote inabakia kuwa jiji la taa moja tena ya kuongozea magari pale buzuruga junction, Are we serious?"

hata aibu huoni chief? Soma hio paragraph vizuri mwanza ulienda kwa shangazi au mjomba eti jiji la taa moja ya kuongozea magari. Nipo hapa kuwanyoosha wapotoshaji kama wewe
Hahahaaa, Ninachojua mimi ni kufikisha ujumbe kama fanani na ndo kazi ya fasihi.
 
JIJI LA MWANZA LINAUNDWA NA WILAYA NGAPI?
Mbona unatubebesha jukumu lako? kabla ya kutuuliza humu na kujaza servers za JF ulipaswa kujijibu mwenyewe, kwani shule ukwenda ndugu yetu mpaka utumie herufi kubwa kutuuliza maswali ya darasa la 4.
 
Back
Top Bottom