Serikali kutochapisha takwimu za kiuchumi: Ifahamu IMF

Tulivyofundishwa shuleni IMF na WB ni mikono ya ubeberu na hutumia mikopo au misaada ili kututawala. Waswahili husema baniani mbaya kiatu chake dawa. Na kipindi tulifundishwa fedha sio msingi wa maendeleo. Nilikuwa najiuliza saaana hivi kwa nini hawa mabwana kama ni mabeberu yaliyojaaa uhafidhina, kwa nini bado tunawakimbilia na kuwakaribisha kwa mbleko na bashasha?
Tuliwahi kuandamana kumpongeza Nyerere kwa kukataa kurudi nyuma ili tusigeuke kuwa jiwe. Nyimbo na mashairi ya kizalendo yalitungwa, na chamoto tulikipata. Mwishowe mzee akasema nang'atuka. Hawa jamaa sio wepesi kama tunavyojifariji, tusije tukaanza kushikana uchawi!
 
Under Article IV of its Articles of Agreement, the IMF is authorized to inspect the economic, financial and exchange-rate policies of its members to ensure a smooth-running international monetary system. ...
Sasa sisi kama wanachama tunatakiwa kukubali masharti haya!
je kuna nchi ambazo ziliwahi kujitoa IMF ?
 
Wanajidanganya na kukimbilia China lkn hawajui kuwa hata China wanawaheshimu hao wakubwa wa dunia
Moja ya kosa kubwa la JPM alianza kuwakamata wachina then akakorofishana na wazungu, sijui kama alikuwa anajua anachokifanya, nadhani akili yake ilimtuma akikusanya Kodi inatosha kuendesha nchi akasahau kumbe na biashara za ndani kaziua Kwa kuwafungia watu biashara na Kodi ikaanza kushuka, ameanza kuingilia watu kwenye biashara zao wengine wamenyanganywa pesa zao Kwa sababu tu account zao zinaonyesha Wana akiba kubwa, kuna makampuni yanapewa kesi zisizo za maana ili Tu yalipe fines, na ukiona hizi dalili jua ndio dalili za serikali kuishiwa.
Waziri wa fedha ameenda kuwabembeleza wafanyabiashara kariakoo warudi wakati anaambiwa bungeni kuwa anaenda kuuwa biashara alikuwa mbishi.
Watanzania wenzangu hawa watu kama waziri wa fedha, makatibu wakuu wizara ya fedha na hazina, gavana wa benki kuu lazima huko mbeleni baada ya mkuu kuondoka waje watujibu Kwa makosa waliofanya kwenye mifumo ya fedha na kuharibu biashara, na tusikubali visingizio vyao kwamba Rais kawatuma maana kama unaona rais amekosea na anakulazimisha Bora ujiuzuru watz watakuelewa lakini kuendelea kufanya makosa ukijua unakosea ni kulikosea taifa na taifa ni zaidi ya rais
 
Mkuu hawa IMF hawakutulazimisha sisi kuwa wanachama wao,tulijiunga wenyewe tena tukiwa na akili zetu timamu baada ya kujiridhisha na majibu ya hayo maswali yako uchwara na mengine,wakati huo nchi ikiongozwa na watu wenye akili zao na exposure za kutosha? Serikali hii iliyoamua kuwekeza kwenye uongo ndo shida,kinachotokea kwa IMF ndo hicho hicho kinatokea kwa Prof Assard,Sasa wewe Kama huoni tatizo kwenye serikali hii binafsii sijui tukusaidie vipi
Sidhani kama kuna mgonjwa wa akili atakaekuelewa mkuu
 
Nadhani tungewaona IMF wapumbavu kama maisha ya kawaida ya watu mtaani wapo safi wanakula bagga n.k kiwango cha pesa mfukoni zinatosha kununua mahitaji ya lazima tena tungeandama na kuchoma hata kila mahali palipo na neno Imf na sisi ni wazalendo halisi hatutaki ujinga wao. LAKINI sas imekuwa sawa na kumwaga mtoto wako supu ya kuku halafu mbele za wageni unajisifu kwa kusema wanakula kuku mitoto mijinga kama mimi nitakugomea mbele za wageni.
IMF inaweza kuwa sahihi kwa sababu indicators za UKATA zipo wazi
 
Unataka kunieleza ya kwamba serikali inashinikizwa kufanya vitu visivyo halali kwa lengo la manufaa ya hawa jamaa kwanza, na si 50/50
Wewe nchi masikini wb na IMF wakuonee wivu gani na Lindi lako la umasikini?? Chapa lapa uko
 
Yaani leo CCM inawaona IMF ni wabaya. Narubiri siku mtakapowapiga pin na World Bank ndiyo utakuwa wanzo wa safari ya Zimbabwe.
Na I swear hatutakubali, nawaona ccm ikilewa kama alivyofanya albashir na Mugabe, sincerely hatutakubali na apo ndo watajua kuwa watanzania huwa wakorofi
 
Kuna mjadala kwa sasa unaendelea kuhusu serikali kugoma kuruhusu kuchapisha taarifa za majadiliano ya kiuchumi yaliofanyika, baina ya serikali na wadau wa IMF takwimu zinaozoonyesha uchumi wa Tanzania kukua kwa 4% badala ya 7% ilotarajiwa.
sababu zimeelezwa katika tafiti

Mjadala huu ningependa uwe wenye tija ,kwa maana ya kulisaidia taifa,dhidi ya kitu kinachoitwa vita vya kiuchumi,

Sina uzoefu sana na masuala ya kiuchumi,ila naamini wachumi wabobezi wazalendo wa kitanzania kwani nia ya dhati kabisa watatueleza kama ni kweli,
kwa nini serikali imegoma kuruhusu kutolewa tafiti hizo,kuna faida zipi na hasara ipi kwa kuzitoa au kutozitoa.

Pia ningependa kufahamu historia ya IMF ,

1,kuanzishwa kwake

2,kusudio la kuanzishwa kwake

3,Malengo ya kuanzishwa kwake

4,uaminifu wa taarifa zake kwa wanachama,especially nchi zinazoinukia kiuchumi

5,kilicho nyuma ya pazia kuhusu shirika hili ambacho hatukielewi,ispokua wachumi wabobezi mnakielewa.

6,chombo hiki cha kimataifa hakiwezi tumika kama siraha kwa baadhi ya mataifa yasiokubaliana na baadhi ya sera?

7,kama nchi, inajinasuaje na hali hii?.maswali ni mengi lakini naamini wachumi wabobezi wazalendo wasio na mlengo wowote wanaweza kutusaidia kujifunza kupitia uzi huu.
Swali na hoja yako ni nzuri na tunahitaji kukubalina kwenye merits zaidi za kwanini Serikali imewakatalia IMF.
Hata JKN nae kuna wakati mwingi tu walizinguana na IMF wakati akiwa mkuu wa kaya.

Ili upata ufahamu kwa kimapana ukiweza tafuta kitabu cha Dead Aid na Dambisa Moyo

Dambisa ni mchumi (mzaliwa wa Zambia), graduate wa Harvard na Oxford. Kafanya kazi na world bank na anafanya kazi kama consultant kwenye uchumi.
Kwa uzoefu alionao juu ya IFM na WB, utajua kuwa hizi taasisi hazina nia ya kututoa kwenye umasikini.

Wakati zinaundwa sisi Africa hatukuwa sehemu ya uasisi. Vision yao behind the curtain na matendo yao hayana nia ya dhati kuona economic reforms model zinaondoa umasikini. Kwa tafiti alizofanya Dambisa ameweka wazi, viashiria vya umasikini vimeongezeka kwa kiasi kikubwa toka nchi nyingi za AFRICA zianze kufuata masharti yao.

So far, IMF na USA na EU; kwa kuingalia Congo DR kama mmoja wa beneficiaries wa economic development model za IFM, hali ni mbaya Congo DR at expense ya wao kukwapua Almasi, magogo, dhahabu, Cobalt huku wao (EU & USA) wakifaidika na kuuza silaha, vyakula kama maziwa, mayai, nyama, samaki. Hawataki Congo ijitegemee wazalishe chakula chao na kukua kiuchumi at expense of Congolese resources.

Dambisa wakati anachapisha kitabu chake, nakupa quote... "Remember that just thirty years ago Malawi, Burundi and Burkina Faso were economically ahead of China on a per capita income basis. A dramatic turnaround is always
possible....

Ili tutoke hapa, we got to adopt new economic models. Na njia rahisi ni kutumia key tools kama
Strategic economic intelligence,
Strategic business intelligence,
Strategic Competitive intelligence...
Kwa kutumia competitive advantage ya raw materials kuwa processed into consumables na kuuza moja kwa moja kwa consumers au kwa intermediaries. Iko namna ya kufanya.

Tuna jukumu la kushirikiana ili tufike huko. How, we got to think and work as team-players. Honestly, kuna namna hapa nchini tumegawanyika hasa kwenye miradi ya maendeleo yenye quick return on investment.
 
Ukipingana na WB na IMF jiandae kula nyasi ,mwalimu Nyerere yalimkuta haya, maisha hayakuwa rahisi,kupata vitu kwa foreni mpaka aliposalimu amri,haya mabeberu sio ya mchezomchezo
Na sakata hili ni moja ya jambo lililomlazimisha Mwalimu kukaa pembeni na kumpa Mwinyi nafasi
 
Back
Top Bottom