Serikali kutoa magari 700 kwa ajili ya Jeshi la Polisi nchini

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, inatarajia kutoa magari 700 ambayo yanatarajiwa kusambazwa katika wilaya na mikoa yote nchini kwa ajili ya kusaidia kukabiliana na vitendo vya uhalifu nchini.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Hamad Masauni, alisema hayo wakati akizindua kituo cha askari polisi wa majini na kukabidhi boti wilayani Chato mkoani Geita, itakayotumika kusaidia shughuli za ulinzi katika Ukanda wa Ziwa Victoria.

Masauni alieleza kuwa, Serikali imejipanga kupunguza tatizo la uhaba wa vitendea Kati na uchakavu wa vifaa vya Jeshi la Polisi kwa kununua magari ya kutosha.
IMG_6282.JPG

Ni vyema katika kipindi hiki ambacho Serikali ya Awamu ya Tano inaboresha utendaji kazi wa Jeshi la Polisi kwa kulipatia vitendea kazi, tukumbuke kuwa, katika kipindi kilichopita, Jeshi hilo lilijikuta linategemea waliokuwa wakiitwa wadau kwa kuomba mafuta ya magari ama kupeleka kwenye matengenezo. Hili suala lilikuwa la aibu na ndilo lililosababisha kuwepo kwa kundi la watu wasioshikwa na Polisi, licha ya wengi wao kuwa wahalifu wakubwa.

Uamuzi huu wa Serikali ni wa kupongeza, ila Serikali ijitahidi kuongeza kasma ya Ofisi za Ma-OCDs kwani bado ni ndogo mno, in fact ni kama nil hasa kwa Wilaya za pembezoni.
 
Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, inatarajia kutoa magari 700 ambayo yanatarajiwa kusambazwa katika wilaya na mikoa yote nchini kwa ajili ya kusaidia kukabiliana na vitendo vya uhalifu nchini...
mpango mkakati wa kuua upinzani unaendelea kwa kasi,ile ahadi ya kuvifutilia mbali vyama vya upinzani aliyosema ni lazima aitekeleze
 
Tunampongeza sana mh. Rais, yatumike kwa ajili ya kudhibiti wahalifu sio kunyanyasa wapinzani
 
Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, inatarajia kutoa magari 700 ambayo yanatarajiwa kusambazwa katika wilaya na mikoa yote nchini kwa ajili ya kusaidia kukabiliana na vitendo vya uhalifu nchini
Kuzibiti upinzani, watu milioni 40, thubutu kwa gari hata 2000
 
Hizo ndio zingekuwa Ambulance na zikasambazwa kweye Zahanati na Hospitali za wilaya na mikoa. CCM hii biashara yao ya kina Mtatiro, Mwita na wengine wala isingekuwa Ajenda yao kuu.
 
Ningewaona wamaana kama wangeongeza maslahi ya hao viumbe wao(askari)
 
Yanatolewa magari yote hayo kwenda kudhibiti upinzani??

Hiyo sababu nyingine iliyotolewa kuwa eti yanaenda kuzuia uhalifu ni geresha tupu!
 
Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, inatarajia kutoa magari 700 ambayo yanatarajiwa kusambazwa katika wilaya na mikoa yote nchini kwa ajili ya kusaidia kukabiliana na vitendo vya uhalifu nchini. Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Hamad Masauni, alisema hayo wakati akizindua kituo cha askari polisi wa majini na kukabidhi boti wilayani Chato mkoani Geita, itakayotumika kusaidia shughuli za ulinzi katika Ukanda wa Ziwa Victoria.
Masauni alieleza kuwa, Serikali imejipanga kupunguza tatizo la uhaba wa vitendea Kati na uchakavu wa vifaa vya Jeshi la Polisi kwa kununua magari ya kutosha.
View attachment 836379
Ni vyema katika kipindi hiki ambacho Serikali ya Awamu ya Tano inaboresha utendaji kazi wa Jeshi la Polisi kwa kulipatia vitendea kazi, tukumbuke kuwa, katika kipindi kilichopita, Jeshi hilo lilijikuta linategemea waliokuwa wakiitwa wadau kwa kuomba mafuta ya magari ama kupeleka kwenye matengenezo. Hili suala lilikuwa la aibu na ndilo lililosababisha kuwepo kwa kundi la watu wasioshikwa na Polisi, licha ya wengi wao kuwa wahalifu wakubwa.
Uamuzi huu wa Serikali ni wa kupongeza, ila Serikali ijitahidi kuongeza kasma ya Ofisi za Ma-OCDs kwani bado ni ndogo mno, in fact ni kama nil hasa kwa Wilaya za pembezoni.
Sawa, uchaguzi unakaribia na Chadema bado wapo.
 
Back
Top Bottom