Serikali kutekeleza maazimio ya bunge ni amri au hiari???

OSOKONI

JF-Expert Member
Oct 20, 2011
10,965
5,336
Wapendwa wana JF nianze kwa kuwatakia heri ya mwaka mpya 2012, pokeeni baraka za mungu kwenye mwaka huu.

Ninachotaka tujadili ni hiki hapa:
Bunge kwa maana yake ndicho chombo cha juu kabisa cha kuwakilisha wananchi, bunge linatunga sheria, linaisimamia serikali nakutenda yote kwa niaba ya wananchi, Kwa nyakati tofauti bunge limekuwa likitoa maazimio mbalimbali kwa serikali mfano kamati ya Dr. Mwakyembe ilitoa mapendekezo 23 kwa serikali kwa ajili ya utekelezaji mfano bunge liliagiza serikali kuwachukulia hatua za kisheria wote waliohusika na kashfa ile wakiwepo mawaziri waliojiuzulu, mwanasheria mkuu na Dr. Hosea na wengine wengi lakini serikali haikufanya hivo.

Hivi karibuni kwenye kashfa ya Jairo na wenzie Bunge limetoa maazimio kadhaa kwa serikali kwa utekelezaji ikiwepo kuwachukulia hatua za kisheria Jiaro, Luhanjo, Ngeleja. CAG na wengine wote waliohusika serikali haijachukua wala haionyeshi dalili za kutekeleza, sasa pointi yangu ya mjadala ni hii utekelezaji wa maazimio ya bunge na serikali huwa ni lazima au serikali ina uhuru wa kutekeleza au kutokutekeleza??

Na je pale serikali kwa kiburi chake inapokataa kutekeleza maazimio ya bunge ambalo ndio sauti ya wananchi walioiweka madrakani serikali ni nini kinachotakiwa kufanywa na bunge??

Nawasilisha
 
Hata mimi hilo swali huwa najiuliza lakini nimeona mapendekezo ya kamati za bungr zinazoundwa si lazima itekeleze kama yalivyoletwa.

Na ndiyo maana Luhanjo na wenzake hawajachukuliwa hatua yoyote ile ukiachilia sakata la Dowans.
 
Huo ni ubabe wa serikali walitakiwa watekeleze maazimio ya Bunge,tatizo hapa Bunge letu lenyewe imekua kama taasisi ya serikali kwa sababu ya kuwepo wabunge wengi wa chama tawala,wananchi tuikatae ccm ili Bunge letu lipata nguvu ya kuidhiti serikali.
 
Nawashauri wabunge waachane na mijadala yooote kipindi kijacho cha bunge ili swali lako lipate jibu mwafaka....Lakini kwa vile hili ni bunge la posho hili halitowezekana. Wamegeuzwa kijiwe cha Ghahawa!
 
Hata mimi hilo swali huwa najiuliza lakini nimeona mapendekezo ya kamati za bungr zinazoundwa si lazima itekeleze kama yalivyoletwa.

Na ndiyo maana Luhanjo na wenzake hawajachukuliwa hatua yoyote ile ukiachilia sakata la Dowans.
Mkuu kuna Maazimio na Mapendekezo. Kama ni mapendekezo serikali inaweza kutekeleza ama kutotekeleza lakini hili la maazimio nadhani serikali inatakiwa itekeleze!
 
Nawashauri wabunge waachane na mijadala yooote kipindi kijacho cha bunge ili swali lako lipate jibu mwafaka....Lakini kwa vile hili ni bunge la posho hili halitowezekana. Wamegeuzwa kijiwe cha Ghahawa!
Mkuu hili nalo ni neno la kufanyia kazi. Kama maazimio hayatekelezwi basi kuna haja gani ya kuunda Tume Teule za Bunge ambazo tija yake haionekani?
 
Back
Top Bottom