kwani jiwe aliajiri wale walimu wote aliosema?
na hii ni yale yale tu...........
 
Kati ya mawaziri siwapi credit kabisa basi ni huyu, yai wameshindwa kuwa wabunifu kutengeza ajira kweli, mpaka wanatoa ajira kama bonus utafikiri sio haki kuwatengezea ajira Watanzania
Waziri Mzigo
 
Hatuwezi kutengeneza ajira za mambo mengine zaidi ya hayo.

Viongozi tujifunze kufikiria, hizo ajira za afya na elimu haziko related na investment.

Tujitahidi kwenda na uchumi halisi tuwekeze, tutengeneze ajira zinatokana na uwekezaji. Huo ndio uchumi.
 
tumegeuzwa joyce wowo inatuchezesha akili mpaka miaka hii.mambo kama haya yangekuwa sio kupoteza mda bungeni.sasa wanaboresha nini wanayo jinadi nayo kila siku .sijui elimu,afya na mengine
 
Watu mwaka jana wakajipinda tuma maombi wizara...maombi tamisemi mwisho wa siku wakaajiriwa watu 20 Ajira walizoahidi 2000 sina hamu aisee sema ngoja tuonee
 
Nyie @Mods Bora huu Uzi wangu muufute tu kuliko kuunganisha na Uzi mwingine, yaan simaindi kabisa huu upuuzi,, kama vp futeni tu uzi wangu nilisticky kwenye jambo jingine na sio kutangaza Ajira kama mlikoupeleka.. mods mnamambo za ajabu sana👺👺
 
Waziri Jenister Mhagama akitoa kauli ya Serikali bungeni kuhusu upungufu wa watumishi nchini, amesema Rais ameridhia na kutoa kibali cha kuajiri watumishi 30,000 na wiki ijayo atazitangaza.

Waziri Jenister Muhagama: Nasimama hapa kwa heshima kubwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninaomba niwaarifu waheshimiwa wabunge, mheshimiwa Rais na Serikali yake wametambua tatizo hili la uhaba wa watumishi na hasa kwenye miradi ya sekta ya afya na sekta ya elimu na hivyo basi, mheshimiwa Rais ametoa kibali, ahadi ya Serikali katika mwaka huu wa fedha ilikuwa tuajiri watumishi elfu 44.

Tayari Serikali ilikwisha kuajiri watumishi wapya na watumishi wa ajira mbadala 12,000. Niwathibitishie wabunge, mheshimiwa Rais ameridhia na wiki ijayo nitatoa tangazo Rasmi la ajira 32,000 na utaratibu wa ajira hizo na mgawanyo wake katika sekta ambazo zinaongoza kwa uhaba wa watumishi, maelezo yote nitayatoa wiki ijayo.

===========================

Serikali imeyangaza kuwa itataoa ajira za watumishi 32,000 ambapo miradi ya afya na sekta ya elimu ndiyo watakaokuwa wanufaika wakubwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Jenista Mhagama ameyasema hayo Bungeni leo Aprili 6, 2022.

“Kumekuwa na hofu kuhusu sekta ya elimu na afya, naomba niwaarifu kuwa Rais na Serikali yake wametambua tatizo la uhaba wa watumishi hasa kwenye miradi ya afya na sekta elimu, ahadi ya Serikali kwa mwaka huu wa fedha ilikuwa tuajiri watumishi 44,000.

“Tayari Serikali imeshapitisha watumishi wapya 12,000, naomba niwathibitishie kuwa Rais ameridhia na wiki ijayo tutatoa tangazo la ajira 32,000 mpya. Utaratibu na mgawanyo wake, maelezo yote nitayatoa wiki ijayo,” – Jenista Muhagama.
Hao 12000 waliajiriwa linu?
 
-Serikali kwenye hilo tamko, kuhusu mishahara ambayo iliwekwa kwenye bajeti ya miezi 10 au 11 kwa watumishi wapya 32,000 watakaoajiriwa Mwezi wa tano au sita.
-Kwenye bajeti ya 2021/22 Serikali iweka mishahara ya waajiriwa wapya 44,000 ya miezi 12,
-labda Serikali ituambie kuwa , Watumishi 12,000 ndiyo walitengewa bajeti miezi 12 na hao 32,000 walitengewa bajeti ya miezi 2 au 1.
-serikali imeokoa(Save) mishahara ya miezi 10 na zaidi kwa kuchelewa kuajiri

Ushauri

-bajeti ya mishahara ya watumishi 32,000 ambayo haikulipwa,zitolewe Kama ruzuku kwa waagizaji wa bidhaa za petrol,ili kupunguza makali ya maisha.
-Mchakato wa ajira ufanyike haraka, kuepuka bajeti hiyo ya mishahara kuwa frozen tunakaribia mwisho wa mwaka wa fedha 2021/22.
-CAG afanye performance audit,na Waziri mwenye majukumu ya ajira Serikali awajibike kwa kuchelewesha mchakato
 
Sisi ambao tunazururazurura Huku Halmashauri nyingi na wakuu wa idara tunaelewa.. wewe hujui lolote, So usinisumbue mkuu kama hutaki pita kushoto na sikulazimishi ukubali nikisemacho
Vijana wa siku hizi mna shida, kama ww unazurura Halmashauri ndio unajua kila kitu ?! Kwann usijibu swali nililokuuliza ?!

Tujibiane kwa hoja, maana wote hatujuani. Tumekutana J

Ujuaji ni moja ya sababu ya vijana wengi kuendelea kukaa mitaani,
 
Nazani hata mwezi haujaisha tangu Mama aseme hivi.
20220407_092454.jpg
 
Back
Top Bottom