Serikali kusaini mikataba ya madini na makampuni

mwengeso

JF-Expert Member
Nov 27, 2014
9,219
6,650
Nimeisikia muda huu kupitia channel Ten Waziri mhusika akilisema hilo. Faida alizozitaja (pato kwa Serikali na Ajira) hazihakisi thamani ya madini ambayo ni "non-renewable natural resource). Watachimba na kuacha mashimo (uchumi usio endelevu)

Kama Serikali ina nia ya dhati ya nchi kuwa na uchumi endelevu iweke mazingira rafiki ya uwekezaji kwenye kilimo na uchumi wa bluu. Nchi ina ardhi ya kutosha yenye rutuba pia ina mito, maziwa kwa ajili ya uvuvi na umwagiliaji.

Vilevile ina ukanda wa bahari wa kuwezesha uvuvi. Sekta ya kilimo na uvuvi siyo tu zitaongeza nafasi za ajira bali zitatoa nafasi kwa ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani ya mazao yake.
 
Kuna mapori mengi, kila mmoja wetu aanze kumiliki ekari 20 na aanze kulima mazao ya biashara kwa faida yake na familia yake, kuna maeneo ekari moja ni shilingi 50,000 au chini ya hapo. Tuanze kazi
 
Polepole yupo na wananchi ndiyo maana viewers ni wengi sana kwake .

Nape na Makamba wanajulikana ni timu msoga ( wapigaji)
Siasa ni sanaa kwa sababu haina systematic way, ndio maana inafundishwa vyuoni. Nitabuni namna ya kuteka mawazo yako ili nitimize lengo langu. ndivyo siasa ilivyo.
 
Polepole yupo na wananchi ndiyo maana viewers ni wengi sana kwake .

Nape na Makamba wanajulikana ni timu msoga ( wapigaji)
Kama alivyosema Polepole Wahuni bado wako Serikali.

Wahuni wanatengeneza matabaka ya walio nacho na wasio. Wakati Vibaka wanasukumwa gerezani, mafisadi wanafutiwa mashitaka na kulindwa. Wafanya biashara ndogondogo aka Machinga wanatengenezewa mazingira magumu ya kufanya biashara wakati wenye nacho wanapewa nafasi ya kufanya Taifa shamba la bibi.

Jana tumeshuhudia ati wachimba madini, maliasili isiyodumu (non-renewable natural resource), wakitia sahihi mikataba mbele ya Rais kwa kile kinachodaiwa kuwa ni UWAZI!!!!
 
Back
Top Bottom