Serikali kupitia simu za mkononi, inaweza kukusanya fedha na kuanzisha Mfuko(Fund) wa kugharamia Bima ya Afya na Elimu ya Juu kwa Watanzania wote

Mkuu tatizo nchi watu wana roho mbaya,wivu,wezi na wanakula hadi rambi rambi.Ingekuwa sio hivyo tungekuwa mbali sana kama taifa
 
Yaani mnawaza kuwanyonya wananchi tu sio...
Watanzania kwa mentality hizi,tutabaki kuwa masikini na kubaki nyuma.

Hiyo mia tano kwa mwezi unaweza kuiona ni nyingi, ila jiulize unatumia kiasi gani kwenye kununua airtime za kawaida au unatumia kiasi gani kunywa pombe au kununua vitu kama soda na vitu vingine vya aina hiyo kwa siku.
 
Ndio maana napendekeza njia hiyo kugharamia Bima ya Afya,kwani licha ya swala la Bima kuwa ni muhimu,ila watu watalipa pasipo kuhisi maumivu, na zaidi zitapatkana hela nyingi zaidi zinazoweza kuelekezwa kwenye maeneo mengne ya kugharamia huduma za kijamii kama elimu.
... halafu hao hao wanaenda kuzibadilisha matumizi. Zitaelekezwa kwenye manunuzi sijui ujenzi wa nini sijui a lot of white elephant projects. Zitatumika kumtukuza bwana yule na genge lake. Zitawekewa vikokotoo na kila aina ya mizengwe ili watu wakose au wapunguziwe haki zao.

Mara hii tumesahau wazee wetu wanavyoteseka kupata haki zao hifadhi ya jamii? Wazo zuri ila sio chini ya mboga mboga kwa kweli!
 
Dah!.. gharama za mawasiliano zitaongezeka likitekelezwa hili itabidi hata hizo vocha ziuzwe 600 au 700 badala ya 500.
 
Hiyo ni Bima kwa ajili ya Afya yako na inaweza isiwe lazima.Kumbuka watanzania wengi hawana Bima ya Afya na wako watu wanakufa kwa kukosa fedha za matibabu.Sasa kipi bora?
Najaribu kufikiria mtu achangie sh. 6000 kwa mwaka ( 500×12) na atibiwe "bure" wakati wowote atakapougua.....!! Aisee kweli bima ni mchezo wa kamali....!!
 
Kwa kawaida,unapokuja na wazo au kitu kigeni,watanzania huwa ni wagumu kukielewa/kukipokea na huchukua muda kukikubali na kukizoea kwahiyo sikushangai.
Kwa mtizamo wangu suala la jero hero Ni usumbufu, Kama zilivyofutwa road license zikaingizwa kwenye mafuta, Kama ilivyoanzishwa RDL railway development Levy on importation, ianzishwe Kodi ya bima ya lazima, na mfuko maalum wa kulea WATOTO walio mazingira hatarishi.ikiwa utakuwa 3% ya airtime charge maana yake ukiweka jero Kila siku kwa mwezi utachangia 450, Sasa hapo wapi watakoutumia mpaka 300,000 huyu atanikuta kachanhia 9000.
Ukweli Ni kwamba muda mwingi tunaotumia kwenye simu sio for economic productions, mostly for social reasons
 
Sipingi wazo lako mkuu ila najaribu kufikiri tu, kwa ikivyo sasa, NHIF inakusanya kwa uchache kabisa sh 54,000 kwa mwaka, na mpaka sh 1,500,000 kwa kiwango cha juu, sasa kwa idadi ile ile ya wachangiaji, inashindwa kutoa huduma ya afya kwa ubora unaostahiki, unadhani nini kinawashinda hawa wa sasa na kipi cha tofauti kitafanyika kwa hili wazo?

Hifadhi ya jamii ni moja ya mifano ya kuonesha kuwa, ilimradi utahusisha serikali na uendeshaji wa wazo lenyewe, basi mkwamo hauepukiki.

Na kuna mdau ameuliza kama takwimu ya wamiliki wa simu iko sawa? Na akasema kama iko sawa, inabidi ufanyike udadisi, kwakuwa asilimia 50 ya idadi ya watu wa TZ amesema ni watoto chini ya 18, ambapo TZ wanasema tuko takribani milioni 60.

VAT, PAYE na nyinginezo zitoshe kufanya jambo hilo. Tuanze na wale wenye exemption za kodi na wafananao, tuone tutapata ngapi toka maeneo hayo kisha tukimalizana na loose ends zote, ndo tufukirie kumkamua huyo ng'ombe anayekaribia kutoa damu.
 
Habari wadau,

Leo nimekaa na kutafakari sana juu ya uwezekano wa laini za simu tunazotumia katika simu zetu kutumika kukusanya fedha zinazoweza kugharamia matibabu ya karibu kila mtanzania na pia kukusanya fedha zinazoweza kutumika kugharamia Elimu ya juu.

Kwanini simu ya mkononi kupitia laini ya simu iliyosajiliwa?
Kulingana na Ripoti ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, hadi kufikia mwezi December mwaka 2017,watanzania wapatao milioni 40 wanatumia simu za mkononi, idadi hii ikiwa ni kutoka watumiaji milioni 27.62 mwaka 2012 hivyo tunaweza kupata fedha nyingi nazingine tukazielekeza katika maeneo mengine.Pia,tusisahau idadi ya watumiaji wa simu itaendelea kuongezeka kila mwaka.

Tunaweza kukusanya fedha kiasi gani kufanikisha jambo hili kulingana na takwimu hizo?
Ni rahisi tu. Kwa mfano,ikakubaliwa na kupitishwa kuwa kila mwananchama atapaswa kuchanga shilingi miatano tu tu(500/=) kwa mwezi kupitia line yake ya simu(simu ya mkononi)

Sasa chukua 40,000,0000 x 500=20,000,000,000(Bilioni 20) na hii ni kwa mwezi mmoja tu.

Kwa mwaka maana yake ni 20,000,000,000 x12=240,000,000,000(Biloni 240).

Sasa wadau tujiulize,kwa fedha yote hii kwa mwaka,swala la kuwa na Bima ya Afya itakayohudumia kla mtanzani litashindikana na hata kiasi kingiine cha fedha kutumika kwa mambo mengine kama kuanzisha mfuko wa kugharamia elimu ya juu au fedha hizo kutumika pia kuboresha huduma za afya kama ujenzi wa vituo vya afya na mahospitali?


https://www.google.com/url?sa=t&rct=j&q=&esrc=s&source=web&cd=&cad=rja&uact=8&ved=2ahUKEwiz4PSC-KfsAhXj1uAKHVM6ARIQFjAHegQIChAC&url=https://www.pressreader.com/tanzania/mtanzania/20190630/281603832012081&usg=AOvVaw1tWi_hNU4DeItvAHpXM6AH

Kwa maana hiyo na kulingana na ongezeko hilo,mwaka huu wa 2020, idadi hiyo ya watumiaji milioni 40 itakuwa imeongezeka zaidi ya hapo.

Nini kinaweza kufanyika kufanikisha wazo hili?
Kinachoweza kufanyia ni serikali, kupitia Mamlaka ya Mawasiliano nchini(TCRA) ikishirkiana na makampuni ya simu za mkononi, kuanzisha tozo maalumu kwa asilimia ya kila muda wa maongezi mtumiaji wa simu anaponunua airtime au kuanzisha vocha maalumu zitazoingizwa kama vocha za kawaida za simu ila hela itayopatikana inaingia moja kwa moja serikalini na makampuni ya simu yanaweza kulipwa aslimia fulani kama maliupo ya kazi ya uwakala wa kukusanya mapato hayo.

Kutoza kwa asilimia kwa kila muda wa maongezi(airtime) utaonunuliwa
Kinachoweza kufanyika ni wataalamu walioko serikalini(watu wa Bima ya Afya na wadau wengineo) kukaa chini na kuangalia gharama halisi ambayomkila mwannchi anaemilki simu(kulingana na idasdi iliyopo) anaweza kuchangia kupitia manunuzi ya airtime anunuapo muda wa maongezi. Hapa namanisha wataalamu wakishakaa chini na kupiga mahesanu yao,wanaweza kuamua/kupendekeza asilimia ya makato kwa kila manunuzi ya airtime yanayofanyika.

Kwa maana hiyo, gharama ya kila vocha pamoja na muda wa mangezi kwa njia ya kurusha, zinaweza kuongezwa kidogo ili kuweza kupata/kuksanya makato hayo na kuyapeleka serikalini, na asilimia fulani kubaki katka kampuni husika ya simu kama malipo ya uwakala wa kukusanya mapato hayo ya serikali.

Kuanzisha vocha maalumu kwa ajili ya kuchangia huduma hii
Hili pengine linaweza kuwa ni wazo zuri zaidi kuliko hilo hapo juu.Katika hili,serikali kwa kushirikiana na makampuni ya simu, wataandaa vocha maalumu(labda ya shilingi 100,200,300 au 500 kutokana na itavyoonekana inafaa) na mtumiaji wa simu kununua vocha hizo na kuziingiza kama anavyongiza vocha za muda wa maongezim ila fedha inayopatikana itapelekwa serkalini na kampuni huska ya simu.

Wanachoeza kufanya makampuni ya simu ni kuongeza option ya malipo haya katika "menu" zao(kama inawezeka kitaalamu kulingana na teknolojia iliyopo) ili kutenganisha malipo au manunuzi ya vocha za kawaida na hizo vocha mpya.

Namna gani fedha zinaweza kutozwa?
Kwasababu kila line ya simu imesajiliwa na bila shaka kuna database, wataalamu wanaweza kuamua ni namna gani watu watozwe(iwe ni kila anaponunua airtime kama watatozo kwa kuchaji asilimia fulani kila unaponunua airtime au atozwe mara moja kwa mwezi,mara mbili au vinginevyo).

Hapa namanisha kuwa,kwasababun kila line ya simu imesajiliwa jina moja,mtu huyo akishanunua vocha na kufikisha kiwango kilichopangwa kwa mwezi, system haitamkata tena hela anaponunua airtime nyingine ndani ya mwezi husiku(kama itakuwa ni kulipia kwa mwezi).

Kwa wenye line zaidi ya moja itakuwaje?
Kwanza lazima ieleweke kuwa,wananchi watakaoukuwa teyari kwa huduma hii ya Bima,watapaswa kusajiliwa wao pamoja na line za simu watazopendelea zitumike kwa kulipia huduma hii za simu zitakazotumika kwa huduma hii na hivyo kuondoa uwezekana wa mtu kuchajiwa kwa kila line anayomiliki.

Kwa kununua vocha maalumu, mtumiaji wa simu anaweza pia kutumia line ya simu iliyosajiliwa kutumika katika kulipia huduma hii kulipia michango yake yake ya Bima.

Namna gani watumiaji wa huduma hii watatambulika katika mahosipitali na katika vituo vya afya?
Kwasababu huduma hii itakuwa inaendeshwa kielektroniki, zinzaweza kuandaliwa kadi za kielektoniki ambazo kila mtumiaji atapewa kama kadi yake ya utambulisho, kadi ambazo zitapaswa kutambuliwa na vifaa maalumu vitavyopatikana katika hospitali na vituo husika vya afya nchi nzima.

Kadi hii, licha ya kumtambulisha mwanachama,bado inaweza pia kubeba taarifa zake zote zikiwemo taarifa za michango yake na pia kueleza kama ametimiza vigezo na mashariti yote ya kuhudumiwa na Mfuko utakaoanzishwa kulinga na sheria itayounda Mfuko huo.

Kwanini ni muhimu kuwa na Mfuko wa aina hii licha ya gharama zitazoongezeka kwa watumiaji wa simu?
Ni ukweli ulio wazi kuwa Bima ya Afya ni jambo muhimu sana kwani magonjwa huja bila kujali una fedha au huna huku magonjwa mengine gharama zake zikiwa ni juu kuliko uwezo wa watanzania walio wengi hivyo ni bora kutozwa hizo gharama ndogo ili hata unapougua usishindwe kuhudumiwa kwa kukosa fedha.

Na kama tunazotozwa fedha kila tunaponunua vitu vitu/bidhaa kama umeme kuendeshea taasisi kama EWURA au REA wanaohusika na usambazaji umeme vijijini kuna ubaya gani tukatozwa fedha kidogo kupitia simu zote za mkonono kwa ajili ya afya zetu au kugharamia elimu za watoto wetu?

Pia, unaweza kuona hiyo miatano(500/=) na nyingi lakini jiulize kwa mwezi unatumia kiasi gani kuweka kwenye simu yako na kuwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki tena sometimes kuwasalimia tu.Pia jiulize ni kiasi gani unakatwa kulipia deni la Bodi ya Mikopo kila mwezi alafu ndio uone kama hiyo 500 au 300 kwa mwezi inaweza kuwa ni nyingi, na pia jiulize ni kiasi gani unaweza kukopa mkopo wa riba kugharamia matibabu yako,ya mwanao au ya mzazi wako kule kijijini au aliekuja nyumbani kwako(mjini) kwa ajili ya matibabu.

Kuunda Mfuko(Fund) husika

Wataalamu na wadau wote wanaohusika wakiona jambo hili linawezekana, basi watapeleka mapendekezo yao serikalini kwa ajili ya utekeleazaji ambapo serikali itapaswa kuandaa sera na sheria itayotumika kuanzisha na kusimamia uendeshaji wa Mfuko huu.

Sheria inaweza kuweje?
Hii ni kazi ya wataalamu ila pamoja na mambo mengine,sheria inaweza kutamka kuwa ni lazima kila mtanzania mwenye kumliki line ya simu ajiunge na huduma hii au iwe ni hiari ya mtu(ni vizuri iwe hiari lakini itafaa zaidi fedha zitazokusaywa zitumike pia katika kuhamasisha watu wajiunge na Mfuko huu na pia zitumike kutoa elimu kwa umma juu ya umuhimu wa kuwa na Bima ya Afya kupitia semina,makongamono,matangazo katika vyombo vya habari,n.k).

Kwa kila mchangiaji mwenye watoto au tegemezi,sheria itamke wazi ni watoto au ni wategemezi wangapi wanaweza kunufaika na huduma hiyo.

Pia,sheria itakayounda Mfuko huu, imtake kila mwanachama, kueleza ni i nani ataotaka wafaidike kupitia michango yake kwenye mfuko husika.

Usalama wa Mfuko
Ili kuzuia serikali kuingilia utendaji wa Mfuko huu, na pia ili kuufanya Mfuko uwe huru kwa lengo la kufanya wanasiasa wasiwe na mamlaka juu ya uendeshaji wa huu Mfuko huu, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huu asiteuliwe na Raisi ,na pia sheria itamke bayana kuwa serikali hairuhusiwi kukopa kutoka katika huu Mfuko isipokuwa panapotokea dharura maalumu kama vile kukabiliana na madhara yaliyosababishwa na majanga ya asili au nchi inapoingia katika vita ,n.k.

Faida nyingine za kuanzishwa kwa Mfuko/tozo ya aina hii

Wafanyakazi/Waajiriwa, hawatalazimika tena kukatwa hela(maelfu kadhaa ya shlingi) kutoka kwenye mishahara yao kila mwezi kwa ajili ya kuchangia Bima ya Afya ya Taifa na hivyo wataokoa fedha na kupuguza wingi/mzigo wa makato katika mishahara yao.

Watanzania wengi hata wale wasio na ajira za kuelewaka/rasimi, wanaweza kupata Bima ya Afya kwa kumiliki tu simu ya mkononi.

Makusanyo haya yanaeweza pia kutumiwa kugharamia elimu ya juu na kusomesha watanzania wote bila kuwa na element za kubaguana na hata kuwezessha elimu bure mpaka vyuo vikuu.

Kuanzishwa kwa chombo kama hiki, pia kutatengeneza fursa za ajira kwa watanzania watakaojiriwa katika Mfuko huu,makampuni ya simu yataongeza faida na hivyo yatalipa kodi zaidi serkalini ,na pia uuzaji wa vocha hizi maalumu nao utatoa ajira kwa vijana wataojihusisha na biasharan hii,n.k.

Hasara zinazoweza kujitokeza

Binafsi sioni hasara yoyote katika kuanzisha Mfuko kama huu.

Yangu ni hayo,mnaweza kuboresha au kukosa pale ambapo nimekosea kwani naamini humu wamo watu wa fani za aina nyingi hivyo kuna wenye kuweza kuwa na mawazo bora zaidi kulingana na fani zao.

Tusisahau hata vitu kama Mpesa na tigo pesa vilibuniwa na watu, hivyo hata na sisi tunawza kubuni vya kwetu na wengine wakaiga.
Tujaalie bima hiyo iwe ni kwa wazee na watoto pekee. Ambapo idadi hao ni kama watu mil 30. Kwa bil 240 maana yake kila mfaidika analipa shs 8000 kwa mwaka. Hakuna bima ya afya ya kiasi hicho. Kwa Leo ninatofautiana Na wewe
 
Tembo,Simba mlima Kilimanjaro upo tuu wazungu wanataka walipie waangalie ninyi mmeweka Kodi kubwa kwa magari wanayopanda kuangalia wanyama wanaishia kupata magari mabovu na wakisimuliana hawarudi tena baada ya kupunguza Kodi ya Land Cruiser ili kuboresha mazingira mnataka tena kujibana hata ninyi msipigiane simu vocha tuu zina VAT bado hujaamisha fedha...
 
Habari wadau,

Leo nimekaa na kutafakari sana juu ya uwezekano wa laini za simu tunazotumia katika simu zetu kutumika kukusanya fedha zinazoweza kugharamia matibabu ya karibu kila mtanzania na pia kukusanya fedha zinazoweza kutumika kugharamia Elimu ya juu.

Kwanini simu ya mkononi kupitia laini ya simu iliyosajiliwa?
Kulingana na Ripoti ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, hadi kufikia mwezi December mwaka 2017,watanzania wapatao milioni 40 wanatumia simu za mkononi, idadi hii ikiwa ni kutoka watumiaji milioni 27.62 mwaka 2012 hivyo tunaweza kupata fedha nyingi nazingine tukazielekeza katika maeneo mengine.Pia,tusisahau idadi ya watumiaji wa simu itaendelea kuongezeka kila mwaka.

Tunaweza kukusanya fedha kiasi gani kufanikisha jambo hili kulingana na takwimu hizo?
Ni rahisi tu. Kwa mfano,ikakubaliwa na kupitishwa kuwa kila mwananchama atapaswa kuchanga shilingi miatano tu tu(500/=) kwa mwezi kupitia line yake ya simu(simu ya mkononi)

Sasa chukua 40,000,0000 x 500=20,000,000,000(Bilioni 20) na hii ni kwa mwezi mmoja tu.

Kwa mwaka maana yake ni 20,000,000,000 x12=240,000,000,000(Biloni 240).

Sasa wadau tujiulize,kwa fedha yote hii kwa mwaka,swala la kuwa na Bima ya Afya itakayohudumia kla mtanzani litashindikana na hata kiasi kingiine cha fedha kutumika kwa mambo mengine kama kuanzisha mfuko wa kugharamia elimu ya juu au fedha hizo kutumika pia kuboresha huduma za afya kama ujenzi wa vituo vya afya na mahospitali?


https://www.google.com/url?sa=t&rct=j&q=&esrc=s&source=web&cd=&cad=rja&uact=8&ved=2ahUKEwiz4PSC-KfsAhXj1uAKHVM6ARIQFjAHegQIChAC&url=https://www.pressreader.com/tanzania/mtanzania/20190630/281603832012081&usg=AOvVaw1tWi_hNU4DeItvAHpXM6AH

Kwa maana hiyo na kulingana na ongezeko hilo,mwaka huu wa 2020, idadi hiyo ya watumiaji milioni 40 itakuwa imeongezeka zaidi ya hapo.

Nini kinaweza kufanyika kufanikisha wazo hili?
Kinachoweza kufanyia ni serikali, kupitia Mamlaka ya Mawasiliano nchini(TCRA) ikishirkiana na makampuni ya simu za mkononi, kuanzisha tozo maalumu kwa asilimia ya kila muda wa maongezi mtumiaji wa simu anaponunua airtime au kuanzisha vocha maalumu zitazoingizwa kama vocha za kawaida za simu ila hela itayopatikana inaingia moja kwa moja serikalini na makampuni ya simu yanaweza kulipwa aslimia fulani kama maliupo ya kazi ya uwakala wa kukusanya mapato hayo.

Kutoza kwa asilimia kwa kila muda wa maongezi(airtime) utaonunuliwa
Kinachoweza kufanyika ni wataalamu walioko serikalini(watu wa Bima ya Afya na wadau wengineo) kukaa chini na kuangalia gharama halisi ambayomkila mwannchi anaemilki simu(kulingana na idasdi iliyopo) anaweza kuchangia kupitia manunuzi ya airtime anunuapo muda wa maongezi. Hapa namanisha wataalamu wakishakaa chini na kupiga mahesanu yao,wanaweza kuamua/kupendekeza asilimia ya makato kwa kila manunuzi ya airtime yanayofanyika.

Kwa maana hiyo, gharama ya kila vocha pamoja na muda wa mangezi kwa njia ya kurusha, zinaweza kuongezwa kidogo ili kuweza kupata/kuksanya makato hayo na kuyapeleka serikalini, na asilimia fulani kubaki katka kampuni husika ya simu kama malipo ya uwakala wa kukusanya mapato hayo ya serikali.

Kuanzisha vocha maalumu kwa ajili ya kuchangia huduma hii
Hili pengine linaweza kuwa ni wazo zuri zaidi kuliko hilo hapo juu.Katika hili,serikali kwa kushirikiana na makampuni ya simu, wataandaa vocha maalumu(labda ya shilingi 100,200,300 au 500 kutokana na itavyoonekana inafaa) na mtumiaji wa simu kununua vocha hizo na kuziingiza kama anavyongiza vocha za muda wa maongezim ila fedha inayopatikana itapelekwa serkalini na kampuni huska ya simu.

Wanachoeza kufanya makampuni ya simu ni kuongeza option ya malipo haya katika "menu" zao(kama inawezeka kitaalamu kulingana na teknolojia iliyopo) ili kutenganisha malipo au manunuzi ya vocha za kawaida na hizo vocha mpya.

Namna gani fedha zinaweza kutozwa?
Kwasababu kila line ya simu imesajiliwa na bila shaka kuna database, wataalamu wanaweza kuamua ni namna gani watu watozwe(iwe ni kila anaponunua airtime kama watatozo kwa kuchaji asilimia fulani kila unaponunua airtime au atozwe mara moja kwa mwezi,mara mbili au vinginevyo).

Hapa namanisha kuwa,kwasababun kila line ya simu imesajiliwa jina moja,mtu huyo akishanunua vocha na kufikisha kiwango kilichopangwa kwa mwezi, system haitamkata tena hela anaponunua airtime nyingine ndani ya mwezi husiku(kama itakuwa ni kulipia kwa mwezi).

Kwa wenye line zaidi ya moja itakuwaje?
Kwanza lazima ieleweke kuwa,wananchi watakaoukuwa teyari kwa huduma hii ya Bima,watapaswa kusajiliwa wao pamoja na line za simu watazopendelea zitumike kwa kulipia huduma hii za simu zitakazotumika kwa huduma hii na hivyo kuondoa uwezekana wa mtu kuchajiwa kwa kila line anayomiliki.

Kwa kununua vocha maalumu, mtumiaji wa simu anaweza pia kutumia line ya simu iliyosajiliwa kutumika katika kulipia huduma hii kulipia michango yake yake ya Bima.

Namna gani watumiaji wa huduma hii watatambulika katika mahosipitali na katika vituo vya afya?
Kwasababu huduma hii itakuwa inaendeshwa kielektroniki, zinzaweza kuandaliwa kadi za kielektoniki ambazo kila mtumiaji atapewa kama kadi yake ya utambulisho, kadi ambazo zitapaswa kutambuliwa na vifaa maalumu vitavyopatikana katika hospitali na vituo husika vya afya nchi nzima.

Kadi hii, licha ya kumtambulisha mwanachama,bado inaweza pia kubeba taarifa zake zote zikiwemo taarifa za michango yake na pia kueleza kama ametimiza vigezo na mashariti yote ya kuhudumiwa na Mfuko utakaoanzishwa kulinga na sheria itayounda Mfuko huo.

Kwanini ni muhimu kuwa na Mfuko wa aina hii licha ya gharama zitazoongezeka kwa watumiaji wa simu?
Ni ukweli ulio wazi kuwa Bima ya Afya ni jambo muhimu sana kwani magonjwa huja bila kujali una fedha au huna huku magonjwa mengine gharama zake zikiwa ni juu kuliko uwezo wa watanzania walio wengi hivyo ni bora kutozwa hizo gharama ndogo ili hata unapougua usishindwe kuhudumiwa kwa kukosa fedha.

Na kama tunazotozwa fedha kila tunaponunua vitu vitu/bidhaa kama umeme kuendeshea taasisi kama EWURA au REA wanaohusika na usambazaji umeme vijijini kuna ubaya gani tukatozwa fedha kidogo kupitia simu zote za mkonono kwa ajili ya afya zetu au kugharamia elimu za watoto wetu?

Pia, unaweza kuona hiyo miatano(500/=) na nyingi lakini jiulize kwa mwezi unatumia kiasi gani kuweka kwenye simu yako na kuwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki tena sometimes kuwasalimia tu.Pia jiulize ni kiasi gani unakatwa kulipia deni la Bodi ya Mikopo kila mwezi alafu ndio uone kama hiyo 500 au 300 kwa mwezi inaweza kuwa ni nyingi, na pia jiulize ni kiasi gani unaweza kukopa mkopo wa riba kugharamia matibabu yako,ya mwanao au ya mzazi wako kule kijijini au aliekuja nyumbani kwako(mjini) kwa ajili ya matibabu.

Kuunda Mfuko(Fund) husika

Wataalamu na wadau wote wanaohusika wakiona jambo hili linawezekana, basi watapeleka mapendekezo yao serikalini kwa ajili ya utekeleazaji ambapo serikali itapaswa kuandaa sera na sheria itayotumika kuanzisha na kusimamia uendeshaji wa Mfuko huu.

Sheria inaweza kuweje?
Hii ni kazi ya wataalamu ila pamoja na mambo mengine,sheria inaweza kutamka kuwa ni lazima kila mtanzania mwenye kumliki line ya simu ajiunge na huduma hii au iwe ni hiari ya mtu(ni vizuri iwe hiari lakini itafaa zaidi fedha zitazokusaywa zitumike pia katika kuhamasisha watu wajiunge na Mfuko huu na pia zitumike kutoa elimu kwa umma juu ya umuhimu wa kuwa na Bima ya Afya kupitia semina,makongamono,matangazo katika vyombo vya habari,n.k).

Kwa kila mchangiaji mwenye watoto au tegemezi,sheria itamke wazi ni watoto au ni wategemezi wangapi wanaweza kunufaika na huduma hiyo.

Pia,sheria itakayounda Mfuko huu, imtake kila mwanachama, kueleza ni i nani ataotaka wafaidike kupitia michango yake kwenye mfuko husika.

Usalama wa Mfuko
Ili kuzuia serikali kuingilia utendaji wa Mfuko huu, na pia ili kuufanya Mfuko uwe huru kwa lengo la kufanya wanasiasa wasiwe na mamlaka juu ya uendeshaji wa huu Mfuko huu, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huu asiteuliwe na Raisi ,na pia sheria itamke bayana kuwa serikali hairuhusiwi kukopa kutoka katika huu Mfuko isipokuwa panapotokea dharura maalumu kama vile kukabiliana na madhara yaliyosababishwa na majanga ya asili au nchi inapoingia katika vita ,n.k.

Faida nyingine za kuanzishwa kwa Mfuko/tozo ya aina hii

Wafanyakazi/Waajiriwa, hawatalazimika tena kukatwa hela(maelfu kadhaa ya shlingi) kutoka kwenye mishahara yao kila mwezi kwa ajili ya kuchangia Bima ya Afya ya Taifa na hivyo wataokoa fedha na kupuguza wingi/mzigo wa makato katika mishahara yao.

Watanzania wengi hata wale wasio na ajira za kuelewaka/rasimi, wanaweza kupata Bima ya Afya kwa kumiliki tu simu ya mkononi.

Makusanyo haya yanaeweza pia kutumiwa kugharamia elimu ya juu na kusomesha watanzania wote bila kuwa na element za kubaguana na hata kuwezessha elimu bure mpaka vyuo vikuu.

Kuanzishwa kwa chombo kama hiki, pia kutatengeneza fursa za ajira kwa watanzania watakaojiriwa katika Mfuko huu,makampuni ya simu yataongeza faida na hivyo yatalipa kodi zaidi serkalini ,na pia uuzaji wa vocha hizi maalumu nao utatoa ajira kwa vijana wataojihusisha na biasharan hii,n.k.

Hasara zinazoweza kujitokeza

Binafsi sioni hasara yoyote katika kuanzisha Mfuko kama huu.

Yangu ni hayo,mnaweza kuboresha au kukosa pale ambapo nimekosea kwani naamini humu wamo watu wa fani za aina nyingi hivyo kuna wenye kuweza kuwa na mawazo bora zaidi kulingana na fani zao.

Tusisahau hata vitu kama Mpesa na tigo pesa vilibuniwa na watu, hivyo hata na sisi tunawza kubuni vya kwetu na wengine wakaiga.
Salary Slip
Your idea is superb! Yaani kuna watu wengine hata hawana uwezo wa kugharmia matibabu. Ukiangalia kipindi cha Mimi na Tanzania kila wiki J4 kinachoendeshwa na Hoyce Temu ITV, utasikitika sana. If implemented, your ides could save lives of people. Idea hii inabidi iwafikie kwa haraka sana Mh. Ndugulile na Mh. Waziri wa Afya. Ninadhani pia kuwa wamo humu jukwaani. Au basi imfikie hata mtani wangu wa kuibiana ng'ombe. Mh. Dr. Mollel
 
Serikali inakusanya pesa nyingi kutoka vyanzo vingi ilivyonavyo lakini bado wazo lako halijawahi kufikiwa.. Pili katika watu milioni 40 sio wote kwao 500 ni fedha isiyo na madhara, wapo watu hawaweki hela kwenye simu mpaka line inafungiwa..
Angalau nusu ya hao million 40 ni uhakika kuwa 500 haiwezi kuwa na madhara kwao. Hata nusu tu ya watu hawa inatosha kabisa kwa wazo hili la Salary Slip kuwa implemented. Kumbuka pia kuna watu wengine wenye ukwasi wanaoweza wakawa wanachangia mfuko huu kwa hiari, wengine wana uwezo wa kutoa hata TZS Billion moja, au vimillion kadhaa, kwa mfano.
 
Back
Top Bottom