Serikali kupitia BoT, iruhusu watumishi wa umma wanaolipwa posho za mwezi kukopa kupitia posho zao

Sasa ukikopa ndio hiyo pesa itaongezeka ???

Sana sana ukikopa maana yake umeongeza matumizi ya hiyo pesa wakati bado ni ndogo.
Inategemea umekopa kufanya nini.Kama umrkopa kwenda kulipia ada ya mtoto kwanini usiumie?

Na kama umekopa ukamalizia fremu za biashara au nyumba za kupangisha, unadhani hata hayo maumivu ya makato utasikia?
 
la msingi na la maana, serikali kushusha riba za mikopo kwa wafanyakazi na wafanyabiashara mtaani iwe mpaka chini ya 5%.... wafanyabiashara wadogo wawekewe mazingira rahisi kuaccess hiyo mikopo.... hapo ndio uchawi ulipo...
 
la msingi na la maana, serikali kushusha riba za mikopo kwa wafanyakazi na wafanyabiashara mtaani iwe mpaka chini ya 5%.... wafanyabiashara wadogo wawekewe mazingira rahisi kuaccess hiyo mikopo.... hapo ndio uchawi ulipo...
Umedhamiria kuandika la maana, wazo zuri!!
 
Kinachomuumiza huyo mlengwa ni riba za mabenki na si kipi anatakiwa akitumie kukopea, posho ibaki kama mali ya familia.
Suluhu ya hili ni benki kushusha riba kwa wahitaji.
Ni kweli lakini hili la kushusha riba ni wimbo wa miaka nenda miaka rudi.
 
Ni kweli lakini hili la kushusha riba ni wimbo wa miaka nenda miaka rudi.
Maelekezo yamekwisha tolewa mara kadhaa kuelekeza mabenki kushusha riba, ni wakati sasa wa Vyama vya wafanyakazi kuomba hili na kupaza sauti kama kero inayowamaliza wastahiki, badala yake wasiwekeze nguvu katika kupandishiwa mishahara tuu, watazamie na hili litakalo wanufaisha baada ya mishahara kupandishwa.
 
Nimerejea mara mbili kuhakiki jukwaa, hii mada haipo jukwaa la siasa.
Tujikite kwenye hoja iliyowekwa jamvini.
Hawa wanajadili mada kutegemea imeletwa na nani na wala sio content.

Hawajui kuwa kuna watu wana posho mpaka 500,000 kwa mwezi ambazo wakiruhusiwa kuziokpea, wanaweza kufanya uwekezaji mkubwa tu na serikali ikapata kodi.
 
Hawa wanajadili mada kutegemea imeletwa na nani na wala sio content.

Hawajui kuwa kuna watu wana posho mpaka 500,000 kwa mwezi ambazo wakiruhusiwa kuziokpea, wanaweza kufanya uwekezaji mkubwa tu na serikali ikapata kodi.
Ukimwambia posho mwenzio anawaza zile wanazolipana kwenye semina na posho za madaraka ya mwl mkuu nk.
 
Ila Kuna watu wanalipa na kutumia hela vibaya then wanaanza kuteseka maana duh
 
Ungekuwa unajua kutumia vizuri hiyo mikopo uliyokopa ingeshakutoa usingehitaji Tena kuwa posho nazo ziingizwe ukakopee .Wewe inanyesha mshahara wote unaishia kulipa madeni.Kwani ulizokopa ulifanyia Nini ambacho hakizalishi ujikwamue kwenye Lindi la madeni
Unaogea hearsay tu badala ya kuja na hoja za msingi.

Huyo Magu unaemtetea ndio alikuwa bingwa wa kukopa tena na kuwekeza kwenye miradi isiyo na tija ila hilo halikuwa tatizo bali tatizo ni mtumishi kuongezewa wigo wa kukopa.
 
Ila Kuna watu wanalipa na kutumia hela vibaya then wanaanza kuteseka maana duh
Kuna mambo mengine hatuwezi tu kuyaweka wazi humu. Kuna taasisi baadhi ya watumishi wake wana allowance za kila mwezi zinazozidi hata mishahara(take home) za watumishi wengine na hawa ndio wangefaidika zaidi kuruhusiwa kukopea kupitia hizo posho

Matajiri tunaowaona wengi wana mikop katika mabenki halafu mtu anapinga hoja ya mtumishi kuongezewa wigo wa kukopa.
 
Kuna mambo mengine hatuwezi tu kuyaweka wazi humu. Kuna taasisi baadhi ya watumishi wake wana allowance za kila mwezi zinazozidi hata mishahara(take home) za watumishi wengine na hawa ndio wangefaidika zaidi kuruhusiwa kukopea kupitia hizo posho
Hili jambo nimetazamia kuwa ni sahihi zaidi wakopee kwenye mifuko ya Taasisi zao.
Yaani anaekulipa posho ndio akukopeshe kwa riba nafuu na kwa kipindi kifupi cha marejesho.
 
Unaogea hearsay tu badala ya kuja na hoja za msingi.

Huyo Magu unaemtetea ndio alikuwa bingwa wa kukopa tena na kuwekeza kwenye miradi isiyo na tija ila hilo halikuwa tatizo bali tatizo ni mtumishi kuongezewa wigo wa kukopa.
Kifupi mleta mada umefilisika kifedha

Kufilisika kifedha kuko hivi unakuwa na madeni makubwa kuliko kipato chako .Wewe hiyo stage umeshaifikia .Hebu fikiria unawaza kukopea Hadi posho ya chakula na mavazi eti ikifika mwisho wa mwezi unamwambia mkopeshaji rejesho nikate posho ya chakula na mavazi matokeo yake utabaki uchi sababu huna hela ya mavazi na utakufa njaa!!!

Kifupi wewe umeshafilisika Uko bankrupt
 
Kifupi mleta mada umefilisika kifedha

Kufilisika kifedha kuko hivi unakuwa na madeni makubwa kuliko kipato chako .Wewe hiyo stage umeshaifikia .Hebu fikiria unawaza kukopea Hadi posho ya chakula na mavazi eti ikifika mwisho wa mwezi unamwambia mkopeshaji rejesho nikate posho ya chakula na mavazi matokeo yake utabaki uchi sababu huna hella ya mavazi na utakufa njaa!!!

Kifupi wewe umeshafilisika Uko bankrupt
 
Kuna mambo mengine hatuwezi tu kuyaweka wazi humu. Kuna taasisi baadhi ya watumishi wake wana allowance za kila mwezi zinazozidi hata mishahara(take home) za watumishi wengine na hawa ndio wangefaidika zaidi kuruhusiwa kukopea kupitia hizo posho

Matajiri tunaowaona wengi wana mikop katika mabenki halafu mtu anapinga hoja ya mtumishi kuongezewa wigo wa kukopa.
Bora wasiruhisiwe watateseka sana na mikopo Yao majority wanateseka sana
 
Back
Top Bottom