Serikali: Kupanda kwa bei ya Nyama kunatokana na upungufu wa Ng'ombe

Sasa hapo kilichopanda ni nini?? Maana nyama nimekuwa nikiinunua sh 8000 toka mwaka juzi
 
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega ameeleza sababu ya nyama kupanda kwa bei katika maeneo mbalimbali nchini ni kutokana na upungufu wa upatikanaji wa ng’ombe na ongezeko la mahitaji ya viwanda vya kuchakata nyama.

Hata hivyo wafanyabiashara wa mifugo na wauza mabucha wamesema kuwa kupanda kwa kitoweo hicho kuanzia wanakochukua (machinjioni), gharama za usafirishaji na msimu huu wa kiangazi kumesababisha pia bei ya nyama kupanda kwani wafugaji wengi hawapendi kuuza ng’ombe wakati huu wakidai kwamba mifugo hiyo inakua haina uzito kutokana na kupungua kwa malisho na maji.

Bei ya nyama kwenye mikoa ya Arusha, Moshi na Dar es Salaam inadaiwa kuwa shilingi 7,000 mpaka shilingi 8,000 kwa kilo tofauti na awali ambapo kitoweo hicho kilikua kikiuzwa shilingi 6,000.
Sawa, tusubiri ng’ombe wanenepe, then wataanza kuuzwa kwa wingi na wafugaji, na nyama itashuka
 
Kama nyama yenyewe ndio hiyo kwenye picha, hata 10,000 bado rahisi,
Hatupati kabisa nyama kama hiyo buchani
 
Waziri alitegemea bei ibaki kama awali au kushuka? Serikali na wabunge wake(kumbuka wananchi hatuna wabunge, wote ni wateule wa serikali) wanapo pitisha budget inayotegemea ongezeko la bei ya mafuta wanategemea budhaa zisipande? Bei kabla ya kupanda ulaji wa nyama ulipugua, hela imepunguzwa kwa watu kupitia tozo.
 
Sisi si ndiyo mnasemaga tuna Ng'ombe wengi sijui wa pili Africa
Baada ya Ethiopia ni Tanzania ndiyo ya pili kwa idadi ya mifugo Afrika.

Ukweli ni kwamba, wafugaji hasa wasukuma hawataki kuuza mifugo yao kwa sababu wanacho chakula cha kutosha (Mahindi na mpunga), na hakuna namna ya kuwalazimisha wauze kwa sababu wanafuga kama ufahari, na huuza wanapokuwa na njaa!

Serikali lazima ijikite kuwawezesha wafugaji wafuge kibiashara.
 
Baada ya Ethiopia ni Tanzania ndiyo ya pili kwa idadi ya mifugo Afrika.

Ukweli ni kwamba, wafugaji hasa wasukuma hawataki kuuza mifugo yao kwa sababu wanacho chakula cha kutosha (Mahindi na mpunga), na hakuna namna ya kuwalazimisha wauze kwa sababu wanafuga kama ufahari, na huuza wanapokuwa na njaa!

Serikali lazima ijikite kuwawezesha wafugaji wafuge kibiashara.
Point!
 
Aisee jembe buchani unauziwa elfu 8. Kuna siku niko buchani mdada ananunua nyama robo kilo. Sikuelewa kabisa anaenda kutumia kwenye nini. Kupikia? Au kutengeneza dawa?! Dah! Nilijisikia vibaya. Nikatamani nimuongee ila nikahofia ataona nimemdharau
 
serikali ndio chanzo haya yote kuanzia wakulima,wafugaji na wavuvi.
kwa nini!

sijui nchi za nje wanaenda kujifunza nini!

leo nchi kama dubai wanaongoza kufuga ng’ombe wa nyama na maziwa wakati jangwa.
jiulize kwa nini!

tuendelee kudumisha ccm kubaki madarakani ndio wanalofikilia sio mengine
 
Baada ya Ethiopia ni Tanzania ndiyo ya pili kwa idadi ya mifugo Afrika.

Ukweli ni kwamba, wafugaji hasa wasukuma hawataki kuuza mifugo yao kwa sababu wanacho chakula cha kutosha (Mahindi na mpunga), na hakuna namna ya kuwalazimisha wauze kwa sababu wanafuga kama ufahari, na huuza wanapokuwa na njaa!

Serikali lazima ijikite kuwawezesha wafugaji wafuge kibiashara.
Okay nimekupata Mkuu kumbe Jamaa zetu wanafuga Ng'ombe kama Urembo
 
Okay nimekupata Mkuu kumbe Jamaa zetu wanafuga Ng'ombe kama Urembo
Usukumani wanafuga ng'ombe kama urembo kabisa.

Unakuta msukuma ana ng'ombe kama mia mbili hivi halafu anaishi kwenye nyumba ya nyasi. Ukitaka mgombane nae, mwambie akuuzie ng'ombe wakati hajapanga kuuza.

Ndani kukiwa na mpunga wa kutosha, viazi, mtama, na mahindi, hauzi ng'ombe.
 
Usukumani wanafuga ng'ombe kama urembo kabisa.

Unakuta msukuma ana ng'ombe kama mia mbili hivi halafu anaishi kwenye nyumba ya nyasi. Ukitaka mgombane nae, mwambie akuuzie ng'ombe wakati hajapanga kuuza.

Ndani kukiwa na mpunga wa kutosha, viazi, mtama, na mahindi, hauzi ng'ombe.
Dah,Basi kuna kazi kubwa sana ya kuwaelimisha Jamaa zetu Wafugaji.
 
Huku Makambako, mabucha yanauza kwa kupokelezana. Sio kwamba nyama adimu, bali hakuna hela za kutosha kama zamani!
 
Ufafanuzi Ni kwamba Bei ya nyama imepanda kutokana na kupanda kwa Bei Ng'ombe Kwenye soko la Dunia imepanda....
IMG_20210917_184023.jpg
 
Wapromote ufugaji wa Ngrooohhhh? Miezi sita tu anaingia sokoni, wakati Ng'ombe anahitaji miaka miwili na uzao wao ni wa 1\1\ na mimba ya miezi 9. Wakati Ngrooohhh mimba moja watoto 12 na mimba ni miezi mitatu tu.
Mashehe......
IMG_20210918_180913.jpg
 
Back
Top Bottom