Serikali: Kuongezeka kwa ufaulu ni matokeo ya ubora wa elimu

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,476
17,674
Serikali imetangaza kwamba zaidi ya 96% ya wanafunzi wa shule za msingi waliohitimu darasa la saba mwaka 2013 wamechaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari mwaka 2014.

Akitangaza matokeo hayo, katibu mkuu wa TAMISEMI amesema kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu kumetokana na ubora wa elimu na kwamba hiki ni kiashiria kwamba wanafunzi wanaelewa masomo kwa kuwa wanasomea katika mazingira bora.

Ili kuhakikisha kwamba nafasi zote za sekondari zilizopo zinajazwa, serikali ilishusha alama za ufaulu (passmark) hadi 40 kati ya alama 250 (kuna papers 5 na kila paper inachangia alama 50). Hii maana yake ni kwamba mwanafunzi yeyote aliyemudu kupata wastani wa alama 8 (sawa na 16% ya ufaulu) kwa kila somo alichaguliwa kujiunga sekondari.

Source : TBC1
 
Kwi kwi kwi kwi kwi lol!!!! Ukiwauliza kipi walichokifanya baada ya matokeo mabaya ya 2012 na 2013 kilichoongeza ubora wa Elimu nchini wataanza kung'aa macho. Hii mijitu ni mipumbavu ya kutupa!!!!! dah!!!!


Kwi! Kwi! Kwi! Kwi!
 
Hicho ni kioja kikubwa kuliko Division 5. Yaani 16% anaenda Sekondari? Sasa naelewa kwa nini hataCCM wanamwita Kawambwa Mzigo. Kwa kituko hicho nami namwona kweli Kawambwa ni mzigo mzito sawa na Gunia la misumari
 
Over 12,000 illiterates ‘sat Standard 7 exam

wanafunzi.jpg

"Teachers and schools in general know very well the progress of pupils academically, so they are in a better position to decide whether or not pupils should progress to the next class...it all boils down to academic performance," .

Over 12,000 illiterates

 
Ili kuhakikisha kwamba nafasi zote za sekondari zilizopo zinajazwa, serikali ilishusha alama za ufaulu (passmark) hadi 40 kati ya alama 250 (kuna papers 5 na kila paper inachangia alama 50). Hii maana yake ni kwamba mwanafunzi yeyote aliyemudu kupata wastani wa alama 8 (sawa na 16% ya ufaulu) kwa kila somo alichaguliwa kujiunga sekondari.

Source : TBC1


Kwa kadri nilivyoelewa kwa maneno hayo(in red) lengo lilikuwa ni kujaza nafasi kuliko ufaulu. Lengo hili linameza maelezo mengine yote hapo juu na kuyafanya ni siasa tupu. Tunazidi kuumiza taifa na kuachwa nyuma kwa kuingiza siasa katika eneo hili nyeti.

Hata hivyo hao 4% wanaenda wapi? Tupo karne ya 21 sasa yenye changamoto nyingi za kisayansi na kiuchumi, raia wa kada ya darasa la saba(7) ni mzigo na maafa kwa taifa lenye malengo ya kupiga hatua. Wakati ni huu sasa nchi ikaja na sera mpya ya elimu itakayobainisha kuwa elimu ya msingi(kwa wote) ni mpaka kidato cha nne na baada ya hapo vijana waendelee(wote) na masomo katika vyuo vya kada ya kati katika fani mbalimbali watakazochagua.
 
Sasa Jamani Haya Majanga. Kabla Ya Kawambwa Matokeo Yalikuwa Yanatoka Mapeema Na Hivyo Kutoa Muda Wa Kutosha Kwa Wazazi Kujiandaa. Hali Ni Mbaya Sana Sikuhizi Kwani Bado Siku Zisizo Zidi Kumi Njuka Wanahitajika Shule. Sisiemu Ni CHAMA CHA MIZIGO!
 
Mkuu, naona JK bado ana kibarua kikubwa - nani ambaye ajui kwamba Wizara ya Elimu na huko TAMISEMI kuna baadhi ya wajiliwa ambao ni waigizaji tu i.e commitment ya kuendeleza Elimu nchini ni ndogo sana - hivi huyo jamaa wa TAMISEMI anataka kulieleza Taifa letu kwamba ghafla bin vooom vijana wetu wamepata Walimu mahili na vitendea kazi na motisha wa kufa mtu yaani ndani ya miezi sita/saba wakawafundisha vijana wetu usiku na mchana mpaka wakafikia kiwango cha kufahulu kwa asilimia 96% - this's 2 good 2 be true which's true! Tujaribu kuwa wakweli hapa, nilimuona jamaa alivyo kuwa anajieleza, one could sense kwamba all is not well at warfront - Mataifa mengi Duniani ni maskini leo kutokana na kupuuzia Elimu, tusije tuka ambiwa mwaka kesho kwamba asili mia kubwa ya watoto waliochaguliwa kujiungia kidato cha kwanza hawajui vizuri kuandika/kusoma - tusifanye liende jamani i.e kunawa mikono, hali ya Elimu nchini inatisha sana tusifanye maigizo!! Leo hii nimejiuliza maswali mengi - hivi tukitafuta an independent consultant, akatufanyia ka-utafiti anaweza kulithibitishia Taifa letu na Rais kwamba msemaji anachosema kina ukweli wowote au ndio kutaka kuwa-please RAIA wakati tatizo bado lipo pale pale, huu umakini wa ku-reverse udololoji wa elimu katika Taifa letu in no TIME umeanza lini jamani? Ufaulu wa design hii hata kwenye Guiness book of record haupo kabisa.
 
Hongera Vijana...

Miaka Minne ijayo, tutapata JIBU SAHIHI la ongezeko hili la KASI YA AJABU.

B.R.N at WORK
 
Mkuu, naona JK bado ana kibarua kikubwa - nani ambaye ajui kwamba Wizara ya Elimu na huko TAMISEMI kuna baadhi ya wajiliwa ambao ni waigizaji tu i.e commitment ya kuendeleza Elimu nchini ni ndogo sana - hivi huyo jamaa wa TAMISEMI anataka kulieleza Taifa letu kwamba ghafla bin vooom vijana wetu wamepata Walimu mahili na vitendea kazi na motisha wa kufa mtu yaani ndani ya miezi sita/saba wakawafundisha vijana wetu usiku na mchana mpaka wakafikia kiwango cha kufahulu kwa asilimia 96% - this's 2 good 2 be true which's true! Tujaribu kuwa wakweli hapa, nilimuona jamaa alivyo kuwa anajieleza, one could sense kwamba all is not well at warfront - Mataifa mengi Duniani ni maskini leo kutokana na kupuuzia Elimu, tusije tuka ambiwa mwaka kesho kwamba asili mia kubwa ya watoto waliochaguliwa kujiungia kidato cha kwanza hawajui vizuri kuandika/kusoma - tusifanye liende jamani i.e kunawa mikono, hali ya Elimu nchini inatisha sana tusifanye maigizo!! Leo hii nimejiuliza maswali mengi - hivi tukitafuta an independent consultant, akatufanyia ka-utafiti anaweza kulithibitishia Taifa letu na Rais kwamba msemaji anachosema kina ukweli wowote au ndio kutaka kuwa-please RAIA wakati tatizo bado lipo pale pale, huu umakini wa ku-reverse udololoji wa elimu katika Taifa letu in no TIME umeanza lini jamani? Ufaulu wa design hii hata kwenye Guiness book of record haupo kabisa.
Elimu ya Tanzania kama kichwa cha mwendawazimu kila mtu anafanya anachokitaka. Hivi hayo matokeo si yalishatangazwa na NECTA na yapo kwenye website hadi leo? sasa ufaulu wa 94% umetoka wapi yaani imefika mahali tunadaganywa mchana kweupe!!!
This can only happen in Tanzania
 
Cha kushangaza kuna mwanafunzi mmoja aliesimamishwa kufanya mtihani kwa kushindwa kulipa ada eti nae kafaulu wakati hakufanya mtihani
 
Elimu ya Tanzania kama kichwa cha mwendawazimu kila mtu anafanya anachokitaka. Hivi hayo matokeo si yalishatangazwa na NECTA na yapo kwenye website hadi leo? sasa ufaulu wa 94% umetoka wapi yaani imefika mahali tunadaganywa mchana kweupe!!! This can only happen in Tanzania
Well said mkuu - wala tusiende mbali kuonyesha usanii unaoendelea katika Taifa letu, katika sekta ya ELIMU ni janga mkuu. Ebu soma taarifa hii kutoka gazeti la NIPASHE, samahani browser yangu ina tatizo kuweka paragraph vile vile na link:- SHULE TAABANI. Lakini yafaulisha wanafunzi wote Katika hali isiyo ya kawaida, shule moja wilayani Bagamoyo imekutwa ikiwa na mwalimu mmoja tu anayefundisha wanafunzi kuanzia chekechea hadi darasa la saba, wote wakifundishwa katika chumba kimoja kwa kutumia ubao mmoja. Hata hivyo, katika matokeo ya Darasa la Saba Mwaka huu, wanafunzi wote 12 walifaulu kuingia kidato cha kwanza. Shule hiyo ya msingi Machala, iliyokuwa na idadi ya wanafunzi 198 na imejengwa kwa majani kuanzia chini hadi kwenye paa. Mwandishi wa habari hizi aliyetembelea shule hiyo, alimkuta mwalimu huyo akiwafundisha wanafunzi hao wa madarasa tofauti wakiwa kwenye chumba kimoja, huku ubao wa kufundishia ukiwa umechorwa mistari mitatu kutenganisha masomo ya chekechea hadi darasa la pili, mstari mwingine darasa la tatu hadi la tano na mwingine darasa la sita hadi la saba. Mwalimu huyo, Christopher Rukutu, aliliambia NIPASHE Jumamosi kuwa shule hiyo hutumia kivuli cha mti kama ofisi. Shule hiyo iliyopo katika kijiji cha Mihunga Kata ya Miono, Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, ilianzishwa na serikali tangu mwaka 2007 ikiwa na wanafunzi 12 ambao wamemaliza darasa la saba, mwaka huu na kubahatika kufaulu wote. Kwa mujibu wa mwalimu Rukutu, wanafunzi wote waliofaulu walipata alama za A na B isipokuwa mmoja aliyepata alama C. Pamoja na kuwa katika mazingira magumu, shule hiyo kiwilaya ilishika nafasi ya sita na kimkoa nafasi ya 20. Alisema shule hiyo haina vitabu vya kiada wala vya kufundishia na amekuwa akiazima kutoka shule za jirani. "Ninafundisha kwa akili za kuzaliwa sina kitabu cha mtaala wa elimu, nguvu zangu zote nilimalizia kwa darasa la saba ili wajue kusoma, kuandika na kuhesabu. Kwa mwaka mzima sijafundisha darasa la nne nina wasiwasi matokeo yao hayatakuwa mazuri kwa sababu niko peke yangu," alisema kwa masikitiko. Alifafanua kuwa tangu shule hiyo ianzishwe, serikali ilikuwa imewapanga walimu wawili tu, ambao kutokana na mazingira kuwa magumu waliripoti bila kuingia darasani na kuaga baada ya kuonyesha vyeti vya hospitali vinavyonyesha kuwa afya zao haziwezi kustahimili mazingira magumu. Aliilalamikia serikali kuanzia ngazi ya kata hadi wilaya kwa kuisahau shule hiyo bila kuipa msaada wowote. Mbali na kukosa msaada, shule hiyo pia inatumia tundu moja tu la choo kwa wanafunzi wa kike na kiume na kusababisha wengi wao kujisaidia vichakani.Alisema kutokana na hali hiyo, wanafunzi wengi hushambuliwa na ugonjwa wa kichocho. Aliiomba Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kuwapangia wanafunzi wake 12 waliofaulu katika shule yake ya Machari kwenye shule za sekondari zenye mahitaji muhimu ili kuwapunguzia mateso wanafunzi hao. Alisema wanafunzi wake hawajawahi kuona vitabu vya kujisomea na huduma muhimu za kiafya. CHANZO: NIPASHE
 
hii comedy haina tofauti na ile ya division 5

unasema zaidi ya 96% waliohitimu? mkuu acha basi uwongo...kuna tofauti kubwa kati ya waliohitimu na waliofaulu na kujiunga na kidato cha kwanza..

96% ya waliofaulu mtihani wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza
 
Serikali imetangaza kwamba zaidi ya 96% ya wanafunzi wa shule za msingi waliohitimu darasa la saba mwaka 2013 wamechaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari mwaka 2014.

Akitangaza matokeo hayo, katibu mkuu wa TAMISEMI amesema kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu kumetokana na ubora wa elimu na kwamba hiki ni kiashiria kwamba wanafunzi wanaelewa masomo kwa kuwa wanasomea katika mazingira bora.

Ili kuhakikisha kwamba nafasi zote za sekondari zilizopo zinajazwa, serikali ilishusha alama za ufaulu (passmark) hadi 40 kati ya alama 250 (kuna papers 5 na kila paper inachangia alama 50). Hii maana yake ni kwamba mwanafunzi yeyote aliyemudu kupata wastani wa alama 8 (sawa na 16% ya ufaulu) kwa kila somo alichaguliwa kujiunga sekondari.

Source : TBC1

Hii ni kejeli Plus Plus
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom