BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 422
- 1,049
Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema takwimu za matukio ya vitendo vya ukatili Nchini vilivyoripotiwa kwenye vituo vya Polisi kuanzia mwaka 2019 hadi Machi, 2022 ni 27,838.
Masauni amesema hayo leo Aprili 6, 2022 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge la Viti Maalum, Fatma Toufiq alipohoji Je, kuna wahanga wangapi wa vitendo vya ukatili nchini kuanzia mwaka 2019 hadi 2022?
Masauni amesema mchanganuo wa takwimu hiyo ni matukio ya kubaka ni 19,726, kulawiti ni 3,260 kati yao wanaume 3,077 na wanawake 183, kuunguzwa kwa moto ni 198 kati yao wanaume 73 na wanawake 125, kutupa watoto wachanga ni 443 kati yao wanaume 177 na wanawake 266, kipigo ni 4,211 kati yao wanaume 16 na wanawake ni 4195.
Masauni amesema jumla ya kesi zilizofikishwa Mahakamani ni 21,063 na watuhumiwa waliohukumiwa ni 14,278 na mashauri mengine yako kwenye hatua mbalimbali za upelelezi na mahakamani.
Aidha, Serikali inaendelea kuiasa jamii kutumia vema taasisi za familia, kaya, jumuiya za kidini na ngazi za vitongoji, vijiji na mitaa kudhibiti vitendo vya ukatili katika jamii.