Serikali kumsaka nyoka mwenye miaka 209

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
[h=2]20 JULY 2012[/h]Na Theonestina Juma, Bukoba

SERIKALI imedhamiria kumsaka nyoka mwenye umri wa miaka 209 aliyepo katika Msitu wa Akiba Minziro, uliopo Wilaya ya Misenyi, mkoani Kagera.

Lengo la kumsaka nyoka huyo ni kutokana na ukongwe wake hivyo kuwa kivutio kikubwa duniani hasa katika sekta ya utalii.

Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki nchini, Dkt. Felician Kilahama, aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema nyoka huyo mwenye futi 47, atapatikana baada ya mapito yake katika msitu huo kuonekana ila ni vigumu kuonekana hadharani kwa sababu hupendelea kuishi mapangoni.

“Huyu nyoka lazima tumfanyie mahesabu ya kumkamata kirahisi, umri wa miaka 209 sio mchezo, ameweza kutambulika Baada ya kupima urefu wa mapito yake, pia kuna chatu na nyoka wenye mapembe,” alisema Dkt. Kilahama.

Aliongeza kuwa, licha ya nyoka kuhatarisha maisha ya watafiti lazima kufanyike uharaka wa kuupandisha hadhi msitu huo uwe hifadhi ya Taifa ili kuboresha usimamizi wake.

“Kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa Kagera (RCC), kilipitisha msitu huu upandishwe hadhi, nyoka huyu ambaye ni aina ya Giant Forest Cobra, kichwa chake kina rangi nyekundu na sehemu ya kiwiliwili rangi ya kijani.

“Alianza kufanyiwa utafiti mwaka 2000 baada ya kupatikana kwa taarifa kutoka kwa wenyeji wa maeneo hayo juu ya kuwepo kwa aina ya nyoka huyo katika msitu huu,” alisema.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Halmashauri ya Missenyi, kupitia Maofisa wa Misitu, mwaka 2010 walianza kuweka mitego ya sindano katika mapito anayotumia ili kuchukua damu yake na kwenda kuipima vina saba ndipo ilibainika kuwa hadi kufikia mwaka huo, alikuwa na miaka zaidi ya 207.

Dkt. Kilahama alisema nyoka huyo atakuwa kivutio muhimu mkoani hapa kama atapatikana licha ya kukabiliwa na tatizo la ukumbwa wa msitu ambao hekta 25,000 kwani nyoka huyo amekuwa akihama mara kwa mara kwa ajili ya mawindo.

Ofisa Misitu wilayani hapa, Bw. Wilbard Bayona, alisema nyoka huyo ana uwezo wa kuishi siku 68 bila kula chochote zaidi ya maji baada ya kumeza mnyama yeyote ambaye atamkamata mawindoni.



 
[h=2]20 JULY 2012[/h]Na Theonestina Juma, Bukoba

SERIKALI imedhamiria kumsaka nyoka mwenye umri wa miaka 209 aliyepo katika Msitu wa Akiba Minziro, uliopo Wilaya ya Misenyi, mkoani Kagera.

Lengo la kumsaka nyoka huyo ni kutokana na ukongwe wake hivyo kuwa kivutio kikubwa duniani hasa katika sekta ya utalii.

Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki nchini, Dkt. Felician Kilahama, aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema nyoka huyo mwenye futi 47, atapatikana baada ya mapito yake katika msitu huo kuonekana ila ni vigumu kuonekana hadharani kwa sababu hupendelea kuishi mapangoni.

“Huyu nyoka lazima tumfanyie mahesabu ya kumkamata kirahisi, umri wa miaka 209 sio mchezo, ameweza kutambulika Baada ya kupima urefu wa mapito yake, pia kuna chatu na nyoka wenye mapembe,” alisema Dkt. Kilahama.

Aliongeza kuwa, licha ya nyoka kuhatarisha maisha ya watafiti lazima kufanyike uharaka wa kuupandisha hadhi msitu huo uwe hifadhi ya Taifa ili kuboresha usimamizi wake.

“Kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa Kagera (RCC), kilipitisha msitu huu upandishwe hadhi, nyoka huyu ambaye ni aina ya Giant Forest Cobra, kichwa chake kina rangi nyekundu na sehemu ya kiwiliwili rangi ya kijani.

“Alianza kufanyiwa utafiti mwaka 2000 baada ya kupatikana kwa taarifa kutoka kwa wenyeji wa maeneo hayo juu ya kuwepo kwa aina ya nyoka huyo katika msitu huu,” alisema.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Halmashauri ya Missenyi, kupitia Maofisa wa Misitu, mwaka 2010 walianza kuweka mitego ya sindano katika mapito anayotumia ili kuchukua damu yake na kwenda kuipima vina saba ndipo ilibainika kuwa hadi kufikia mwaka huo, alikuwa na miaka zaidi ya 207.

Dkt. Kilahama alisema nyoka huyo atakuwa kivutio muhimu mkoani hapa kama atapatikana licha ya kukabiliwa na tatizo la ukumbwa wa msitu ambao hekta 25,000 kwani nyoka huyo amekuwa akihama mara kwa mara kwa ajili ya mawindo.

Ofisa Misitu wilayani hapa, Bw. Wilbard Bayona, alisema nyoka huyo ana uwezo wa kuishi siku 68 bila kula chochote zaidi ya maji baada ya kumeza mnyama yeyote ambaye atamkamata mawindoni.




Samahani, hivi life span ya nyoka ni miaka mingapi? Nilidhani ni kobe tu mwenye life span ndefu.
 
yaani badala ya kufanya utafiti na ugunduzi wa nafaz za kazi wanakwenda kumtafuta nyoka ambaye wanahisi yupo lakini hawamuoni! Duh kazi kweli kweli
 
kumpata huyo lazima wengi mpoteze maisha, na si rahisi kumpata, kwasababu nyoka huyo ni shetani, ni mzimu fulani wa watu wa huko ambao hakika yake hata mtu akichanjwa chale kwa mzimu huo mashetani yake kuja kumtoka si rahisi kwasababu amechanja na kujiunganisha na shetani mwenyewe.....kama mna akili timamu, hivi kuna kiumbe hai chenye damu ambacho kinaweza kuishi miaka yote hiyo kama si spiritual being?
 
Samahani, hivi life span ya nyoka ni miaka mingapi? Nilidhani ni kobe tu mwenye life span ndefu.

naomba nikuulize, hivi ulihitaji kunukuu post yote ya awali wakati shida yako ni kuuliza hili swali moja?, huoni kama unatujazia server yetu bila sababu?.
 
Samahani, hivi life span ya nyoka ni miaka mingapi? Nilidhani ni kobe tu mwenye life span ndefu.

average life span 22 years record is 47 years. Nyoka wa umri miaka 207 NAHISI uzushi, mradi wa kupata chochote kitu. How do you determine age from genetic material? ( only aware of radio carbon method of determining age of fossils)
 
Aliongeza kuwa, licha ya nyoka kuhatarisha maisha ya watafiti lazima kufanyike uharaka wa kuupandisha hadhi msitu huo uwe hifadhi ya Taifa ili kuboresha usimamizi wake.

"Kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa Kagera (RCC), kilipitisha msitu huu upandishwe hadhi,
nyoka huyu ambaye ni aina ya Giant Forest Cobra, kichwa chake kina rangi nyekundu na sehemu ya kiwiliwili rangi ya kijani.

Aina hii ya fikra na mitazamo kwa hawa watu wa misitu sijui itaisha lini? Yaani wao mawazo ni kuweka misitu katika hadhi ya uhifadhi tu! Hawawazi kama raia wanaokaa karibu na msitu huo kama wao wanataka msitu huo uwe wa hifadhi!!

Matokeo yake, aina hii ya utekelezaji wa sera (top - down approach) ni kuwa hata huo usimamizi wanaotaka kuboresha unakuwa ni hadithi za Alfu Ulela. Usimamizi bila kuwashirikisha (tena kuwashirikisha kiuhalisia - kuanzia kwenye wazo la kuufanya msitu uwe wa hifadhi au lah) ni kazi bure. Pia ni jambo ambalo halina mafanikio ya muda mrefu, kwani bila kuwa na mipango madhubuti ya kutafuta vyanzo mbadala vya mapato baada ya msitu husika kuwa wa hifadhi, ina maana raia watakuwa wanasukumwa zaidi katika dimbwi la umaskini; kwani vyanzo vya mapato na kusukumia maisha vitakuwa vimepigwa stop - kwa jina la uhifadhi!

Halafu huyo Giant Forest Cobra katika jamii za nyoka sijawahi sikia..najua kuna forest cobra, lakini giant forest cobra?!?




Huyu ndiye forest cobra! Sasa huyu ginat forest cobra sijui yukoje?!?!
 
Aina hii ya fikra na mitazamo kwa hawa watu wa misitu sijui itaisha lini? Yaani wao mawazo ni kuweka misitu katika hadhi ya uhifadhi tu! Hawawazi kama raia wanaokaa karibu na msitu huo kama wao wanataka msitu huo uwe wa hifadhi!!

Matokeo yake, aina hii ya utekelezaji wa sera (top - down approach) ni kuwa hata huo usimamizi wanaotaka kuboresha unakuwa ni hadithi za Alfu Ulela. Usimamizi bila kuwashirikisha (tena kuwashirikisha kiuhalisia - kuanzia kwenye wazo la kuufanya msitu uwe wa hifadhi au lah) ni kazi bure. Pia ni jambo ambalo halina mafanikio ya muda mrefu, kwani bila kuwa na mipango madhubuti ya kutafuta vyanzo mbadala vya mapato baada ya msitu husika kuwa wa hifadhi, ina maana raia watakuwa wanasukumwa zaidi katika dimbwi la umaskini; kwani vyanzo vya mapato na kusukumia maisha vitakuwa vimepigwa stop - kwa jina la uhifadhi!

Halafu huyo Giant Forest Cobra katika jamii za nyoka sijawahi sikia..najua kuna forest cobra, lakini giant forest cobra?!?




Huyu ndiye forest cobra! Sasa huyu ginat forest cobra sijui yukoje?!?!

Sikujua wanaishi miaka yote hiyo
 
this is fantastic news. uchunguzi kuhusu huyo nyoka ni muhimu sana si tu kwa ajili ya intrinsic value of doing so, bali pia kuitangaza hiyo hifadhi na pengine kujua hiyo eco-system nzima inahusikaje na huyo kiumbe. kwa wale wenye mawazo ya kigagula na/au kutokujua umuhimu wa research poleni sana.
 
kumpata huyo lazima wengi mpoteze maisha, na si rahisi kumpata, kwasababu nyoka huyo ni shetani, ni mzimu fulani wa watu wa huko ambao hakika yake hata mtu akichanjwa chale kwa mzimu huo mashetani yake kuja kumtoka si rahisi kwasababu amechanja na kujiunganisha na shetani mwenyewe.....kama mna akili timamu, hivi kuna kiumbe hai chenye damu ambacho kinaweza kuishi miaka yote hiyo kama si spiritual being?
unasema wewe, unauliza wewe ? Khaaa!
 
Aina hii ya fikra na mitazamo
kwa hawa watu wa misitu sijui itaisha lini? Yaani wao mawazo ni kuweka
misitu katika hadhi ya uhifadhi tu! Hawawazi kama raia wanaokaa karibu
na msitu huo kama wao wanataka msitu huo uwe wa hifadhi!!

Matokeo yake, aina hii ya utekelezaji wa sera (top - down
approach
) ni kuwa hata huo usimamizi wanaotaka kuboresha unakuwa ni
hadithi za Alfu Ulela. Usimamizi bila kuwashirikisha (tena
kuwashirikisha kiuhalisia - kuanzia kwenye wazo la kuufanya msitu uwe wa
hifadhi au lah) ni kazi bure. Pia ni jambo ambalo halina mafanikio ya
muda mrefu, kwani bila kuwa na mipango madhubuti ya kutafuta vyanzo
mbadala vya mapato baada ya msitu husika kuwa wa hifadhi, ina maana raia
watakuwa wanasukumwa zaidi katika dimbwi la umaskini; kwani vyanzo vya
mapato na kusukumia maisha vitakuwa vimepigwa stop - kwa jina la
uhifadhi!

Halafu huyo Giant Forest Cobra katika jamii za nyoka sijawahi
sikia..najua kuna forest cobra, lakini giant forest cobra?!?





Huyu
ndiye forest cobra! Sasa huyu ginat forest cobra sijui
yukoje?!?!

Ana kichwa chekundu na kiwiliwili cha kijani!
 
Kwani Intelejensia ya Kova haifanyikazi huko msituni? Mafisadi wanamiradi mingi sana ya kutafuna kodi za walalahoi
 
Ana kichwa chekundu na kiwiliwili cha kijani!

Huyu giant forest cobra mwenye kichwa chekundu atakuwa ndiyo amegunduliwa duniani. Kwanza katika jamii za cobra, ni King Cobra (Ophiophagus hannah) ndiye mkubwa zaidi kuliko wote, ambaye anaweza kuwa na urefu wa wastani wa mita 3 hadi 4; na uzito uwa ni kama 6kg. Ila kama akiwa yupo kwenye Zoo anaweza kuwa mrefu hadi mita 5.7.

Anyway, ngoja tuone matokeo ya uchunguzi huo; huwezi jua, anaweza patikana species mpya ya cobra.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom