BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Serikali kumlipa fidia baba wa Waziri Masha
Nashon Kennedy, Mwanza
Daily News; Monday,December 22, 2008 @21:15
Aliyekuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Sengerema mkoani hapa kupitia chama cha United Democratic (UDP) mwaka 2000, Dk. Fortunatus Masha, ameshinda kesi yake dhidi ya serikali bada ya serikali kuamuriwa kumlipa fidia ya Sh milioni 50 kutokana na kipigo cha polisi alichokipata wakati wa uchaguzi huo.
Masha ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa UDP Taifa, alifungua shauri hilo mwaka 2006, katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, akidai alipwe fidia ya Sh bilioni moja kutokana na kupigwa na askari Polisi wa wilayani Sengerema Oktoba 31, 2000 wakati wa Uchaguzi Mkuu wa rais, wabunge na madiwani.
Kwa mujibu wa Msajili wa Mahakama Kanda Kuu ya Mwanza, Frederica Mgaya, hukumu hiyo ilitolewa Desemba 16, mwaka huu na Jaji A. Sumari. Dk. Masha ni baba wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, ambaye inadaiwa wakati wa tukio hilo la mwaka 2000, alikuwa pamoja na baba yake.
Dk. Masha ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Afrika Mashariki, alikuwa akimlalamikia Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutokana na kupigwa na polisi wakati huo wa uchaguzi, ambao mgombea wa CCM alikuwa ni Dk. William Shija ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola. Katika kesi hiyo, Dk. Masha alikuwa akitetewa na Wakili maarufu nchini, Mabere Marando wakati serikali ilikuwa ikiwakilishwa na mawakili wake wawili, Ewin Kakolaki na Dora Komba.
Kesi hiyo kwa mara ya kwanza ilifunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam mwaka 2001 na baadaye kuhamishiwa katika Mahakama Kuu ya Kanda ya Mwanza ambako ni jirani na eneo la tukio hilo, nia ikiwa ni kuupata ushahidi na kuharakisha shauri hilo ambalo lilisajiliwa kwa namba 10/2006. Hata hivyo, mahakama hiyo imeacha wazi nafasi ya serikali kukata rufaa endapo kwa namna moja ama nyingine haikuridhika na uamuzi huo.
Nashon Kennedy, Mwanza
Daily News; Monday,December 22, 2008 @21:15
Aliyekuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Sengerema mkoani hapa kupitia chama cha United Democratic (UDP) mwaka 2000, Dk. Fortunatus Masha, ameshinda kesi yake dhidi ya serikali bada ya serikali kuamuriwa kumlipa fidia ya Sh milioni 50 kutokana na kipigo cha polisi alichokipata wakati wa uchaguzi huo.
Masha ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa UDP Taifa, alifungua shauri hilo mwaka 2006, katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, akidai alipwe fidia ya Sh bilioni moja kutokana na kupigwa na askari Polisi wa wilayani Sengerema Oktoba 31, 2000 wakati wa Uchaguzi Mkuu wa rais, wabunge na madiwani.
Kwa mujibu wa Msajili wa Mahakama Kanda Kuu ya Mwanza, Frederica Mgaya, hukumu hiyo ilitolewa Desemba 16, mwaka huu na Jaji A. Sumari. Dk. Masha ni baba wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, ambaye inadaiwa wakati wa tukio hilo la mwaka 2000, alikuwa pamoja na baba yake.
Dk. Masha ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Afrika Mashariki, alikuwa akimlalamikia Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutokana na kupigwa na polisi wakati huo wa uchaguzi, ambao mgombea wa CCM alikuwa ni Dk. William Shija ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola. Katika kesi hiyo, Dk. Masha alikuwa akitetewa na Wakili maarufu nchini, Mabere Marando wakati serikali ilikuwa ikiwakilishwa na mawakili wake wawili, Ewin Kakolaki na Dora Komba.
Kesi hiyo kwa mara ya kwanza ilifunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam mwaka 2001 na baadaye kuhamishiwa katika Mahakama Kuu ya Kanda ya Mwanza ambako ni jirani na eneo la tukio hilo, nia ikiwa ni kuupata ushahidi na kuharakisha shauri hilo ambalo lilisajiliwa kwa namba 10/2006. Hata hivyo, mahakama hiyo imeacha wazi nafasi ya serikali kukata rufaa endapo kwa namna moja ama nyingine haikuridhika na uamuzi huo.