Serikali kumlipa fidia baba wa Waziri Masha

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Serikali kumlipa fidia baba wa Waziri Masha

Nashon Kennedy, Mwanza
Daily News; Monday,December 22, 2008 @21:15

Aliyekuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Sengerema mkoani hapa kupitia chama cha United Democratic (UDP) mwaka 2000, Dk. Fortunatus Masha, ameshinda kesi yake dhidi ya serikali bada ya serikali kuamuriwa kumlipa fidia ya Sh milioni 50 kutokana na kipigo cha polisi alichokipata wakati wa uchaguzi huo.

Masha ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa UDP Taifa, alifungua shauri hilo mwaka 2006, katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, akidai alipwe fidia ya Sh bilioni moja kutokana na kupigwa na askari Polisi wa wilayani Sengerema Oktoba 31, 2000 wakati wa Uchaguzi Mkuu wa rais, wabunge na madiwani.

Kwa mujibu wa Msajili wa Mahakama Kanda Kuu ya Mwanza, Frederica Mgaya, hukumu hiyo ilitolewa Desemba 16, mwaka huu na Jaji A. Sumari. Dk. Masha ni baba wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, ambaye inadaiwa wakati wa tukio hilo la mwaka 2000, alikuwa pamoja na baba yake.

Dk. Masha ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Afrika Mashariki, alikuwa akimlalamikia Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutokana na kupigwa na polisi wakati huo wa uchaguzi, ambao mgombea wa CCM alikuwa ni Dk. William Shija ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola. Katika kesi hiyo, Dk. Masha alikuwa akitetewa na Wakili maarufu nchini, Mabere Marando wakati serikali ilikuwa ikiwakilishwa na mawakili wake wawili, Ewin Kakolaki na Dora Komba.

Kesi hiyo kwa mara ya kwanza ilifunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam mwaka 2001 na baadaye kuhamishiwa katika Mahakama Kuu ya Kanda ya Mwanza ambako ni jirani na eneo la tukio hilo, nia ikiwa ni kuupata ushahidi na kuharakisha shauri hilo ambalo lilisajiliwa kwa namba 10/2006. Hata hivyo, mahakama hiyo imeacha wazi nafasi ya serikali kukata rufaa endapo kwa namna moja ama nyingine haikuridhika na uamuzi huo.
 
Kwa mujibu wa Msajili wa Mahakama Kanda Kuu ya Mwanza, Frederica Mgaya, hukumu hiyo ilitolewa Desemba 16, mwaka huu na Jaji A. Sumari. Dk. Masha ni baba wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, ambaye inadaiwa wakati wa tukio hilo la mwaka 2000, alikuwa pamoja na baba yake.

- Muandishi angekua mkweli tu kuwa wote wawili baba na mtoto, walikula kipigo na wote walitupwa rumande mpaka kesho yake walipotolewa kwa dhamana kwa kujaribu kushindana na Shija, aliyekua waziri kwenye serikali ya Mwinyi na Mkapa pia.
 
Duh!! Katika suala hili la kupigwa kwa wananchi wote wangelipwa (Mil50) serikali yetu ingekuwa mufilisi kwa sababu ni watu wengi sana wanapigwa, sasa naona uchaguzi wa 2010 itabidi tuwe tunatembea na video kamera ili kurekodi kila kitu na kurudi kudai mahakamani, nadhani hapo matendo ya kupigana yatapungua sasa.
 
Duh!! Katika suala hili la kupigwa kwa wananchi wote wangelipwa (Mil50) serikali yetu ingekuwa mufilisi kwa sababu ni watu wengi sana wanapigwa, sasa naona uchaguzi wa 2010 itabidi tuwe tunatembea na video kamera ili kurekodi kila kitu na kurudi kudai mahakamani, nadhani hapo matendo ya kupigana yatapungua sasa.

Watu wanaendelea kupigwa, kuuawa au kuporwa mali zao. Na serikali au baadhi ya watu walioko serikali pia wanafanya hivyo na haki haitendeki, kuna wengine wanafungwa kwa kubambikiziwa kesi na kufanyiwa unyama mwingi tu. Hii ndio Tanzania yetu, wajanja wanaweza kulipwa wanyonge wataendelea kunyongwa. Kwa hiyo huyu jamaa inawezekana amelipwa kutokana na kuwa sasa kidogo yuko kwenye system and mwanae yuko huko, lakini angekuwa nje hata madai yake yasingesikilizwa.
 
Dk. Fortunatus Masha ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Afrika Mashariki.

Naomba kuuliza aliingia bungeni kwa tiketi ya chama gani mwishoni mpaka akaenda bunge la E.A?
 
Duh!! Katika suala hili la kupigwa kwa wananchi wote wangelipwa (Mil50) serikali yetu ingekuwa mufilisi kwa sababu ni watu wengi sana wanapigwa, sasa naona uchaguzi wa 2010 itabidi tuwe tunatembea na video kamera ili kurekodi kila kitu na kurudi kudai mahakamani, nadhani hapo matendo ya kupigana yatapungua sasa.

Kwa yaliyotokea Tarime! LISU tafadhali saidia...
 
Dk. Fortunatus Masha ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Afrika Mashariki.

Naomba kuuliza aliingia bungeni kwa tiketi ya chama gani mwishoni mpaka akaenda bunge la E.A?

Kama unaamanisha kuingia Bunge la Tanzania, Mzee Masha hayumo humo wkani wabunge wa A. Mash hawatokani na wabunge wa nchi husika, wanachagukliwa kutoka nje ya Bunge. Huyu alipigiwa kampeni na watu wa CCM (nadhani mwanawe alihusika kwenye kuinjinia mzee apate nafasi hiyo)
 
Kama unaamanisha kuingia Bunge la Tanzania, Mzee Masha hayumo humo wkani wabunge wa A. Mash hawatokani na wabunge wa nchi husika, wanachagukliwa kutoka nje ya Bunge. Huyu alipigiwa kampeni na watu wa CCM (nadhani mwanawe alihusika kwenye kuinjinia mzee apate nafasi hiyo)



Ok shukrani ,maana mimi nilikuwa naelewa siku zote wabunge wa Jamuhuri ndio wanabigiana kura kutoa wanaoenda kwenye bunge la E.A na nakumbukumbu kama hiyo .

Ok vyema ,kumbe alirudi chichiemu apate urahisi.
 
Ok shukrani ,maana mimi nilikuwa naelewa siku zote wabunge wa Jamuhuri ndio wanabigiana kura kutoa wanaoenda kwenye bunge la E.A na nakumbukumbu kama hiyo .

Ok vyema ,kumbe alirudi chichiemu apate urahisi.

Wabunge wetu hao, wanaangalia maslahi yao tu, na si kutetea wananchi kama wanavyojinadi. Ni nani anaweza kutumia mamilioni ya pesa zake kupiga kampeni eti ili awatetee wananchi?
 
Ok shukrani ,maana mimi nilikuwa naelewa siku zote wabunge wa Jamuhuri ndio wanabigiana kura kutoa wanaoenda kwenye bunge la E.A na nakumbukumbu kama hiyo .

Ok vyema ,kumbe alirudi chichiemu apate urahisi.

Hajarejea CCM. Wabunge wa A Mash kutoka TZ wanapigiwa kura na wabunge wa Tanzania. kwa utaratibu uliopo, kunakuwa na wanne kutoka CCM na mmoja anatoka upinzani, nafasi ya upinzani ndio kaipata baba wa masha lakini kwa kupigiwa kura ya wabunge wengi wa CCM
 
Duh!! Katika suala hili la kupigwa kwa wananchi wote wangelipwa (Mil50) serikali yetu ingekuwa mufilisi kwa sababu ni watu wengi sana wanapigwa, sasa naona uchaguzi wa 2010 itabidi tuwe tunatembea na video kamera ili kurekodi kila kitu na kurudi kudai mahakamani, nadhani hapo matendo ya kupigana yatapungua sasa.

Mobile phone zitawamaliza
 
Back
Top Bottom