Serikali kulamba mkopo mwingine kutoka Benki ya Biashara ili kufanikisha ujenzi wa SGR

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,444
7,808
Mwigulu Nchemba.jpg
CITI BANK imeahidi kuisaidia Tanzania kupata mikopo yenye masharti nafuu kutoka katika Benki hiyo pamoja na washirika wake kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ukiwemo mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) pamoja na kuahidi kuwa balozi wa kutafuta wawekezaji wataowekeza mitaji na teknolojia hapa nchini.

Ahadi hiyo imetolewa Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa wa Benki hiyo anayesimamia nchi za Afrika-Kusini mwa Jangwa la Sahara, Bw. Akinsowon Dawodu, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb).

Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa, Dkt. Mwigulu Nchemba, aliishukuru Benki hiyo kwa kuwasilisha mapendekezo yake serikalini kuhusu namna ya kufanikisha ujenzi wa mradi mkubwa wa Reli ya Kisasa ambao utakuwa na manufaa makubwa kiuchumi si tu kwa Tanzania, bali nchi nyingine zinazopakana na Tanzania ambazo hazipakani na Bahari.

Alieleza kuwa Mkandarasi atakayejenga kipande cha Reli ya Kisasa kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi mkoani Tabora amepatikana na mkandarasi atayejenga reli hiyo kutoka Isaka hadi Mwanza yuko katika eneo la mradi na Mkandarasi atakayejenga reli kuanzia Isaka hadi Tabora atapatikana muda si mrefu kuanzaia sasa.

“Dira ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuona kuwa Reli ya Kisasa ya kuanzia Makutopora (Singida) hadi Mpaka Mwanza na kuanzia Tabora hadi Kigoma, ijengwe sambamba na kwa kasi, wakati huohuo Reli ya Kusini mwa Tanzania kutoka Bandari ya Mtwara hadi Mbamba bay kuelekea nchi za SADC zilizoko ukanda huo ziweze kufikiwa na reli hiyo” alieleza Dkt. Nchemba

CHANZO: Wizara ya Fedha
 
Mkopo sio shida ila kweli hela intaelekezwa kwenye kazi elio pangwa? Au kwenye miradi mingine ya uchaguzi
 
Daraja ya tanzanite tayari..machoyetu sasa kwenye SGR..daraja la busisi na NHD..kopeni ibeni ila tunahitaji hiyo miradi ikamilike kwa wakati.

Narudia tena ikamilike kwa wakati na katika viwango sahihi.

Mana ni miradi yenye faida kwa nchi yetu.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu unakuta jitu linaiba hela za umma linakula bata na Malaya.... Jitu kama hili likitiwa ndani au kupotezwa tunaanza mambo ya haki za binadamu...
 
CITI BANK imeahidi kuisaidia Tanzania kupata mikopo yenye masharti nafuu kutoka katika Benki hiyo pamoja na washirika wake kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ukiwemo mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) pamoja na kuahidi kuwa balozi wa kutafuta wawekezaji wataowekeza mitaji na teknolojia hapa nchini.

Ahadi hiyo imetolewa Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa wa Benki hiyo anayesimamia nchi za Afrika-Kusini mwa Jangwa la Sahara, Bw. Akinsowon Dawodu, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb).

Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa, Dkt. Mwigulu Nchemba, aliishukuru Benki hiyo kwa kuwasilisha mapendekezo yake serikalini kuhusu namna ya kufanikisha ujenzi wa mradi mkubwa wa Reli ya Kisasa ambao utakuwa na manufaa makubwa kiuchumi si tu kwa Tanzania, bali nchi nyingine zinazopakana na Tanzania ambazo hazipakani na Bahari.

Alieleza kuwa Mkandarasi atakayejenga kipande cha Reli ya Kisasa kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi mkoani Tabora amepatikana na mkandarasi atayejenga reli hiyo kutoka Isaka hadi Mwanza yuko katika eneo la mradi na Mkandarasi atakayejenga reli kuanzia Isaka hadi Tabora atapatikana muda si mrefu kuanzaia sasa.

“Dira ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuona kuwa Reli ya Kisasa ya kuanzia Makutopora (Singida) hadi Mpaka Mwanza na kuanzia Tabora hadi Kigoma, ijengwe sambamba na kwa kasi, wakati huohuo Reli ya Kusini mwa Tanzania kutoka Bandari ya Mtwara hadi Mbamba bay kuelekea nchi za SADC zilizoko ukanda huo ziweze kufikiwa na reli hiyo” alieleza Dkt. Nchemba

CHANZO: Wizara ya Fedha
Wapi walipoandika kwamba Serikali itakopa kwa masharti ya kibiashara?

Hapo huyo director ameleta mapendekezo ya kuona kama Serikali wanaweza Kukopa kwao so ni juu ya serikali kuamua Kukopa au hapana kulingana na masharti..

Hakuna mkopo wa kibiashara unakopwa Nje ya Nchi na Mama, mikopo ya biashara imekopwa ndani ya Nchi tuu.
 
Wapi walipoandika kwamba Serikali itakopa kwa masharti ya kibiashara?

Hapo huyo director ameleta mapendekezo ya kuona kama Serikali wanaweza Kukopa kwao so ni juu ya serikali kuamua Kukopa au hapana kulingana na masharti..

Hakuna mkopo wa kibiashara unakopwa Nje ya Nchi na Mama, mikopo ya biashara imekopwa ndani ya Nchi tuu.

Nimeandika kutoka benki ya biashara na si masharti ya kibiashara.. Labda utuambie City Bank sio commercial bank..
 
CITI BANK imeahidi kuisaidia Tanzania kupata mikopo yenye masharti nafuu kutoka katika Benki hiyo pamoja na washirika wake kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ukiwemo mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) pamoja na kuahidi kuwa balozi wa kutafuta wawekezaji wataowekeza mitaji na teknolojia hapa nchini.

Ahadi hiyo imetolewa Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa wa Benki hiyo anayesimamia nchi za Afrika-Kusini mwa Jangwa la Sahara, Bw. Akinsowon Dawodu, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb).

Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa, Dkt. Mwigulu Nchemba, aliishukuru Benki hiyo kwa kuwasilisha mapendekezo yake serikalini kuhusu namna ya kufanikisha ujenzi wa mradi mkubwa wa Reli ya Kisasa ambao utakuwa na manufaa makubwa kiuchumi si tu kwa Tanzania, bali nchi nyingine zinazopakana na Tanzania ambazo hazipakani na Bahari.

Alieleza kuwa Mkandarasi atakayejenga kipande cha Reli ya Kisasa kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi mkoani Tabora amepatikana na mkandarasi atayejenga reli hiyo kutoka Isaka hadi Mwanza yuko katika eneo la mradi na Mkandarasi atakayejenga reli kuanzia Isaka hadi Tabora atapatikana muda si mrefu kuanzaia sasa.

“Dira ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuona kuwa Reli ya Kisasa ya kuanzia Makutopora (Singida) hadi Mpaka Mwanza na kuanzia Tabora hadi Kigoma, ijengwe sambamba na kwa kasi, wakati huohuo Reli ya Kusini mwa Tanzania kutoka Bandari ya Mtwara hadi Mbamba bay kuelekea nchi za SADC zilizoko ukanda huo ziweze kufikiwa na reli hiyo” alieleza Dkt. Nchemba

CHANZO: Wizara ya Fedha
kama fedha hizo zitasimamiwa kwa ueledi kwa kweli nchi itafunguka lkn kama upigaji utaendelea natabiri hali itakuwa mbaya sana huko mbeleni sababu fedha nyingi za ndani zitatumika kuservice haya mamikopo na miradi mingine itasimama.
 
Kwani zile trillion 2 za kodi wanazo jisifia kukusanya kila mwezi kupitia TRA, zinapelekwa wapi? Achilia mbali zile tozo kandamizi kwenye mafuta naiamala ya simu.
 
Magufuli muda wote alidanganya kwamba ni fedha za ndani akijua kabisa kwamba anasema uongo huku bado akisema msema kweli ni mpenzi wa Mungu. What a hypocrisy.
 
kama fedha hizo zitasimamiwa kwa ueledi kwa kweli nchi itafunguka lkn kama upigaji utaendelea natabiri hali itakuwa mbaya sana huko mbeleni sababu fedha nyingi za ndani zitatumika kuservice haya mamikopo na miradi mingine itasimama.
Upigwaji upo ndio maana kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake
 
Back
Top Bottom