Serikali kukata rufaa upya, kupinga mgombea huru.

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
habari Leo

SERIKALI kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu imeanza taratibu za kuwasilisha tena rufani inayopinga mgombea binafsi baada ya Mahakama ya Rufaa kutupa rufani yao kutokana na kubaini kasoro kadhaa.

Alhamisi iliyopita, Mahakama ya Rufaa ilitupa rufani ya serikali inayopinga mgombea binafsi baada ya kubaini kasoro kadhaa katika rufani iliyowasilishwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Akizungumza na gazeti hili jana, Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe alisema taratibu hizo zilianza mwisho wa wiki iliyopita, ikiwa ni siku moja baada ya uamuzi huo wa Mahakama ya Rufaa.

Mbali na kuwasilisha rufani yao, Waziri alisema lengo la kupinga uamuzi huo wa Mahakama Kuu wa kuruhusu mgombea binafsi wa urais na ubunge ni kutaka uamuzi kama huo utolewe na mahakama ya juu zaidi nchini ambayo ni Mahakama ya Rufaa.

Alipoulizwa kama Mahakama ya Rufaa ikitoa uamuzi sawa na wa Mahakama Kuu wa kuruhusu mgombea huyo binafsi, Chikawe alisema “serikali haitapinga na itatekeleza mabadiliko ya sheria na kuyawasilisha bungeni kwa kipindi ambacho mahakama itaamuru.”

Awali katika hukumu ya Mahakama Kuu iliamriwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kufanya marekebisho ya Sheria Namba 34 ya 1994 ambayo inapingana na kifungu cha 21 (1) cha Katiba ambacho kinampa haki ya kugombea na kupiga kura.

Mahakama Kuu ilimpa Mwanasheria Mkuu kati ya Mei 5, 2006 hadi uchaguzi ujao awe imewasilisha bungeni sheria inayotoa fursa ya kuwapo mgombea binafsi katika uchaguzi bila kutegemea chama chochote.

Kutokana na uamuzi huo wa Mahakama Kuu uliotolewa na majaji Amir Manento, Salum Massati na Thomas Mihayo, serikali ilikata rufaa ambapo inadai Mahakama Kuu ilikosea kisheria katika kutafsiri Ibara ya 21 (1) ( c ), 39 (1) (c ) (b) na 69 (1) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinachompa haki mtu ya kugombea na kupiga kura.

Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa John Mroso, Edward Rutakangwa na Engela Kileo walitoa hukumu ya kutupilia mbali rufaa ya serikali, hali iliyompa ushindi tena Mwenyekiti wa Democratic Party, (DP), Christopher Mtikila, ambaye amekuwa anahangaika na kuruhusiwa mgombea binafsi tangu mwaka 1993.

Mtikila baada ya kubaini kuwa kuna kasoro katika rufani ya serikali, aliwalisilisha pingamizi mahakamani hapo akidai kuwa ina kasoro kutokana na tarehe iliyoko kwenye amri ya hukumu kuwa tofauti na tarehe iliyoko kwenye hukumu ya Mahakama Kuu.

Katika pingamizi hilo, Mtikila kupitia kwa mawakili wake Richard Rweyongeza na Mpale Mpoki, waliliambia jopo la majaji hao kuwa rufaa hiyo haikuwa na rutuba ya kisheria kutokana na dosari hizo za tarehe tofauti kwenye amri na kwenye hukumu ya mahakama hivyo wakaiomba mahakama kukataa kusikiliza rufani hiyo.

Majaji walikubaliana na hoja za mawakili wa Mtikila wakisema kuwa amri hiyo (kikaza hukumu) ilikuwa hairekebishiki kwa kuwa ilitengenezwa Februari mosi mwaka jana wakati hukumu ya Mahakama Kuu juu ya suala hilo ilitolewa Mei 5, 2006.

Wanasheria Waandamizi, Joseph Ndunguru na Mathew Mwaimu waliokuwa wanaiwakilisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, waliiomba mahakama kukataa pingamizi hilo la Mtikila kwa vile suala hilo liliwasilishwa Mahakama Kuu chini ya sheria za haki za binadamu ambayo haihitaji kuwasilisha amri ya hukumu.

Kwa mujibu wa wanasheria hao walidai kilichokuwa kinabishaniwa siyo agizo la hukumu, bali maamuzi ya mahakama nyingine kwa hiyo hapakuwapo na sheria inayotaka tarehe iliyoko katika amri ya hukumu iwe sawasawa na ile iliyoko katika hukumu kama sheria inavyoelekeza kwenye agizo la hukumu.

Majaji kwa upande wao walisema maamuzi kama hayo yanaendana na sheria za mwenendo wa kesi za madai zinazohitaji amri ya hukumu yoyote ionyeshe tarehe inayofanana na ile iliyoko kwenye hukumu.

Mtikila alifungua kesi hiyo Februari 17, 2005 akiiomba mahakama kutamka kuwa ni kinyume cha Katiba ya nchi kupinga kuwapo kwa mgombea binafsi katika nafasi za kisiasa.

Katika uamuzi wa Mahakama Kuu, jopo la majaji watatu liliruhusu kuwapo kwa mgombea binafsi katika uchaguzi, kwa sababu katiba ya nchi inatoa haki hiyo.

Majaji hao walibainisha kuwa katiba inatamka wazi kuwa kila mwananchi anayo haki ya kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi na haiweki masharti kuwa hilo lifanyike kwa mtu kujiunga na chama fulani.

Mwaka 1993, Mtikila alishinda kesi kama hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, lakini licha ya uamuzi huo wa mahakama, Bunge lilishindwa kutunga sheria ya kuruhusu mgombea binafsi na ndipo Mtikila alifungua kesi hiyo ya kikatiba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na kushinda tena.

My Take:

Nyerere aliwaambia pale Uwanja wa Sokoine kuwa uamuzi wa serikali kufuta haki ya mtu kuchaguliwa kwa vile hataki kujiunga na chama ni uamuzi wa kipumbavu. He was right and still is. Kama mtu ambaye hana chama anaweza kupiga kura kumchagua kiongozi amtakaye, iweje mtu asiye mwanachama anyang'anywe haki ya kupigwa kura na watu wanaomtaka? Haki ya kuchagua na ile ya kuchaguliwa inatokana na haki ya raia. Kama raia anayo haki ya kumchagua amtakaye basi anayo haki pia ya yeye mwenyewe kuchaguliwa na yeyote yule.

Kwanini hata hivyo CCM inahofia sana mgombea binafsi? au wanakumbuka yale ya Chifu Sarwat wa Mbulu.
 
As Mark Twain said "The law is an ass", the high wired technical acts by The Executive's lawyers only further exposes their masters' ignoble ambitions and sense of shameless protectionist entitlement.

I have said in the past and will continue to say that denying Tanzanians the right to elected office just because they do not affiliate with any political party is not only simply unconstitutional, but also a gross violation of human rights, fairness and all decent conduct by civilized societies.The constitution guarantees Tanzanians of age and sane mind the right to stand in elections, the constitution, supposedly mother of all laws, does not mention that a Tanzanian needs to be affiliated to any party. In this matter, The Executive is in direct and clearly undisputable violation of Article 1 of the United Nations Universal Declaration of Human Rights.

It is a shame to see that out of a cannibalistic greed and insatiable power grip the Tanzanian Government is promoting gross violations of the Constitution even after the correct and detailed advise of such eminent people like Nyerere and Nyalali, representing a wider consensus of many individuals and institutions, chief of all the Judiciary which is entrusted with interpreting The Constitution, never mind countless pleas from the civil society, opposition parties and grassroot organizations.

When a pillar of the state such as the Executive chooses to ignore the Judiciary, then under the auspices of the Nyalali Commission, in the process cherry picking what was politically convenient for them and discarding any attempt at a serious look of the status quo, the political manipulation becomes not only juvenile and obvious, but also a dangerous precedent.

The case for private candidacy is not complicated, it is an unspinnable constitutionaly guaranteed right that only a shameless dingbat can attempt to contest, or as this case appears to be, delay .No wonder they are stammerring in the presentation of the government's case, I am curious to find out what are they going to spin this with. the above article potrays a self defeating attitude on the part of the Tanzanian Executive arm of the state, as if they are just stalling for time and would do anything if only to delay this and have a private candidate free 2010.
 
Hii inaonyesha jinsi vipaumbele vya sirikali vilivyo na kasoro. Wakati hadi hii leo wameshindwa kuwafungulia mashtaka mafisadi waliokupua mabilioni ya shilingi pale BoT, lakini wamekimbia haraka sana mahakamani ili kuwanyima haki yao Watanzania wasio na vyama ambao ndio wengi Tanzania kugombea nafasi ya ubunge au urais.
 
wakikubali mgombea binasfi ina maana ndio mwisho wa yafuatayo
1,ruzuku kwa vyama
2,wabunge kupitia viti maalumu
3,kudibiti wabunge wao
 
wakikubali mgombea binasfi ina maana ndio mwisho wa yafuatayo
1,ruzuku kwa vyama
2,wabunge kupitia viti maalumu
3,kudibiti wabunge wao

Kwa maoni yangu, ruzuku kwa vyama inabidi iendelee, wabunge kupitia viti maalum pia wanaweza kuchaguliwa ambao si wafuasi wa vyama vyovyote. Hili la kuwadhibiti wabunge mimi siku zote nalipinga kwa sababu wabunge pamoja na kuwa ni wanachama wa chama cha siasa lakini wapo bungeni kwa maslahi ya nchi. Kwa mantiki hiyo basi, kama wanaona maslahi ya nchi yanaathirika kutokana na mamuzi ya chama chao, basi wawe huru kukikemea chama chao bila mtafaruku wowote.
 
Nataka kugombea huru na hawa CCM wnajifanya kuchelewesha mambo. Kwa hili kwa kweli hawaliwezi hata wafanyeje mgombea binafsi lazima. Nami nitagombea
 
wakikubali mgombea binasfi ina maana ndio mwisho wa yafuatayo
1,ruzuku kwa vyama
2,wabunge kupitia viti maalumu
3,kudibiti wabunge wao

mkuu katibu tarafa..

Hivi vyote havihitajiki...

Serikali ifute ruzuku ya vyama vyote ikiwemo ccm. Majengo na biashara zote za ccm ilizojipatia kabla ya mfumo wa vyama vingi virudishwe serikalini na kisha ccm ilipe riba ya kutumia mali ya watanzania wote kuanzia mwaka 1992 hadi leo.

Mengine zaidi yatafuata... wabunge wa kupitia viti maalumu nao wafutwe tu kwa sasa. Kila mtu agombee kupata nafasi ya kuwa mbunge.
 
Kikubwa hapa wakikubali CCM itakuwa mashakani maana utovu wa nidhamu(Mtu kusema anachokiamini) vitakuwa nje nje.

Na unayemsikia anakataa hili target yake ni kuhakikisha hakuna uhuru. Unaweza kushangaa kwa hali ilivyo na mafisadi walivyojificha nyuma ya CCM, wakiachia wagombea binafsi wote waliowazuri wanakimbia chama na kuacha mafisadi tu sasa hao watakuwa wageni wa nani?

Ukiona hili limekubalika ujue ndio mwanzo wa maendeleo ya watanzania. Tutakuwa tumeondokana na utumwa.
 
Nadhani isomeke CCM KUKATA RUFAA UPYA, KUPINGA MGOMBEA HURU.
lakini kwa kuwa serikali ni ya viongozi basi tuseme serikali imekataa mgombea binafsi, wanatumia nguvu nyingi na kodi zetu kuizima democrasia. ninashaka pia na mahakama ya rufaa kutenda haki, bado jinamizi la kupanguliwa kwa kesi za mwalusanya linanizonga.
Serikali inaumwa gonjwa la MNYONG'ONYO
 
Nadhani isomeke CCM KUKATA RUFAA UPYA, KUPINGA MGOMBEA HURU.
lakini kwa kuwa serikali ni ya viongozi basi tuseme serikali imekataa mgombea binafsi, wanatumia nguvu nyingi na kodi zetu kuizima democrasia. ninashaka pia na mahakama ya rufaa kutenda haki, bado jinamizi la kupanguliwa kwa kesi za mwalusanya linanizonga.
Serikali inaumwa gonjwa la MNYONG'ONYO

My take ni kuwa beneficiaries wakubwa wa uamuzi huu wa Mahakama ni Tanzania na watanzania. Na casualty mkubwa ni CCM, kwa sababu ndani ya CCM kuna watu wengi sana wenye uwezo wa kuiweka nchi yetu kwenye mkondo uliosahihi, lakini ili waweze kudhibitiwa na kufungwa midomo ni lazime wawe wananongea kwa mandate ya CCM na kwa mtazamo wa CCM. Kinyume cha hapo hata kama uko sahihi na na chama kiko wrong, kitu ambacho kimetokea mara nyingi, utaonekana unakurupuka au sio msimamo wa chama (kama alivyosema Mzee Kingunge)
Tungekuwa na mambo ya Private candidate ufisadi mwingi uliofichika sasa ungewekwa wazi, huenda tungekuwa na watu wa Slaa type zaidi ya 100. NI obvious kuwa kama mtu unaishiwa hoja sio rahisi kupambana kwa nguvu ya hoja, Sitta anakumbuka vizuri hii issue aliishiwa hoja alipokuwa waziri wa sheria na katiba akatumia ujanja ujanja, na kuifanya serikali kukataa kutekeleza uamuzi wa mahakama na kwenda kinyume cha katiba.
Pamoja na kuwa it is provided kwenye katiba, lakini sahau kabisa kama itakubalika.
 
Hivi CCM wanakiuka sheria gani kukata rufaa?..ama ndio sheria yenyewe inavyoruhusu.
Nitarudia tena huu ni upotezaji muda na kodi za wananchi kwa pande zote toka Mtikila mwenye aliyepeleka madai ya awali. Hizi siasa za kipuuzi zinanichosha kabisa...
Naomba mnipe hizo faida tutakazo zipata wananchi kutokana na sheria hii ya wagombea binafsi..
 
Hivi CCM wanakiuka sheria gani kukata rufaa?..ama ndio sheria yenyewe inavyoruhusu.
Nitarudia tena huu ni upotezaji muda na kodi za wananchi kwa pande zote toka Mtikila mwenye aliyepeleka madai ya awali. Hizi siasa za kipuuzi zinanichosha kabisa...
Naomba mnipe hizo faida tutakazo zipata wananchi kutokana na sheria hii ya wagombea binafsi..

Faida namba moja:

Hakutakuwa na haja ya kutumia pesa za wizi toka BoT kama vile ccm walivyotumia wakati wa uchaguzi. Wagombea watakuwa huru kuchangisha pesa toka kwa wafuasi wao na watapunguza suala la sasa la kufunga watu kwenye sera na matamko ya vyama kwa vile tu watategemea hivyo vyama kwenye chaguzi.
 
Kwani wakiingia wagombea binafsi CCM hawataruhusiwa kugombea?...
CCM wameiba fedha benki kuu hao kina CUF, Chadema, Na huyo Mtikila wapo kwenye uchaguzi mkuu itakuwaje mtu binafsi awe sababu ya kuondoa wizi BoT.
 
hivi serikali kukata rufaa wamepinda sheria? jee kama hawajapinda sheria kuna kosa gani na sababau zipi za kuogopa?
 
Kwani wakiingia wagombea binafsi CCM hawataruhusiwa kugombea?...
CCM wameiba fedha benki kuu hao kina CUF, Chadema, Na huyo Mtikila wapo kwenye uchaguzi mkuu itakuwaje mtu binafsi awe sababu ya kuondoa wizi BoT.

Wagombea wa ccm wataendelea kugombea ila hawatazuia wanaccm wasiopenda ufisadi kubaki ndani ya chama.
 
Hivi CCM wanakiuka sheria gani kukata rufaa?..ama ndio sheria yenyewe inavyoruhusu.
Nitarudia tena huu ni upotezaji muda na kodi za wananchi kwa pande zote toka Mtikila mwenye aliyepeleka madai ya awali. Hizi siasa za kipuuzi zinanichosha kabisa...
Naomba mnipe hizo faida tutakazo zipata wananchi kutokana na sheria hii ya wagombea binafsi..

Mkandara,

Faida ya kwanza, kuna wanachama wengi wa CCM kwenye uongozi ambao wamechoshwa na CCM lakini hawana chama kingine kizuri cha kujiunga nacho, wanaweza kuuzika kwa wananchi kama watu binafsi.Watu hawa ambao ufisadi wa CCM umewachosha kwa sasa wanalazimika kugombea ubunge, urais na nafasi nyingine kwa tiketi ya kifisadi ya CCM ambayo inakuja na masharti kibao yanayowaondolea independence na integrity yao.

Kwa hiyo faida moja itakuwa siasa zitakuwa na uhuru zaidi.

Faida ya pili hata kina sie ambao hatujaona chama chochote cha kujiunga nacho tutaweza kupata nafasi na haki yetu ya kugombea uongozi.Mimi binafsi siamini katika organizations na ninaamini zaidi katika "the power of individualism", katika mfumo wa sasa itabidi nikubali katiba nisizozielewa naku pay some lip service kwa policies ambazo siziamini.Mimi nataka niwe na nafasi ya kwenda kuongea na wananchi wa Tanzania kama mimi, ukiingia bungeni kama unataka kublast unablast tu hakuna upumbavu wa vikao vya discipline vya chama wala nini.

Kama sheria ya mgombea binafsi ingekuwepo 2005 huyu rais wetu bogus asingeweza kupata urais kirahisi hivi, na pengine mtu kama Salim angeweza kumchallenge kama mgombea binafsi.

Kukatalia wagombea binafsi siyo tu kunawanyima Watanzania wasio na vyama nafasi ya kuchaguliwa, bali pia vinawanyima Watanzania wigo mkubwa wa watu wa kuwachagua.

On closer examination not having a private candidate is at best constitutional but a violation of human rights, the very rights the constitution is entrusted with protecting, as stated above.

At worst the constitution is contradicting its earlier spirit (Ibara ya 2) katika ibara za 5, 39 na 67.

21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39.
ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya
kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki
katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya
Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa
nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi
waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia
utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria

5.-(1) Kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka
kumi na minane anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi
unaofaywa Tanzania na wananchi. Na haki hii itatumiwa kwa
kufuata masharti ya ibara ndogo ya (2) pamoja na masharti
mengineyo ya Katiba hii na ya Sheria inayotumika nchini
Tanzania kuhusu mambo ya uchaguzi.
(2) Bunge laweza kutunga sheria na kuweka masharti
yanayoweza kuzuia raia asitumie haki ya kupiga kura kutokana
na yoyote kati ya sababu zifuatazo, yaani raia huyo-
(a) kuwa na uraia wa nchi nyingine;
(b) kuwa na ugonjwa wa akili;
(c) kutiwa hatiani kwa makosa fulani ya jinai;
(d) kukosa au kushindwa kuthibitisha au kutoa
kitambulisho cha umri, uraia au uandikishwaji kama
mpiga kura,
mbali na sababu hizo hakuna sababu nyingine yoyote
inayoweza kumzuia raia asitumie haki ya kupiga kura.

39.-(1) Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama-
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa
mujibu wa Sheria ya Uraia.
(b) ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa;
(d) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe
wa Baraza la Wawakilishi,
(e) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya
Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika
Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa
kodi yoyote ya Serikali.

(2) Bila ya kuingilia haki na uhuru wa mtu kuwa na maoni
yake, kuamini dini atakayo, kushirikiana na wengine na kushiriki
shughuli za umma kwa mujibu wa sheria za nchi, mtu yeyote
hatakuwa na sifa za kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa
Jamhuri ya Muungano kama si mwananchama na mgombea
aliyependekezwa na chama cha siasa.



 
Pundit,

Sioni vifungu vinavyo jipinga. Hebu nionyeshe. Koti imesema vipo, najua uko right, lakini ni wapi haswa?
 
Kwa mujibu wa gazeti la mtanzania la leo makamu m/kiti anaunga mkono uwepo wa wagombea binafsi na akiwa anabainisha ni kumuenzi nyerere kwa vitendo.

Huu mwanzo mzuri.Na ni vema tunahakikisha rufaa inashindwa kwa kuwa lengo liwe kuboresha na si kunyonga demokrasia.

Kwa wataalam wa sheria hapa JF Nina swali dogo. Je pale itakapotungwa sheria ya kuruhusu wagombea binafsi, je ikitokea mbunge aliyechaguliwa kupitia chama say cuf, tlp, ccm au chadema akaachia ngazi uanachama kwa sababu yoyote ile ataendelea kuwa mbunge, au utakomea hapo kama ilivyokuwa kwa mrema alipoiama ccm?Naomba jibu
 
Tufanye maandalizi ya kutosha KIFIKRA na KIMTAZAMO kwa Watanzania tulio wengi. Vinginevyo tujiandae kuwa na Wabunge na Maraisi kama Manji, Mengi, RA, Gachuma, Diallo, Bakhresa,Chenge, Lowassa, n.k., kwa sababu ya "vijisenti" vyao vs umasikini wetu. Binafsi nakubali mgombea huru hadi ngazi ya UBUNGE.
 
Last edited:
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom