Serikali kukata rufaa kupinga hukumu ya ATCL kulipa mabilioni

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Serikali imesema imeanza mchakato wa kukata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Uingereza dhidi ya Shirika la Ndege la Tanzania(ATCL).

ATCL imeamriwa kulipa Dola 30.1 milioni (Sh69.23bilioni) kwa kampuni moja ya Liberia kama fidia baada ya kuvunjika kwa mkataba wa kukodisha ndege.

Kesi hiyo inahusu makubaliano yaliyofikiwa mwaka 2013 na aliyekuwa Mkurugenzi wa ATCL, David Mattaka ya kukodisha ndege aina ya Airbus kutoka kampuni ya Willis Trading.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Uingereza, Christopher Butcher aliiamuru ATCL kulipa fedha hizo pamoja na riba inayoweza kufikia dola 10 milioni (Sh23 bilioni) kwa kampuni hiyo ya Liberia, ambayo inajishughulisha na masuala ya kuuza na kukodisha ndege, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa.

Hata hivyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Adelardus Kilangi aliliambia Mwananchi kuwa mkataba wenyewe ulikuwa wa kifisadi wa kuitia nchi hasara.

Dk Kilangi alisema kuwa serikali imewasiliana na ofisi yake, ambayo imeanza mchakato wa kukata rufaa. “Tumeanza mchakato wa kukata rufaa na tunazingatia sheria na taratibu za Uingereza,” aliongeza.

Dk Kilangi alieleza kuwa hukumu hiyo imewashangaza kutokana na ukweli kuwa ndege yenyewe ilitumika kwa miezi saba tu. “Hawa watu wameibia nchi na tutapambana mahakamani kuhakikisha tunashinda kesi hii,” alisisitiza Kilangi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, Leonard Chamuriho na Ofisa Mkuu Mtendaji wa ATCL, Ladislaus Matindi wote hawakutaka kuzungumzia suala hilo walipotafutwa kwa njia ya simu.

Kampuni ya Willis Trading iliwasilisha madai yake kwenye Mahakama ya Uingereza inayojishughulisha na masuala ya biashara na majengo kwa kudai kuwa walikuwa wamevunja makubaliano baina yao.

Kampuni hiyo inadai kulikuwepo makubuliano walipwe fidia ya Dola 45 milioni (Sh103 bilioni) mwaka 2014 lakini serikali ya Tanzania haikutelekeza makubaliano hayo.

Mattaka alifikishwa mahakamani Machi 2016 akituhumiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka kutokana na kufikia makubaliano hayo ya ukodishaji ndege bila ya kufuata taratibu za serikali za ununuzi na kesi bado iko mahakamani.

Mahakama ya Uingereza imekataa utetezi wa ATCL, ambapo wanamsukumia lawama Mattaka.

Jaji Butcher amedai kuwa ATCL inapaswa kutekeleza makubaliano ya mwaka 2013 na kulipa Dola 30.1 milioni kwa Wallis Trading.
 
Makosa ya serikali ni kutoiacha hii kampuni ikafa na kutangazwa mufilisi. Sasa hapa tutapambana na hizi makesi mpaka mwisho wa dunia. Hizi ndege wanazonunua sujui zitaruka wapi.

Wangeacha kampuni ya ATCL ife halafu waanzishe kampuni mpya na kuipa hizi za magumashi walizonunua. Poor leadership.
 
Hii serikali ya jiwe inachekesha kweli kweli. Kwamba Mattaka aliingia mkataba wa kifisadi kama yeye binafsi Mattaka au akiwa mtendaji wa ATCL kampuni ya serikali?

Wakatae basi kulipa madeni yaliyokopwa na serikali zilizopita kwa madai kuwa mikopo iliingiwa kifisadi na wangekuwa wao wasingeikubali.
 
Makosa ya serikali ni kutoiacha hii kampuni ikafa na kutangazwa mufilisi. Sasa hapa tutapambana na hizi makesi mpaka mwisho wa dunia. Hizi ndege wanazonunua sujui zitaruka wapi.

Wangeacha kampuni ya ATCL ife halafu waanzishe kampuni mpya na kuipa hizi za magumashi walizonunua. Poor leadership.

Kwani hiyo kampuni ya ATCL haikuwa na mzamini? Serikari haitakwepa jambo hili kinachotakiwa ni kumalizana nalo iwe kwa kulipa au kwa kushinda, Kampunibilikfilisika mdhamini lazima atalipa tu, ambayo ni serikali.
 
Serikali imesema imeanza mchakato wa kukata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Uingereza dhidi ya Shirika la Ndege la Tanzania(ATCL).

ATCL imeamriwa kulipa Dola 30.1 milioni (Sh69.23bilioni) kwa kampuni moja ya Liberia kama fidia baada ya kuvunjika kwa mkataba wa kukodisha ndege.

Kesi hiyo inahusu makubaliano yaliyofikiwa mwaka 2013 na aliyekuwa Mkurugenzi wa ATCL, David Mattaka ya kukodisha ndege aina ya Airbus kutoka kampuni ya Willis Trading.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Uingereza, Christopher Butcher aliiamuru ATCL kulipa fedha hizo pamoja na riba inayoweza kufikia dola 10 milioni (Sh23 bilioni) kwa kampuni hiyo ya Liberia, ambayo inajishughulisha na masuala ya kuuza na kukodisha ndege, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa.

Hata hivyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Adelardus Kilangi aliliambia Mwananchi kuwa mkataba wenyewe ulikuwa wa kifisadi wa kuitia nchi hasara.

Dk Kilangi alisema kuwa serikali imewasiliana na ofisi yake, ambayo imeanza mchakato wa kukata rufaa. “Tumeanza mchakato wa kukata rufaa na tunazingatia sheria na taratibu za Uingereza,” aliongeza.

Dk Kilangi alieleza kuwa hukumu hiyo imewashangaza kutokana na ukweli kuwa ndege yenyewe ilitumika kwa miezi saba tu. “Hawa watu wameibia nchi na tutapambana mahakamani kuhakikisha tunashinda kesi hii,” alisisitiza Kilangi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, Leonard Chamuriho na Ofisa Mkuu Mtendaji wa ATCL, Ladislaus Matindi wote hawakutaka kuzungumzia suala hilo walipotafutwa kwa njia ya simu.

Kampuni ya Willis Trading iliwasilisha madai yake kwenye Mahakama ya Uingereza inayojishughulisha na masuala ya biashara na majengo kwa kudai kuwa walikuwa wamevunja makubaliano baina yao.

Kampuni hiyo inadai kulikuwepo makubuliano walipwe fidia ya Dola 45 milioni (Sh103 bilioni) mwaka 2014 lakini serikali ya Tanzania haikutelekeza makubaliano hayo.

Mattaka alifikishwa mahakamani Machi 2016 akituhumiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka kutokana na kufikia makubaliano hayo ya ukodishaji ndege bila ya kufuata taratibu za serikali za ununuzi na kesi bado iko mahakamani.

Mahakama ya Uingereza imekataa utetezi wa ATCL, ambapo wanamsukumia lawama Mattaka.

Jaji Butcher amedai kuwa ATCL inapaswa kutekeleza makubaliano ya mwaka 2013 na kulipa Dola 30.1 milioni kwa Wallis Trading.
Safi sana, Tuone Kama kuna ndege yoyote ya ATCL itaenda nje ya Tanzania, lazima zikamatwe ili mlipe deni, Tanzania imejaa laana ya kudhulumu, mliwaharibia Fast Jet mkidhani mtafanikiwa, sasa kiko wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiachilia ya kuwa ulikuwa mkataba wa kifisadi which brings the question of legality (tosha kuufunya void) na chances are huyo bwana Mattaka lazima kuna malipo alipewa kukubali vinginevyo hakuna mtu timamu angeweza ingia mkataba wa ovyo vile kwa maelezo ya nakala ya Guardian on Sunday la UK (ambapo hiyo copy himo humu humu JF kwenye thread inayoongea uozo wa huu mkataba way back).

Ukipitia ile nakala kwa upande wa hao walebanese tu kuna vitu kibao tu utaona ilikuwa vya kuvunja mkataba to name a few; errors (consensus in idem) ya subject matter, quality na nature of contract kutokana kilichojiri baada ya ndege kuwasili.

Kuna fraudulent misrepresentation ya ubora wa ndege na kuna material breach ambapo ATCL ndio angekuwa mdai maana ndege yenyewe hata aikutumika

But for some reason Tanzania will find a way to lose even a simple case ambayo ata mwanafunzi wa mwaka wa kwanza kwenye masomo ya biashara na sheria anasoma partially anashinda.

Only in Tanzania
 
Makosa ya serikali ni kutoiacha hii kampuni ikafa na kutangazwa mufilisi. Sasa hapa tutapambana na hizi makesi mpaka mwisho wa dunia. Hizi ndege wanazonunua sujui zitaruka wapi.

Wangeacha kampuni ya ATCL ife halafu waanzishe kampuni mpya na kuipa hizi za magumashi walizonunua. Poor leadership.
Uelewa wako unaulakini, mind u kuna Goverment Guarantee
 
Serikali imesema imeanza mchakato wa kukata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Uingereza dhidi ya Shirika la Ndege la Tanzania(ATCL). ATCL imeamriwa kulipa Dola 30.1 milioni (Sh69.23bilioni) kwa kampuni moja ya Liberia kama fidia baada ya kuvunjika kwa mkataba wa kukodisha ndege.

Hata hivyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Adelardus Kilangi aliliambia Mwananchi kuwa mkataba wenyewe ulikuwa wa kifisadi wa kuitia nchi hasara.

Huu ndio upoyoyo na ukihiyo wa Watanzania wengi pamoja na huyu mwanasheria Mkuu wa Tanzania. Mambo ya ufisadi wenu wan ndani yanawahusu nini wao? Hilo ni tatizo lenu la ndani, kama watu wenu walisaini mkataba wa kifisadi bado mnakuwa na wajibu wa kisheria wa kutekeleza mkataba huo. Kusema hamtekelezi mkataba kwa sababu ulikuwa wa kifisadi ni upumbavu mkubwa vihiyo wa sheria pekee ndio wanaweza kutoa kama sababu za kuvunja mkataba.

Kama wawakilishi wenu katika ku-sign mkataba walikubali rushwa na kuingia mkataba wenye kuitia hasara Tanzania hilo haliwahusu wakodisha ndege. Kama mna ushahidi kwa kuwa kuna nchi zina sheria kali dhidi ya kampuni za kimataifa zinazoingia mikataba kwa kutumia ufisadi. Sio mnapayuka tu kama kasuku mkitegemea kila mtu nje ya nchi anazielewa kelele zenu za uzalendo.
 
Hii serikali ya jiwe inachekesha kweli kweli. Kwamba Mattaka aliingia mkataba wa kifisadi kama yeye binafsi Mattaka au akiwa mtendaji wa ATCL kampuni ya serikali?

Wakatae basi kulipa madeni yaliyokopwa na serikali zilizopita kwa madai kuwa mikopo iliingiwa kifisadi na wangekuwa wao wasingeikubali.
Mbona na yeye ameisababishia nchi hasara kubwa kwenye kuvunja mikataba ya ujenzi wa barabara na kupora samaki waliovuliwa kwenye international water?
 
Back
Top Bottom