Serikali kuingia mikataba kabla ya Due Diligence

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,874
Nimeangalia video ya Mh. Rais @samia_suluhu_hassan akizungumza kuhusu serikali kuingia mkataba na kampuni ya Kituruki (Yutek Gemi San Ltd ) ya ujenzi wa meli 5 ,takribani Tsh. Bil.400 .


Rais Samia anasema mkataba huo uliingiwa tar 15 Juni 2021 huko Mwanza kati ya Serikali kupitia kampuni ya huduma za Meli Tanzania (MSCL) na kampuni hiyo ya Kituruki itwayo YUTEK GEMI SAN LTD.

Katika kufuatilia utekelezaji wa ujenzi wa meli hizo baada ya kuunda timu ya ufuatiliaji ,Rais Samia anasema mambo kadhaa waliyabaini yenye kutia wasiwasi.

1.Timu iligundua Mkandarasi huyo wa kampuni ya Yutek haina eneo lake la ujenzi wa meli yaani Ship-yard isipokuwa ni madalali tuu.

2.Timu iligundua uwezo wa kifedha wa kampuni hiyo ya Yutek ni mdogo mno na Timu hadi inaondoka haijapewa taarifa zozote za kifedha.Na hadi kampuni hiyo haijafanya chochote kuhusu ujenzi.

Ukimuangalia Mh. Rais Samia anavyoongea , sura yake ,matamshi yake huonesha kwamba ana mzigo mzito sana ameubeba.

Lakini mimi najiuliza wataalamu wanaolipwa na kodi zetu , kumsaidia Rais wanamsaidia namna gani ?

Alichoongea Rais Samia , kuhusu nchi kuingia mkataba na huyo Mkandarasi wa Uturuki, unapata kujua bado Rais anajukumu la kutengeneza mifumo imara na kuwa na watu imara wa kumsaidia kazi.

Inafahamika wazi kabla ya kuingia mkataba wowote uwe mkataba binafsi au mkataba wa nchi ,uwe mkataba mdogo au mkubwa na kampuni katika masuala ya kibiashara kuna kitu kinaitwa "Due Diligence" ikiwa na maana ya kupitia na kukagua ( Complete review and Audit) hali ya kampuni unayoingia nayo makubaliano au mkataba huo kabla ya kuingia mkataba wenyewe ili kujua uwezo wa kifedha wa kampuni hiyo (Financial Due Diligence),uhalali wa kampuni hiyo kisheria (Legal due Diligence),uwezo wake katika kufanya kazi (Operational Due Diligence) na mambo mengine, hii ni hatua ya awali kabisa kabla ya kuingia mkataba.

Kwa kauli ya Rais Samia inaonekana Due Diligence haikufanyika kabla ya kuingia mkataba huo,kama wangefanya Due Diligence awali wangebaini changamoto hizo mwanzo kabisa,wangefahamu mapema kama kampuni hiyo haina eneo lake la ujenzi kupitia kufanya Operational Due Diligence, wangefahamu uwezo mdogo wa kifedha wa hiyo kampuni mapema mno kupitia kufanya Financial Due Diligence.

Makosa haya yamekuwa yakijitokeza mara nyingi sana nchini kwetu ,itakumbukwa tar 30 , Januari 2019.Serikali iliingia mkataba huko Arusha na kampuni ya Indo Power Solutions Ltd ya nchini kenya chini ya Mkurugenzi wake Brian Mutembei ili kununua korosho tani laki moja zenye thamani ya Tsh.Bil.418 .Ila mwezi wa 5 ,2019 serikali ikavunja mkataba na kampuni hiyo baada ya kugundulika kampuni hiyo ni ya kijanja kijanja na ni madalali .

Changamoto hizi zenye maslahi ya nchi kiuchumi zinahitaji dawa.

Sitaki kulaumu sana bali nijikite katika ushauri kwa Mh. Rais na serikali ili haya mambo yasitokee tena .Ana nafasi ya kubalisha haya.

1.Tufanye marekebisho ya sheria yetu ya usalama wa taifa tuweke kitengo kitakachojikita na masuala ya ujasusi wa kiuchumi (Economic Intelligence),ndio itakuwa na kazi ya kukusanya taarifa za kiuchumi na makubaliano ya kibiashara kwa maslahi ya nchi kuliko Rais kuanza kuunda Tume ya kuchunguza na kufuatilia baada ya mambo kuharibika.

Marekani walifanya hivyo 1949 walirekebisha sheria yao ya ujasusi ya 1947 na kuweka kitengo cha "Office of economic Research Report".Bado hatujachelewa Mh. Rais , unaweza fanya hivyo .

Nchi nyingi sana sasa hivi zina vitengo hivyo ,nchi nyingi sasa duniani zimeingia katika ushindani na kulinda maslahi yao kiuchumi na kibiashara kwa maslahi ya nchi zao na mataifa yao ,hata sisi Tanzania bado hatujachelewa kufanya hivyo.Katika Thesis ya Valentyn Levytaskyi itwayo "Economic Intelligence of the Modern State ya 2001 " ameelezea vizuri sana kuhusu umuhimu wa nchi kuwa na kitengo cha ujasusi wa kiuchumi.

2.Mikataba yetu iwe wazi , kama ambavyo sheria ya Access information Act 2016, kifungu cha 5 ,na Access information Regulation 2017 kanuni ya 5 inavyoelezea kuhusu mikataba kuwekwa wazi kwa umma.Jambo hili halifanyiki nchini.

3.Itungwe sheria ya Bunge inayoipa Mamlaka Bunge ya kupitia na kupitisha mikataba yote yenye maslahi na nchi yenye kuanzia kiasi fulani cha fedha labda mikataba kuanzia bil. 10 lazima iende Bungeni kupitiwa na kupitishwa.

Ukisoma katiba yetu ya 1977 ibara ya 63(3)E , kuhusu wajibu wabunge katika kujadili na kuridhia makubaliano na mikataba , ibara hii haijajitosheleza kwani ina tafsiriwa tofauti kwamba ni mikataba inayoingia kati ya nchi yetu na nchi nyingine au jumuiya za kimataifa (Bilateral Agreement and Multilateral Agreement) na haitafsiriwi kama pia ni mikataba hii inayoingiwa kati ya taasisi ya Serikali au idara ya Serikali na taasisi nyingi au kampuni au nchi. Hivyo jukumu la kuwa na katiba yenye kutoa tafsiri nzuri katika ibara hii haliepukiki.

Nchini Tanzania ni mikataba ya rasilimali za nchi tuu kama madini na gesi ndio huweza jadiliwa na kupitishwa na Bunge kupitia sheria ya Natural wealth and resource (Permanent Sovereignty) Act ya 2017 na Natural wealth and resource (Review and re-negotiation of unconscionable terms act ya 2017 ).Bado pia sheria hizi zina mapungufu kadhaa .

Hivyo tunapaswa kuwa na sheria itakayoipa mamlaka Bunge , kupitia na kuidhinisha mikataba yote kabla ya Serikali kuingia mikataba hiyo .

4. Tuwe na mifumo imara itakayosaidia nchi kuwa na viongozi imara , pamoja na Bunge imara litakalo kuwa na uwezo wa kujadili ,kukosoa na kuishauri serikali .Na sio kuwa na Bunge la chama kimoja ambalo halina uwezo wa kukosoa na kuishauri serikali. Yote haya yanaweza fanyika kikamilifu kwa kuwa na mifumo imara kupitia mabadiliko ya katiba .

Hivyo katiba mpya ,ni jambo la msingi sana ili kutatua changamoto hizi.

Ahsante.

Abdul Nondo.

Mwenyekiti wa Ngome ya vijana ACT wazalendo Taifa.

05/12/2021.
Kigoma.
 
Hivi vitu abduli vinaeleweka na vinatumika Kama muongozo kwenye utendaji. Shida inakuja kwamba ushakuwa pale na unajua Kuna siku utastaafu tu na unahitaji fedha za pensheni nyingi tu uzeeni "utajiri" usio kifani. Hapa unakuta mate yanakuteremka taratiiiiiiiibu huku ukiona bright future. Aaah wapi 😅 yasikie tu
 
Hii nchi kila mtu anangojea apate tu chance yake ifike na yeye apige zake pesa aondoke, bado uzarendo ni sifuri kabisa kwenye nchi hii.. Pamoja na kuwa na wanasheria na wanauchumi bora kabisa ila inapofika kwenye 10% kila mtu anaweka masilahi yake binafs zaidi taaruma haitumiki tena.

Swali sasa nani amfunge paka kengere?
 
Hivi vitu abduli vinaeleweka na vinatumika Kama muongozo kwenye utendaji. Shida inakuja kwamba ushakuwa pale na unajua Kuna siku utastaafu tu na unahitaji fedha za pensheni nyingi tu uzeeni "utajiri" usio kifani. Hapa unakuta mate yanakuteremka taratiiiiiiiibu huku ukiona bright future. Aaah wapi 😅 yasikie tu
Ni ujinga tu ndo inaendekezwa.
 
Tatizo ninaloona ni wanasiasa kutaka kuwa watendaji. Na wanasiasa kutaka kutoa matamko kwenye majukwaa, press conferences na kwenye twitter. Badala ya watendaji kuwa washauri wa wanasiasa, wamegeuzwa kuwa wasaidizi na watu wakuhalalisha anachokitaka mwanasiasa. Mtendaji Mkuu wa Wizara ni Katibu Mkuu na wa Mkoa ni Katibu Tawala wa Mkoa. Hawa hawasikiki, wanaosikika ni mawaziri na ma rc. Waziri anaenda nchi za nje na akirudi anatoa tamko kuhusu makubaliano aliyofanya na nchi kadhaa! Hizo due diligence zitafanyika wapi na nani wakati tayari mkono wa saa umeishaanza kutembea kwa kasi?

Amandla...
 
Hii nchi kila mtu anangojea apate tu chance yake ifike na yeye apige zake pesa aondoke, bado uzarendo ni sifuri kabisa kwenye nchi hii.. Pamoja na kuwa na wanasheria na wanauchumi bora kabisa ila inapofika kwenye 10% kila mtu anaweka masilahi yake binafs zaidi taaruma haitumiki tena.

Swali sasa nani amfunge paka kengere?
Wa kumfunga paka kengele ni Raisi pekee,taasisi ya Uraisi(presidency).
Majizi chinja,funga,filisi ndio dawa,
Ua kimya kimya,watu watakaa Sawa.
 
😁😁😁
1638006971_1638006971-picsay.jpg
 
Abdul Nondo,

Bandiko zuri la ushauri umetoa. Serikali iwasikilize wananchi maoni yao huwa kuna uwezekano vitengo hivyo vya kijasusi, mabalozi wetu na idara za serikali zikafaidika badala ya kuponda mtandao kama wa JF ambao pia umesheheni data, takwimu, source, links n.k kibao kuisaidia serikali kufanya maamuzi mazuri zaidi au pia serikali ikajisahihisha vizuri zaidi pale inapokosea.



Toka mkataba :


15 Juni 2021
Mwanza, Tanzania

Rais Samia anashuhudia utiaji saini mikataba 5 ya ujenzi na ukarabati wa meli Shilingi Bilioni 417.

Rais Samia Suluhu Hassan ashuhudia utiaji saini mikataba 4 ya ujenzi wa meli mpya na mmoja wa ukarabati wa meli . Mheshimiwa Rais amefarijika kuona kazi inaendelea ya kuifanya Mwanza na ukanda wa ziwa Victoria kuwa kitovu cha uchumi kwa maeneo ya Afrika Mashariki na pia nchi za Maziwa Mkuu za Burundi, Rwanda pamoja na Mashariki ya DR Congo.
  1. Meli ya mizigo uwezo tani 3000 ya kubeba mabehewa (wagon ferry) kukatiza ziwa Victoria
  2. Meli ya abiria uwezo watu 600 na tani 400 ziwa Tanganyika
  3. Meli ya mizigo uwezo tani 2800 ziwa Tanganyika
  4. Meli uwezo tani 2800 ya mizigo katika bahari ya Hindi
  5. Wakati meli ya MV Umoja iliyopo ktk ziwa Victoria ukarabati wake utafanywa na Kampuni toka South Korea.
Shughuli hiyo ilifanyika Leo Mwanza Tanzania ambapo wizara ya Ujenzi kwa niaba ya MSCL Kampuni ya Huduma za Meli Tanzania na Yücel Tekin Shipbuilding Company YÜTEK kampuni toka Uturuki zilisaini mkataba wa thamani ya dola za kimarekani US$180 million sawa na shilingi 417,240,000,000.

Katika hafla hiyo balozi wa Turkey nchini Tanzania, Mhe. Dr. Mehmet Güllüoğlu alikuwa miongoni mwa wageni wengi waliohudhuria shughuli ya utiaji mkataba baina ya mkandarasi wa ujenzi wa meli toka kampuni ya YÜTEK ya Uturuki na wizara ya Ujenzi ya Tanzania.

=========

News in English:
15 June 2021
Mwanza, Tanzania


YÜTEK signed 4 new shipbuilding contracts with the Ministry of Transport of Tanzania​

Yücel Tekin Shipbuilding Company (YÜTEK) signed a new shipbuilding contract to build 2 general cargo, 1 passenger and 1 wagon ferry ship to be built for the Ministry of Transport of Tanzania. It was learned that the cost of the project was 180 million dollars.​

The Turkish shipbuilding industry signed 4 new shipbuilding contracts to the Tanzania Ministry of Transport within the framework of its African expansion.

YÜTEK Shipbuilding Industry Company signed a new shipbuilding contract to Tanzania Ministry of Transport to build 2 general cargo, 1 passenger and 1 wagon ferry ship. It was learned that the cost of the project was 180 million dollars.

Tanzania’s first female President Samia Suluhu Hassan participated in the new shipbuilding contract to be built under the auspices of the Tanzania Ministry of Transport. Mehmet Güllüoğlu and many guests attended.

It was stated that the design of the newly built ships will be carried out by Artı Mühendislik and 3 of the ships to be built by YÜTEK will be built in Tanzania and one general cargo ship will be built in Turkey.

It was stated that 4 new construction ships to be built for the Ministry of Transport of Tanzania will cost 180 million dollars, while it was stated that the ships to be built in Tanzania will serve in Lake Tanganyika and Lake Victoria.

FEATURES OF NEW BUILT SHIPS
Project.1:
3500dwt 100x17m Multi purpose Cargo vessel, operation area Lake Tanganyika. It will carry General Cargo in Cargo holds, Refrigerated and Normal 20″ Containers on deck, 2 25Tx17m Crane-mounted vehicles on the aft deck.

Project.2: 3500dwt 80x17m Multi purpose Cargo vessel, operation site East African Coast/Indian Ocean. General Cargo in Cargo warehouses, Refrigerated and Normal 20″ Container on the deck, 1 pcs. 25Tx17m Crane mounted, will carry vehicles on the aft deck. There will be an animal deck on the vehicle deck that will carry 65 cattle.

Project.3: 600 Passengers + 30 crew + 20 Vehicles + 80x17m Passenger Cargo ship with 400ton load capacity. Operation zone Lake Tanganyika.

Project.4: 124x17m Wagon Ferry with a capacity of 26 wagons. Operation area Lake Victoria

Source: YÜTEK signed 4 new shipbuilding contracts with the Ministry of Transport of Tanzania - News2Sea

=========

Habari za ziada:

Soma jinsi mabalozi wanategemewa kuwezesha fursa kwa kutumia diplomasia ya kiuchumi
: Kuletewa Balozi mtaalamu wa Ulinzi wa Masuala ya Mitandao ni 'Diplomatic Gesture' ?
 
Nimeangalia video ya Mh. Rais @samia_suluhu_hassan akizungumza kuhusu serikali kuingia mkataba na kampuni ya Kituruki (Yutek Gemi San Ltd ) ya ujenzi wa meli 5 ,takribani Tsh. Bil.400 .


Rais Samia anasema mkataba huo uliingiwa tar 15 Juni 2021 huko Mwanza kati ya Serikali kupitia kampuni ya huduma za Meli Tanzania (MSCL) na kampuni hiyo ya Kituruki itwayo YUTEK GEMI SAN LTD.

Katika kufuatilia utekelezaji wa ujenzi wa meli hizo baada ya kuunda timu ya ufuatiliaji ,Rais Samia anasema mambo kadhaa waliyabaini yenye kutia wasiwasi.

1.Timu iligundua Mkandarasi huyo wa kampuni ya Yutek haina eneo lake la ujenzi wa meli yaani Ship-yard isipokuwa ni madalali tuu.

2.Timu iligundua uwezo wa kifedha wa kampuni hiyo ya Yutek ni mdogo mno na Timu hadi inaondoka haijapewa taarifa zozote za kifedha.Na hadi kampuni hiyo haijafanya chochote kuhusu ujenzi.

Ukimuangalia Mh. Rais Samia anavyoongea , sura yake ,matamshi yake huonesha kwamba ana mzigo mzito sana ameubeba.

Lakini mimi najiuliza wataalamu wanaolipwa na kodi zetu , kumsaidia Rais wanamsaidia namna gani ?

Alichoongea Rais Samia , kuhusu nchi kuingia mkataba na huyo Mkandarasi wa Uturuki, unapata kujua bado Rais anajukumu la kutengeneza mifumo imara na kuwa na watu imara wa kumsaidia kazi.

Inafahamika wazi kabla ya kuingia mkataba wowote uwe mkataba binafsi au mkataba wa nchi ,uwe mkataba mdogo au mkubwa na kampuni katika masuala ya kibiashara kuna kitu kinaitwa "Due Diligence" ikiwa na maana ya kupitia na kukagua ( Complete review and Audit) hali ya kampuni unayoingia nayo makubaliano au mkataba huo kabla ya kuingia mkataba wenyewe ili kujua uwezo wa kifedha wa kampuni hiyo (Financial Due Diligence),uhalali wa kampuni hiyo kisheria (Legal due Diligence),uwezo wake katika kufanya kazi (Operational Due Diligence) na mambo mengine, hii ni hatua ya awali kabisa kabla ya kuingia mkataba.

Kwa kauli ya Rais Samia inaonekana Due Diligence haikufanyika kabla ya kuingia mkataba huo,kama wangefanya Due Diligence awali wangebaini changamoto hizo mwanzo kabisa,wangefahamu mapema kama kampuni hiyo haina eneo lake la ujenzi kupitia kufanya Operational Due Diligence, wangefahamu uwezo mdogo wa kifedha wa hiyo kampuni mapema mno kupitia kufanya Financial Due Diligence.

Makosa haya yamekuwa yakijitokeza mara nyingi sana nchini kwetu ,itakumbukwa tar 30 , Januari 2019.Serikali iliingia mkataba huko Arusha na kampuni ya Indo Power Solutions Ltd ya nchini kenya chini ya Mkurugenzi wake Brian Mutembei ili kununua korosho tani laki moja zenye thamani ya Tsh.Bil.418 .Ila mwezi wa 5 ,2019 serikali ikavunja mkataba na kampuni hiyo baada ya kugundulika kampuni hiyo ni ya kijanja kijanja na ni madalali .

Changamoto hizi zenye maslahi ya nchi kiuchumi zinahitaji dawa.

Sitaki kulaumu sana bali nijikite katika ushauri kwa Mh. Rais na serikali ili haya mambo yasitokee tena .Ana nafasi ya kubalisha haya.

1.Tufanye marekebisho ya sheria yetu ya usalama wa taifa tuweke kitengo kitakachojikita na masuala ya ujasusi wa kiuchumi (Economic Intelligence),ndio itakuwa na kazi ya kukusanya taarifa za kiuchumi na makubaliano ya kibiashara kwa maslahi ya nchi kuliko Rais kuanza kuunda Tume ya kuchunguza na kufuatilia baada ya mambo kuharibika.

Marekani walifanya hivyo 1949 walirekebisha sheria yao ya ujasusi ya 1947 na kuweka kitengo cha "Office of economic Research Report".Bado hatujachelewa Mh. Rais , unaweza fanya hivyo .

Nchi nyingi sana sasa hivi zina vitengo hivyo ,nchi nyingi sasa duniani zimeingia katika ushindani na kulinda maslahi yao kiuchumi na kibiashara kwa maslahi ya nchi zao na mataifa yao ,hata sisi Tanzania bado hatujachelewa kufanya hivyo.Katika Thesis ya Valentyn Levytaskyi itwayo "Economic Intelligence of the Modern State ya 2001 " ameelezea vizuri sana kuhusu umuhimu wa nchi kuwa na kitengo cha ujasusi wa kiuchumi.

2.Mikataba yetu iwe wazi , kama ambavyo sheria ya Access information Act 2016, kifungu cha 5 ,na Access information Regulation 2017 kanuni ya 5 inavyoelezea kuhusu mikataba kuwekwa wazi kwa umma.Jambo hili halifanyiki nchini.

3.Itungwe sheria ya Bunge inayoipa Mamlaka Bunge ya kupitia na kupitisha mikataba yote yenye maslahi na nchi yenye kuanzia kiasi fulani cha fedha labda mikataba kuanzia bil. 10 lazima iende Bungeni kupitiwa na kupitishwa.

Ukisoma katiba yetu ya 1977 ibara ya 63(3)E , kuhusu wajibu wabunge katika kujadili na kuridhia makubaliano na mikataba , ibara hii haijajitosheleza kwani ina tafsiriwa tofauti kwamba ni mikataba inayoingia kati ya nchi yetu na nchi nyingine au jumuiya za kimataifa (Bilateral Agreement and Multilateral Agreement) na haitafsiriwi kama pia ni mikataba hii inayoingiwa kati ya taasisi ya Serikali au idara ya Serikali na taasisi nyingi au kampuni au nchi. Hivyo jukumu la kuwa na katiba yenye kutoa tafsiri nzuri katika ibara hii haliepukiki.

Nchini Tanzania ni mikataba ya rasilimali za nchi tuu kama madini na gesi ndio huweza jadiliwa na kupitishwa na Bunge kupitia sheria ya Natural wealth and resource (Permanent Sovereignty) Act ya 2017 na Natural wealth and resource (Review and re-negotiation of unconscionable terms act ya 2017 ).Bado pia sheria hizi zina mapungufu kadhaa .

Hivyo tunapaswa kuwa na sheria itakayoipa mamlaka Bunge , kupitia na kuidhinisha mikataba yote kabla ya Serikali kuingia mikataba hiyo .

4. Tuwe na mifumo imara itakayosaidia nchi kuwa na viongozi imara , pamoja na Bunge imara litakalo kuwa na uwezo wa kujadili ,kukosoa na kuishauri serikali .Na sio kuwa na Bunge la chama kimoja ambalo halina uwezo wa kukosoa na kuishauri serikali. Yote haya yanaweza fanyika kikamilifu kwa kuwa na mifumo imara kupitia mabadiliko ya katiba .

Hivyo katiba mpya ,ni jambo la msingi sana ili kutatua changamoto hizi.

Ahsante.

Abdul Nondo.

Mwenyekiti wa Ngome ya vijana ACT wazalendo Taifa.

05/12/2021.
Kigoma.
Mkuu Abdul Nondo , asante sana kwa nondo hii, huu ndio uzalendo wenyewe wa kweli wa mtu kwa nchi yako. Ulipaswa kusomea sheria, unajadili vizuri hoja za kisheria kuliko wanasheria wenyewe, kiukweli kabisa kwa wenzetu, due diligence report ndio hatua ya kwanza, tungefanya due diligence report kusingetokea EPA, Richmond, Escrow, Tangold, Meremeta etc.

You are still young, hili la sheria, hujachelewa
Big up sana
P
 
Hivi vitu abduli vinaeleweka na vinatumika Kama muongozo kwenye utendaji. Shida inakuja kwamba ushakuwa pale na unajua Kuna siku utastaafu tu na unahitaji fedha za pensheni nyingi tu uzeeni "utajiri" usio kifani. Hapa unakuta mate yanakuteremka taratiiiiiiiibu huku ukiona bright future. Aaah wapi 😅 yasikie tu
🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Unamaanisha vijana wa Hangaya mate yaliteremka?
 
Back
Top Bottom