Serikali "Kufidia" makampuni 50 yaliyoathirika na "Mtikisiko wa Uchumi Duniani"!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Najiuliza hivi ni makampuni gani hayo 50 ambayo yamepata hasara na kutaabikia kutokana na kuvurugika kwa Uchumi wa Dunia pale nchini kwetu Tanzania?

Ni shughuli gani za uzalishaji mali ambazo makampuni haya yanazifanya?

Je, ni wazalishaji wa ndani ya nchi wanaotumia mali ghafi na rasilimali kutengeneza bidhaa na kuziuza nje ya nchi na hivyo mapato yao yamekwenda fyongo na kuwa hasara tubu na bidhaa zao kudoda?

Je, makampuni haya yanaweza kutuonyesha vitabu vyao vya mahesabu vya takriban miaka mitano kabla ya May 2008, na mahesabu yao tangu May 2008 mpaka leo hii?

Je, Makampuni haya yanaweza kutuonyesha ni wapi masoko yao yalilipo na kutupatia takwimu za kiuchumi za nchi ambazo walikuwa wakipeleka bidhaa ili kudhihirisha kuvurugika kwa uchumi na hivyo kukosa soko la bidhaa zao?

Je, makampuni haya yanaweza kutuambia ni njia gani walizotumia hata pamoja na kutafuta masoko mapya ndani na nje ya nchi kuhakikisha kuwa bidhaa hizi zilizozalishwa na Wananchi wetu zinapata soko?

Je, ni lazima tuwape fedha kama fidia? kwa nini tusiwape mkopo wa kuongeza mtaji au kuwafutia kodi na ushuru japo kwa miezi 6?

Kama umeshafika hapa kunisoma, jiulize mbona Mchungaji haongelei makampuni yanayoagiza bidhaa kutoka nje?

Jibu lake ni kuwa wao wanaoagiza, hayajaingia hasara yeyote!

Kwanza wamepata faida marudufu kutokana na kununua bidhaa zao huko ughaibuni kwa bei rahisi na ya nichekee, hivyo itakuwa ni uopngo wakisema kuwa wamepata hasara!

Makampuni yanayoagiza bidhaa, wamepata faida kubwa kwa kununua bidhaa kwa bei ya chini , na bado wameendelea kuwalangua Watanzania kwa kisingizio uchumi wa dunia mbaya!

Hawa hawastahili msamaha wa kodi, kupewa mkopo au kupewa fidia.

Naomba uwasiliane na mwakilishi wako na pigia kelele jambo hili mpaka kieleweke.

Ikiwa kutakuwa na Kampuni inayopagiza bidhaa kutoka nje itadai imeingia hasara, naomba kampuni hiyo itupe orodha ya bidhaa inazoagiza, pamoja na nchi wanakonunua bidhaa hizi. Ama watupe thamani na bei ya bidhaa wanazoagiza tangu January 2006 mpaka leo hii ili tutoe tathmini ya kweli. Zaidi, watupe orodha inayoonyesha bei zao zikishafika nchini, pamoja na kumbukumbu za malipo yao ya ushuru na kodi kwa Serikali na stetimenti ya Benki zao kwa akaunti zao zote kwa miaka mitatu iliyopita.

Tukiweza kuyaona haya yote, ndipo tuanze mchakato wa kubaini ni nani apewe msaada wa kujihimu kutokana na kuanguka kwa uchumi wa Dunia.

La mwisho na ushauri wangu, ni hivi, Benki Kuu isichape noti mpya au kugawa pesa kama peremende, bali itoe mkopo wa riba ndogo au bila riba kabisa kwa makampuni yote ambayo yatathibitika yamepita vipimo vya mchungaji. Pili labda kuwepo na msamaha wa kodi na ushuru kwa makampuni yale yanayopeleka bidhaa nje (export) kati ya miezi 6 hadi mwaka mmoja.

Maoni yangu nayatoa kutokana na habari hii ninayoambatanisha hapa chini!

Makampuni 50 yaliyoathirika na mtikisiko wa uchumi kulipwa fidia

Na Salim Said

SERIKALI imeiagiza Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kufanya mchanganuo wa kampuni 50 ambazo zitapata uhalali wa kuingia katika orodha ya zile zitakazofidiwa na serikali baada ya kupata hasara kubwa kutokana na athari za mtikisiko wa uchumi ulioikumba dunia kuanzia mwaka jana.

Serikali ilitenga Sh 21.9 bilioni kwa ajili ya kuwanusuru kampuni zilizopata hasara kutokana na kuanguka kwa bei ya mazao katika soko la dunia.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Khijja aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kwamba, tayari BoT imeanza mchakato wa kuratibu kampuni hizo.

“Tayari BoT inafanya mchanganuo wa kuzitambua kampuni 50 ambazo ziliathirika zaidi na mtikisiko huu kwa kula hasara kutokana na kununua mazao kwa bei kubwa na kuyauza kwa bei ndogo, baada ya bei kushuka katika soko la dunia,” alisema Khijja mara baada ya kufungua Mkutano wa Mwaka wa Shirikisho la Wenyeviwanda Tanzania (CTI).

“Baada ya mchanganuo wa BoT tutaweza kujua ni kampuni gani inastahiki kupata fedha hizo na ipi haistahiki ili tusije kuingia katika hasara kwa kutoa fedha kwa kampuni ambazo hazikustahiki,” alisema Khijja.

Khijja alibainisha kuwa, kuna baadhi ya kampuni ambazo zilipata hasara miaka mingi iliyopita, lakini tayari kuna nyingine ambazo zimejitokeza na kueleza kwamba nazo zimetikiswa kiuchumi.

Aidha alisema, serikali imeahidi kuzichukulia dhamana baadhi ya kampuni ili kuweza kupata mikopo katika benki mbalimbali nchini, lakini itafanya hivyo kwa zile kampuni ambazo hazina historia nzuri katika sura ya kibenki.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Shirikisho la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (Sido) Mike Laiser alilalamikia mabenki nchini kwa kutoza riba kubwa kwa wakopaji na kuweka riba ndogo kwa mtu anapoweka fedha benki.

“Ukikopa unapigwa riba kati ya asilimia 18 hadi 25 lakini wewe ukiweka fedha benki riba yake ni asilimia mbili hadi nne, hili bado ni tatizo kubwa katika maendeleo ya SMEs,” alisema Laiser.
 
Hapana; huu ni wizi wa waziwazi kabisa. Wanasiasa wanataka kuiba hela za walipa kodi. Inaelekea hii ni njia ya kutenga fedha za kutumika katika kampeini za uchaguzi mkuu mwakani kwa vile Kagoda haitatumika tena.

Tanzania hatuna kampuni hata moja iliyobeba uchumi wa nchi kiasi cha nchi kuogopa kampuni hiyo isipate hasara. Asilimia kubwa ya raia wetu wanategemea ardhi na serikali, na serikali yetu inategemea misaada ya kutoka nchi za nje.

Kampuni itakayopewa pesa hizo lazima iwe na mkono wa wanasiasa ndani ya chama tawala.

Halafu huyu Laizer naye amekaa pale SIDO takribani miaka 20 bado hajui biashara ya benki? Huweki pesa zako benki kupata faida, ukitaka pesa ikupe faida, basi lazima uifanyie biashara. Benki ni sehemu ya kutunzia pesa ili kujiepusha na majambazi tu.
 
Hapana; huu ni wizi wa waziwazi kabisa. Wanasiasa wanataka kuiba hela za walipa kodi. Inaelekea hii ni njia ya kutenga fedha za kutumika katika kampeini za uchaguzi mkuu mwakani kwa vile Kagoda haitatumika tena.

Tanzania hatuna kampuni hata moja iliyobeba uchumi wa nchi kiasi cha nchi kuogopa kampuni hiyo isipate hasara. Asilimia kubwa ya raia wetu wanategemea ardhi na serikali, na serikali yetu inategemea misaada ya kutoka nchi za nje.

Kampuni itakayopewa pesa hizo lazima iwe na mkono wa wanasiasa ndani ya chama tawala.

Halafu huyu Laizer naye amekaa pale SIDO takribani miaka 20 bado hajui biashara ya benki? Huweki pesa zako benki kupata faida, ukitaka pesa ikupe faida, basi lazima uifanyie biashara. Benki ni sehemu ya kutunzia pesa ili kujiepusha na majambazi tu.

Mwalimu Kichuguu,

Ikiwa TBL wametangaza faida marudufu na kuwakatia Wanahisa Mshiko mkubwa, inakuwaje kuwaje kuna vilio 50?

Tuwaulize TBL walifanyaje? Je wao ni Exxon Mobile au Goldman Sachs wa Tanzania?
 
Sasa wakichagua hizo kampuni je parliament ndiyo itapitisha au ndiyo muungwana pekee anaamuru kwamba walipwe? Kumbe kama ni hivyo basi kweli pesa za nchi zinaliwa bila hata daftari. Now I start to believe why this country will remain poor on the books.

Sasa hao viongozi wa upinzani, viongozi wa dini, na free media mko wapi? Hii ni dhuluma ya wazi kabisa. Miaka yote wameshindwa kuipa stimulus TANESCO, Dawasa, medicare, na agriculture wanaenda kuchagua makampuni 50 mwaka 2009. Hivi credit crunch kwa Tanzania imeanza lini? Mie nilifikiri credit crunch kwa Tanzania ipo tu tangu time immemorial!!
 
Sasa wakichagua hizo kampuni je parliament ndiyo itapitisha au ndiyo muungwana pekee anaamuru kwamba walipwe? Kumbe kama ni hivyo basi kweli pesa za nchi zinaliwa bila hata daftari. Now I start to believe why this country will remain poor on the books.

Sasa hao viongozi wa upinzani, viongozi wa dini, na free media mko wapi? Hii ni dhuluma ya wazi kabisa. Miaka yote wameshindwa kuipa stimulus TANESCO, Dawasa, medicare, na agriculture wanaenda kuchagua makampuni 50 mwaka 2009. Hivi credit crunch kwa Tanzania imeanza lini? Mie nilifikiri credit crunch kwa Tanzania ipo tu tangu time immemorial!!

Dear Interested Observer!

I agree with you hapa Tanzania SIYAONI hayo makampuni hamsini labda as you said serikali iyape stimulus mashirika yake ya umma kama Dawasco,Tanesco, ambayo yanaadhirika vibaya na kupanda kwa bei ya mafuta ili hali Ewura inawazuia kupandisha bei ya haduma wanayotoa kwani hawa jamaa hawafanyi biashara in the real sense. Kama Tanesco wananua umeme kutoka Songas kwa Tshs, 150/=( Ukiongezea na Capacity charge ni karibu Tshs.300/= kwa unit {KWhr) moja) na kuizia Zanzibar kwa Tshs. 50/= na bei ya wastani ya Tshs 120/= kwa wateja wengine hapo hakuna biashara bali ni usanii

Kama JMK aka matonya angetumia ABC ya uchumi aliyosoma pale mlimani zaidi ya miaka 30 iliyopita angeamua kutumia hiyo stimulus katika kustabilize bei ya mafuta pamoja na STABEX kwenye kilimo pamoja na pembejeo ahamasishe kilimo. Mabenki hayana historia ya kuimarisha uchumi!! Hayo makampuni ni ya wabunge na wanamtandao waliompeleka madarakani anataka tu kuwalipa fadhila. BENKI kuu iko Mochwari kama wamekubali kumteua fisadi Peter Noni wa RA akaongoze TIB unatarajia muujiza gani!! Look at those fools hata DECI hawakuigundua for 3 soild years Hamshangai tu kwamba the stupid Minister of Finance alifungua tawi la DECI kule kwao na bado JMK anazidi kumkumbatia asimpige paranja kwa sababu tu ya Udini!! hayo makampuni ambayo hayapeleki BOT audited accounts watayapata wapi?? Si bora mkawapa hata wanafunzi vitabu na walimu mishahara tujue moja??

The president and the govt he is leading is not serious na narudia lini Mkwere akawa serious apart from dancing. Kama kuna kampuni iliyoadhirika kikweli kweli si tungeona imefanya massive layouts na hilo bado halijatokea!!!
 
Hapa ni wizi mtupu hakuna cha kampuni wala nini. wanasiasa wanafikiri watanzania hatina akili kabisa. Hii ni aibu kubwa kwa nchi yetu,
WIZI MTUPU!
 
Hivi vichekesho sasa. Kwani kupata hasara si sehemu ya biashara au bishara ni faida kila siku? Pesa za walipa kodi zitatumikaje kusaidia kampuni binafsi??
Na hii lugha "kufidia" maana yake hizi pesa ndo wanagawa? At least marekani ni mkopo.
 
Pengine tushinikize mashirika na vigezo vya stimulus package kutangazwa hadharani (public scrutiny) kwanza kabla ya kulipwa!
 
Kama serikali imeweza kutenga kiasi cha billioni 21 kama stimulus package kwa makampuni 50, then nafikiri huu ndio wakati muafaka wa CWT na chama cha wauguzi kuingia kwenye mgomo,mpaka na wao waingizwe kwenye huu mgao, kumaliza malimbikizo yao ya mishahara tangu enzi za mwalimu. By the way, kama serikali imeweza kutenga billioni 21 kama stimulus, vipi ishindwe kulipa wadeni wake wa ndani? au kwa sababu hawana wasemaji?
 
Kataa ccm, Okoa taifa. hata waje na mahela kiasi gani, kama siyo mpiganaji basi kula pesa, kura peleka sehaemu nyingine. Hizi zote ni mbinu za kupata fedha za kununua shahada na kuhonga khanga vijijini.
 
Please, nipeni majina ya hayo makampuni!!!!???? Hapo suala la uwezeshaji wa makampuni ya kizalendo lipo hapo???? Subiri tuone!!!!! Yangu macho!!!!! For sure ni lazima kuwe na set criteria kwa ajili ya kazi hii!!!!!! Ni kuwa kulingana na set criteria wameshapata 50 coys au ni kuwa wanategemea kutoa kwa 50 coys!!!! Serikali hii, another kind of....
 
Hivi vichekesho sasa. Kwani kupata hasara si sehemu ya biashara au bishara ni faida kila siku? Pesa za walipa kodi zitatumikaje kusaidia kampuni binafsi??
Na hii lugha "kufidia" maana yake hizi pesa ndo wanagawa? At least marekani ni mkopo.
Kweli mkubwa hiki ni kichekesho. Guess what!! The first company in the list kupewa fidia kwa hela za walipa Kodi!!! Naogopa kusema!!!Lol
 
Najiuliza hivi ni makampuni gani hayo 50 ambayo yamepata hasara na kutaabikia kutokana na kuvurugika kwa Uchumi wa Dunia pale nchini kwetu Tanzania?

Ni shughuli gani za uzalishaji mali ambazo makampuni haya yanazifanya?
Mkuu, unadhani fedha za kampeni mwakani zitapatikana wapi?
 
Uchaguzi uko mbioni, sasa njuru zitapatikana wapi wakati EPA, deep green na wengineo mshawapigia kelele.

Hapa ni kudunduliza hadi kipindi kikifika wimbo uwe unaimbika. Uchanguzi ukiisha tunakuja tena kujadili ufisadi wa stumulus package!

Tanzania ndio nchi pekee ya kiafrika iliyotikisika!
 
heshima mbele wakuu, tatizo letu ni kuwa na siasa na wanasiasa (bahati mbaya wanasiasa wamewameza wachumi wetu wote) wasiokuwa na muda wala hamu ya kufikiri... wao kazi yao ni kuangalia USA wamefanya nini na Ulaya (angaklia walivyokuwa na mifano miingi yenye kuangalia nje wamefanya nini), kisha tunataka kuingiza kama yalivyo kwenye uchumi wetu... Hiyo hotuba ukiisoma vizuri inaonyesha kabisa hata huyo mkuu mwenyewe hajui anachokisema.... angalia mifano ya kina TBL etc.....

Hivi wakati ule Gavana wetu mpendwa Ndulu aliposema mtikisiko wa uchumi duniani haujaiathiri Tanzania alikuwa ana maana gani?? tukumbuke tuliongelea hili swala less than 6 months ago tukasema watatugeuga, sasa yamekuwa.....

Nchi ya kisanii inaendeshwa kiusanii na wote tunakaa pembeni tunashangilia na kupiga vigelegele wakati walaji wanajinenepea....

Change.............change...............change!!!
 
this is very serious concern...lazima lifikishwe mbele za wadau wenye ychungu na nchi hii, kwanini viongozi wanatufanya wajinga..hata kikwete alishawahi kusema uchumi wetu haujaguswa na mtikisiko wa uchumi duniani, leo anataka kusaidia kampuni zilizoathirika????
1. hizi kampuni ni zipi?
2. zimekuwa zinachangiaje pato la taifa?
3. uchumi wetu umeathirika kiasi gani kutokana na kuathirika kwa kampuni hizo???
4.tuone historia za biashara zao miaka iliyopita???

JK asiendelee kutubuluza...
 
Samahani watanzania woote,ile sie ni wajinga,hii biashara ya kukubali kuendeshwa day in day out why?!
amani amani,ndio amani ni muhimu lakini sasa sie tumekuwa watumwa.hata wakati wa UKOLONI our masters used to say we had peace and bread to eat why fight for independence.
tunahitaji maandamano ya nchi nzima.nyie wanafunzi wa vyuo vikuu elimu yenu mmepewa ili muiokoe na kuisaidia nchi yenu.sio kuandamana hela zikiwa hazitoshi tu!hela zenu hazitoshi kila siku kwa kuwa zinaliwa mno!nyie waaalimu mishahara yenu viduchu kwa kuwa kuna mijitu ina-ila!!
na nyie miviongozi ya serikali,luxury za kipuuzi na wizi wa kitoto are things of the past!dunia ya sasa hivi a country is respected by how it helps it's people and achieve development.not by few strongmen it has.
haya makampuni tunajua nusu ya hela/au yote mtachukua nyie!kwa ajili ya uchaguzi,na maufisadi yenu yasioisha.
am worn and tired by the level of stupidity and disappointments from our leaders.
 
Dear Interested Observer!

I agree with you hapa Tanzania SIYAONI hayo makampuni hamsini labda as you said serikali iyape stimulus mashirika yake ya umma kama Dawasco,Tanesco, ambayo yanaadhirika vibaya na kupanda kwa bei ya mafuta ili hali Ewura inawazuia kupandisha bei ya haduma wanayotoa kwani hawa jamaa hawafanyi biashara in the real sense. Kama Tanesco wananua umeme kutoka Songas kwa Tshs, 150/=( Ukiongezea na Capacity charge ni karibu Tshs.300/= kwa unit {KWhr) moja) na kuizia Zanzibar kwa Tshs. 50/= na bei ya wastani ya Tshs 120/= kwa wateja wengine hapo hakuna biashara bali ni usanii

Kama JMK aka matonya angetumia ABC ya uchumi aliyosoma pale mlimani zaidi ya miaka 30 iliyopita angeamua kutumia hiyo stimulus katika kustabilize bei ya mafuta pamoja na STABEX kwenye kilimo pamoja na pembejeo ahamasishe kilimo. Mabenki hayana historia ya kuimarisha uchumi!! Hayo makampuni ni ya wabunge na wanamtandao waliompeleka madarakani anataka tu kuwalipa fadhila. BENKI kuu iko Mochwari kama wamekubali kumteua fisadi Peter Noni wa RA akaongoze TIB unatarajia muujiza gani!! Look at those fools hata DECI hawakuigundua for 3 soild years Hamshangai tu kwamba the stupid Minister of Finance alifungua tawi la DECI kule kwao na bado JMK anazidi kumkumbatia asimpige paranja kwa sababu tu ya Udini!! hayo makampuni ambayo hayapeleki BOT audited accounts watayapata wapi?? Si bora mkawapa hata wanafunzi vitabu na walimu mishahara tujue moja??

The president and the govt he is leading is not serious na narudia lini Mkwere akawa serious apart from dancing. Kama kuna kampuni iliyoadhirika kikweli kweli si tungeona imefanya massive layouts na hilo bado halijatokea!!!

Umechangia Uzuri..LKN unapoingiza UDINI unaharibi mada...!!! Talk about Mafisadi...Ina maana angekaa Mtu mwingine asiekuwa na DINI yake ungesemaje....? Hivi ndivyo Mijadala ya JF inavyoharibika....!!!
 
Back
Top Bottom