Serikali kufanyia marekebisho taasisi ya elimu ili kutengeneza vitabu vitakavyoendana na mtaala

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
maja%288%29.jpg


Serikali imepanga kufanya marekebisho makubwa katika taasisi ya elimu nchini ili kuweza kutengeneza vitabu vitakavyoendana na matakwa ya mitaala ya masomo husika vitakavyotumika mashuleni.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo Bungeni dodoma ambapo amesema watatumia wasomi mbalimbali nchini waliojikita kwenye fani ili kutengeneza vitabu bora na kuondokana na makosa yaliyotokea katika vitabu vilivyopita

Akijibu swali kuhusu zoezi la utolewaji wa vitambulisho vya taifa Waziri Mkuu amesema taasisi ya vitambulisho vya taifa “Nida” inaendelea na zoezi la uandikishaji wananchi ili kutoa vitambulisho hivyo ambavyo mpaka sasa vimekwishatolewa katika mikoa zaidi ya tisa nchini

Amesema serikali kupitia taasisi ya Nida imejipanga kufanya kazi hiyo ya uandikishaji kwa umakini mkubwa ili kuepuka kutoa vitambulisho hivyo kwa watu wasio watanzania hasa wananchi wanaoishi katika mikoa ya Pembezoni hivyo isionekane kuwa zoezi hilo linachelewa.


Chanzo; ITV
 
Hivi ni we learn through mistakes au we mistake inorder to learn?
 
Hivi vitabu vilivyotolewa na ma dk wa Taasisi ni shida. Vitabu havina viongozi vya walimu wameleta kitu kipya kinaitwa Miongozo ya masomo, haisaidii ufundishaji
 
Hivi vitabu vya Physics, Chemistry, Biolojia, Hesabu, Kingereza na Kiswahili tulivyo kuwa tunasoma zamani kwani vilikuwa na matatizo gani? Tumevuruga Elimu yetu kutokana na ubinafsi tu, maafisa katika Wizara ya Elimu wanawapatia jamaa zao tenda za kuandika vitabu visivyo kuwa na hadhi yoyoyte mradi wapige hela ndefu na kutajirika, Elimu yetu imefanyiwa usanii mkubwa sana sana hujuma hizi hazina tofauti na wizi wa mchanga wenye madini. Wizara yetu ya Elimu inapaswa kufumuliwa kabisa na kujengwa upya - Wakurugenzi wote na wasaidizi wao wa idara zote waondolewe na kupangiwa kazi nyingine sehemu nyingine kabisa, tukiwalazia damu watandelea na usanii huku Elimu yetu ikishuka exponentially.
 
Back
Top Bottom