comrade igwe
JF-Expert Member
- Jan 12, 2015
- 7,295
- 3,939
Serikali inapitia na kufanya tathimini ya kazi na majukumu ya kila mtumishi wa umma ili kuboresha maslahi ya watumishi wa umma nchini, Kauli hiyo imetolewa na naibu Waziri wa Tamisemi Mh Suleiman Jaffo wakati akijibu maswali ya wabunge kadhaa katika kipindi cha maswali bungeni wabunge walitaka kujua kwann serikali haipandishi madaraja na mishahara kwa watumishi wa umma nchini licha ya zoezi la uhakiki kuisha,
Aidha Mh Jaffo alisema Waziri anaehusika na utumishi wa umma amesema utaratibu wa kupandisha mishahara na madaraja kwa watumishi wa umma upo katika bajeti na watumishi watapewa stahiki zao bila tatizo lolote kwani zoezi la kutafuta wenye vyeti feki na watumishi hewa limekwisha aidha Mh jaffo amesema serikali sasa inapitia na kufanya tathimini za kazi kwa watumishi wote wa umma ili mtumishi apewe anachostahili
TBC live bunge
Aidha Mh Jaffo alisema Waziri anaehusika na utumishi wa umma amesema utaratibu wa kupandisha mishahara na madaraja kwa watumishi wa umma upo katika bajeti na watumishi watapewa stahiki zao bila tatizo lolote kwani zoezi la kutafuta wenye vyeti feki na watumishi hewa limekwisha aidha Mh jaffo amesema serikali sasa inapitia na kufanya tathimini za kazi kwa watumishi wote wa umma ili mtumishi apewe anachostahili
TBC live bunge