Serikali kubana matumizi napo tunasubiri Benki ya Dunia (WB) ituambie? Hatuwezi kuona tunakokwenda?

Plsm

Senior Member
Aug 19, 2021
177
266
Hali ni mbaya sana mitaani na anayebisha akapimwe akili, kwa sasa, wapo wananchi wanaoshindia mkate wa bakhalesa, wapo ambao siku inaweza kupita bila kula kabisa, nina uhakika na hilo, na katika hilo, niseme kwamba, hakuna nchi yenye watu wavumilivu kama Watanzania, si kwenye mambo ya kisiasa, haki zao n.k

Hakuna mwenye matumaini ya kesho na kama wapo ni hao walioko serikarini na wafanyabiashara wakubwa, nao hao wafanyabiashara wanawaza kesho itakuwaje maana bidhaa zimerundikana tu stoo, mitaani pesa hakuna, yaani ni mabalaa juu ya balaa

Wakati wazungu wakiendelea kutukopesha, sisi huku tunazitumbua tu bila kufahamu kesho itakuwaje

Tunaposikia nchi kama Lebanon zipo kwenye hatua mbaya kabisa ya kufilisika na hakuna taifa linalojitokeza kusema litasaidia kuinua uchumi wa nchi hiyo, mikopo na Misaada kwa sasa inaelekezwa kwenye nchi ambazo bado zina rasilimali ili mzungu badaye avune na kuwaacha mahohehahe

Kwani sisi hatuwezi kubana matumizi huku tukiendea kesho kwa tahadhari kubwa?

Je, tunawatu ambao kweli wanauwezo wa kuipima kesho itakuwaje ili kuishauri serikali au tunasubiri hali iwe mbaya zaidi kuliko sasa na kusababisha taharuki kubwa miongoni mwa jamii?

Hakuna vita mbaya kama ya kugombania chakula

Serikali iwe chonjo sana na mwelekeo wa dunia sasa!


 
Mimi nadhani tunapitia hali hii maana tuliikataa ile ya mwanzo yenye machungu mengi,lakini unafuu mkubwa wa maisha.

Tuombe sana Mungu atupe hekima tujue kama taifa tunataka nini kwa maendeleo mapana ya kesho yetu.

Haishangazi kuona leo matukio ya unyanyasaji yanazidi kuliko yale ya "Jiwe walilokataa waashi",tutubu kwamba tulikosea sana kumuombea 'Jamaa' kifo mapema kabla hajatupeleka nchi ya ahadi" aliyokuwa anaijenga.

Now ni mwendo wa kodi tu kila sekta,ambazo hazileti unafuu wowote kwa mwananchi zaidi ya maumivu,inashangaza kuona mpaka fedha ya likizo ya mtumishi wa uma inakatwa kodi.

Tutubu kwakweli.
 
Mimi nadhani tunapitia hali hii maana tuliikataa ile ya mwanzo yenye machungu mengi,lakini unafuu mkubwa wa maisha...
Ni vuzuri sana kuwa na Taifa la wacha MUNGU, lakini ni vizuri zaidi kila mwenye kuongoza Taifa la watu wacha MUNGU kuacha kutembea ktk njia hiyo ya haki na kujisahihisha kila wakati, kuwatendea mema watu wenye kushitakia mambo yao kwa MUNGU
 
Africa bala la giza, wasipoambiwa, hawawezi kufanya hiyo kitu
 
Back
Top Bottom