Serikali, KIA itaua barabara zetu

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,215
3,587
Kufuatia ndege kubwa ya shehena ya mizigo kukaribia kukamilika kuundwa kiwandani, serikali imefanya uamuzi wa kubadili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa KIA kuwa kitovu cha kimkakati cha mizigo yaani Strategic Cargo Hub kwa shehena za mizigo ya safari za anga.

Pamoja na kwamba kimsingi uamuzi ni mzuri unaolenga kupunguza msongamano JNIA, Bandari na barabara za Dar pamoja na kuleta hamshahamsha kwenye uwanja wa KIA, lakini hofu yangu ni kuwa shehena hizo zitalazimika kusafirishwa kwa njia ya barabara kwenda sehemu mbalimbali za nchi ikiwemo Dar.

Nachelea barabara ya T2 na zingine kuwa hatarini kuharibika baada ya muda fulani wa hub hii kutingwa.

Mbadala wa KIA nashauri wazo hili zuri litekelezwe kwenye uwanja wa ndege wa hadhi ya kikanda wa Geita Chato (Regional Airport) kwa sifa moja kuu salama kwa barabara zetu; ya kuwa karibu na reli za SGR na MGR ambazo zitapokea shehena hizo toka uwanja wa ndege wa kikanda wa Geita Chato na kuziingiza kwenye mtandao wa reli nchini na kusalimisha barabara zetu zilizojengwa kwa gharama kubwa.
 
Kimsingi unajaribu kuupigia upatu uwanja wa Chato ili walau utumike , isiwe a "white elephant project" , swali litakuja je Kuna bidhaa zinazozalishwa karibu na chato zenye kuakisi uhitaji wa kuwa "air lifted" ? ( Tusizungumzie minofu ya samaki) , KIA kuwa hub chap kwa haraka kutarahisisha usafirishaji wa maua na veggies zinazozalishwa ukanda huo( na zitakazozalishwa kwa wingi hapo baadae).
 
Una uelewa finyu kwenye Usafirishaji wa bidhaa. Bidhaa zitakazosafirishwa kupitia KIA ni za mikoa ya karibu na KIA tu.
 
Kimsingi unajaribu kuupigia upatu uwanja wa chato ili walau utumike , isiwe a "white elephant project" , swali litakuja je Kuna bidhaa zinazozalishwa karibu na chato zenye kuakisi uhitaji wa kuwa "air lifted" ? ( Tusizungumzie minofu ya samaki) , KIA kuwa hub chap kwa haraka kutarahisisha usafirishaji wa maua na veggies zinazozalishwa ukanda huo( na zitakazozalishwa kwa wingi hapo baadae).
Samaki, madini, utalii, mazao, mazao ya mifugo, miti migumu toka msitu wa Tabora ambao ni extension ya msitu wa kiikweta wa Congo.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Kwamba ndege ije na mizigo ishushe KIA afu mizigo irudishwe Dsm kwa roli?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Ndiyo utusaidie kuwauliza kuwa mtu wa Dar akiagiza mzigo uje kwa njia ya haraka ya ndege badala ya meli labda ni chanjo za dharura alafu sera imesema hub ya mizigo ni KIA je, mizigo hiyo itakujaje Dar kama siyo kwa njia ya malori? Maana hata MGR iliyokarabatiwa kwa gharama kubwa imeshindwa kutumika kufuatia corridor hiyo kutokuwa na mizigo inayoweza kukuza uchumi wa reli. And what if kama shehena ya dharura ni silaha za kwenda Mtwara kudhibiti ISIS, itafikaje Mtwara toka KIA kama siyo kwa njia ya malori unayouliza? Sasa naona unaanza kuelewa mantiki ya mada.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom