Intelligence Justice
JF-Expert Member
- Oct 23, 2020
- 3,032
- 3,478
Kupitia Jukwaa Tukufu,
Nawasilisha ushauri na maoni yangu kupendekeza kwa serikali ya Jamhuri wa Tanzania kujenga bwawa/lambo kubwa linalotokana na uvunaji wa maji ya mvua (rainfall water catchment dam).
katika eneo lolote litakalobainishwa na wataalamu kati ya wilaya za Kongwa, Chamwino na Mpwawa ambako kuna utambarare unaozungukwa na vijilima na makorongo hatarishi pindi mvua inyeshapo.
Bwawa pendekezwa ligawanywe mara mbili kwa matumizi tofauti
1. Sehemu ya kwanza ya lambo hilo itahudumia Kilimo cha mboga mboga, zabibu, alizeti, karanga, korosho na ufugaji wa kisasa wa mifugo ya ng'ombe. mbuzi na kuku (matumizi bora ya maji kwa njia ya dripu yataelekezwa vizuri na watalaamu)
2. Sehemu ya pili itahudumia wananchi kwa ajili ya mapumziko, kuogelea na uvuvi mdogo wa ndoana (maji haya yatatengenezewa mfumo wa kutembea kupitia vyumba maalum ambavyo vitayafanya kujirejesha kwa usafi kama ilivyo kwenye mabwawa ya maji machafu
3. Eneo hilo la bwawa ambalo halitahitaji kuchimba chini ardhini badala yake eneo lenye uwezo wa kupokea maji kutoka pande zote kisha matuta makubwa yenye upana wa kupita gari juu yatajengwa kwa kuzingatia taratibu za ujenzi na uimara wa udongo.
4. Eneo hilo la bwawa linatakiwa kupandwa miti isiyotumia kiwango kikubwa cha maji na rafiki wa utunzaji mazingira.
5. Eneo la bwawa linatakiwa angalau liwe na ukubwa wa kilomita za mraba kati ya (20*25) sawa na 500 Km2 au (20*30) sawa na 600 Km2.
6. Mibuyu yote iliyotamalaki maeneo ya Chamwino, Kongwa na Mpwawa isikatwe ila itunzwe na tunda na magome yatumike kwa matumizi ya binadamu ya asili na ya viwandani kama utengezaji wa sabuni ya mbuyu, nk
Endapo serikali itaridhia na kuweka ksenye mpango iwa utekelezaji manufaa yatakayopatikana itakuwa ni kumbukumbu isiyofutika vizazi na vizazi kwa kuchochea utayari wa kila mtu kuishi na kuwekeza Dodoma maana palipo na maji kwa matumizi ya kibinadamu, mimea, shughuli za kiuchumi na kijamii migogoro hupungua.
Nawasilisha kwa mjadala kutoka kwenye tanuru la fikira chanya.
Nawasilisha ushauri na maoni yangu kupendekeza kwa serikali ya Jamhuri wa Tanzania kujenga bwawa/lambo kubwa linalotokana na uvunaji wa maji ya mvua (rainfall water catchment dam).
katika eneo lolote litakalobainishwa na wataalamu kati ya wilaya za Kongwa, Chamwino na Mpwawa ambako kuna utambarare unaozungukwa na vijilima na makorongo hatarishi pindi mvua inyeshapo.
Bwawa pendekezwa ligawanywe mara mbili kwa matumizi tofauti
1. Sehemu ya kwanza ya lambo hilo itahudumia Kilimo cha mboga mboga, zabibu, alizeti, karanga, korosho na ufugaji wa kisasa wa mifugo ya ng'ombe. mbuzi na kuku (matumizi bora ya maji kwa njia ya dripu yataelekezwa vizuri na watalaamu)
2. Sehemu ya pili itahudumia wananchi kwa ajili ya mapumziko, kuogelea na uvuvi mdogo wa ndoana (maji haya yatatengenezewa mfumo wa kutembea kupitia vyumba maalum ambavyo vitayafanya kujirejesha kwa usafi kama ilivyo kwenye mabwawa ya maji machafu
3. Eneo hilo la bwawa ambalo halitahitaji kuchimba chini ardhini badala yake eneo lenye uwezo wa kupokea maji kutoka pande zote kisha matuta makubwa yenye upana wa kupita gari juu yatajengwa kwa kuzingatia taratibu za ujenzi na uimara wa udongo.
4. Eneo hilo la bwawa linatakiwa kupandwa miti isiyotumia kiwango kikubwa cha maji na rafiki wa utunzaji mazingira.
5. Eneo la bwawa linatakiwa angalau liwe na ukubwa wa kilomita za mraba kati ya (20*25) sawa na 500 Km2 au (20*30) sawa na 600 Km2.
6. Mibuyu yote iliyotamalaki maeneo ya Chamwino, Kongwa na Mpwawa isikatwe ila itunzwe na tunda na magome yatumike kwa matumizi ya binadamu ya asili na ya viwandani kama utengezaji wa sabuni ya mbuyu, nk
Endapo serikali itaridhia na kuweka ksenye mpango iwa utekelezaji manufaa yatakayopatikana itakuwa ni kumbukumbu isiyofutika vizazi na vizazi kwa kuchochea utayari wa kila mtu kuishi na kuwekeza Dodoma maana palipo na maji kwa matumizi ya kibinadamu, mimea, shughuli za kiuchumi na kijamii migogoro hupungua.
Nawasilisha kwa mjadala kutoka kwenye tanuru la fikira chanya.