Serikali izibane hotel zote za kulala Tanzania zinaibia wateja

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,911
51,902
Kawaida mtu ukiingia hotel muda unaoingia ndio kesho yake unatakiwa uwe muda wako wa kutoka sababu unalipia kwa siku yaani masaa 24

Mahotel ya Tanzania yamejiwekea utaratibu wa wizi kuwa muda wa kutoka lazima uwe saa nne asubuhi bila kujali umeingia saa ngapi.

Nilikuwa Nigeria niliingia saa nne usiku hotelini wakaniambia muda wangu wa kutoka ni kesho usiku muda kama huo huo nilioingia.Wanahesabu MASAA 24 kamili bila kupunja

Tanzania hata uingie saa nane usiku hotelini wanataka saa nne asubuhi uachie chumba wakati umelipia siku nzima wao wanakulaza masaa machache tu na kukwambia toka kama vile wewe ni changudoa uliyeenda kupanga chumba short time

Wanasheria bebeni hili kesi buruzeni wamiliki mahoteli mahakamani wakome wizi
 
Hapa ukiacha wageni wa kiukweli wanaolala Hotelini

Huu uzi utaungwa mkono kwa asilimia kubwa pia na sisi "wageni wenyeji"(wazinzi/ mabaharia) tunataka haki yetu ya kunyanduana masaa 24😂😂😂😂

Yani jumamosi nikipotea nyumbani jion jion naenda kupiga ulabu naingia lodge saa8 usiku nashinda kesho yake yote hadi usiku hahahaaaa
 
Daaah
Kweli upumbavu ni mzigo sana.
Kwahiyo ukizaliwa March tubadili mwaka uanze March
Wiki ianze J5
Acheni ujinga wenu. Kimsingi kufika hiyo saa 4 asubuhi ni feva tu. Siku inaisha saa 6 usiku
Ukiingiia hotelini ukasema nalala kwa siku moja Tar 15.12.2019 unapaswa uishi hotelini hapo kwa siku hiyo tuu. Sasa ukiingia saa 4 usiku inapaswa saa 6:01 ulipe upya lakini wanakupa feva mpaka kesho saa 4 asubuhi halafu unaleta matapishi hapa.
Pumbavu sana
 
YEHODAYA, Akili za kimaskini tu hizi. Wewe ulifikia hostel na siyo hotel. tunaotumia hotel tunakwenda hotel hata kupumzika tu kusubili departure time badala ya kukaa airport masaa mengi.

Usiandike tena huu ujinga wako mbele ya watu wenye akili timamu na exposure kubwa.

Hotel zote zenye hadhi kuna check in and check out time. Cleaning room time. Free breakfast time and so on........





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu mtoa post katumwa na mabeberu,hajui kama sirikali ya mtukufu haikosolewi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Hajui kitu kinaitwa standard
Pia hajui sehemu inaitwa mwanzo na mwisho
Mfano: mwanzo wa mwaka wa serekali ni July 1. Mwanzo wa mwaka wa kitaaluma ni October, na mwanzo wa mwaka wa calebder ni Jan 1.
Kuna nchi mfano za ulaya, marekani, Philippine na Uturuki, Muda wa kuchukua chumba unaanza saa saba mchana na kumalizika saa 6 mchana. Ukifika saa 4, 5 au 6 asubuhi hawakupi chumba mpaka muda ufike.
Sasa huyu pimbi kashiba kande anatuletea upupu hapa
 
Tena huu hua ni wizi hili suala liangaliwe maana masaa 24 yawe yanahesabiwa kiufasaha maana hata vifurushi vya simu ukiunga saa mbili usiku hadi kesho saa mbili usiku ndio masaa 24 yanakamilika iweje hotel tuwe tunatolewa nje kabla ya masaa 24 kukamilika, halafu ukiingia kuanzia saa sita 6 kamili usiku unalazimishwa uandike tarehe ya jana huu ni wizi wa mchana kweupe serikali iliangalie hili


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom