Serikali iweke kikomo cha kuwania Ubunge wa Viti Maalumu

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,060
4,046
Viti maalum vya wanawake ni utaratibu unaopatikana katika nchi mbalimbali unaolenga kuongeza idadi ya wanawake na makundi yao katika bunge na mabaraza. Kuna nchi nyingi za dunia zilizochukua hatua za kuongeza nafasi za wanawake serikalini kulingana na Mkataba kuhusu ufutaji wa ubaguzi wote wa wanawake (Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women) uliosainiwa na mataifa 189 tangu kuanzishwa mwaka 1981 na kuimarishwa na azimio la Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 2011.

Kwa tafsiri rahisi kabisa ni mpango mahsudi ambao unalenga kuwajengea uwezo kundi maalumu katika kushika nafasi mbalimbali katika ngazi ya maamuzi na uongozi.

Mpango huo unalenga sana katika kupunguza na kutokomeza dhana za ukandamizaji wa kijinsia na makundi maalumu kwa kuwapa fursa ya kupata nafasi za usawia katika maamuzi mbalimbali na uongozi.

Cha ajabu sasa tunawaona baadhi ya wawakilishi wetu kupitia viti maalumu wanaonekana kama hawajaielewa falsafa ya viti maalumu vizuri, maana mbunge anapata fursa ya kuteuliwa zaidi ya mara mbili lakini bado anakuwa hajajiamini na kujijengea dhana ya ushindani wajimbo.

Nashauri Serilikali iweke muda maalumu na kusiwe na fursa ya kujirudia mara mbili, na muwakilishi atayepata fursa ya kuteuliwa viti maalum afanyiwe majaribio baada ya kumaliza huo muda maalumu ili tuone kama dhana ya kumjenga katika kipindi alichopewa imemkaa? Sina maana ya kuvipinga viti maalumu

Viti Maalumu ni chombo cha kutupa fursa na kujiandaa, sio tubaki hapo hapo. Mbunge kama Benadeta Mshashu amekomaa sasa kiasi kwamba anayeweza kuwania jimbo bila kutegemea viti maalum, hii itasaidia kutoa fursa kwa wanawake wengine mkoa wa Kagera kuwania viti maalum.

Pamoja na kuangalia yote hayo, watanzania tujitathmini tangu tumeanzisha viti maalumu,

Je, lile lengo letu tunafanikiwa?

Je, wawakilishi wa viti maalumu wanaelewa kwa nini wamepata fursa ya kuwawakilisha watu maalumu katika viti hivyo maalumu?
 
Viti maalum vya wanawake ni utaratibu unaopatikana katika nchi mbalimbali unaolenga kuongeza idadi ya wanawake na makundi yao katika bunge na mabaraza. Kuna nchi nyingi za dunia zilizochukua hatua za kuongeza nafasi za wanawake serikalini kulingana na Mkataba kuhusu ufutaji wa ubaguzi wote wa wanawake (Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women) uliosainiwa na mataifa 189 tangu kuanzishwa mwaka 1981 na kuimarishwa na azimio la Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 2011.

Kwa tafsiri rahisi kabisa ni mpango mahsudi ambao unalenga kuwajengea uwezo kundi maalumu katika kushika nafasi mbalimbali katika ngazi ya maamuzi na uongozi.

Mpango huo unalenga sana katika kupunguza na kutokomeza dhana za ukandamizaji wa kijinsia na makundi maalumu kwa kuwapa fursa ya kupata nafasi za usawia katika maamuzi mbalimbali na uongozi.

Cha ajabu sasa tunawaona baadhi ya wawakilishi wetu kupitia viti maalumu wanaonekana kama hawajaielewa falsafa ya viti maalumu vizuri, maana mbunge anapata fursa ya kuteuliwa zaidi ya mara mbili lakini bado anakuwa hajajiamini na kujijengea dhana ya ushindani wajimbo.

Nashauri Serilikali iweke muda maalumu na kusiwe na fursa ya kujirudia mara mbili, na muwakilishi atayepata fursa ya kuteuliwa viti maalum afanyiwe majaribio baada ya kumaliza huo muda maalumu ili tuone kama dhana ya kumjenga katika kipindi alichopewa imemkaa? Sina maana ya kuvipinga viti maalumu

Viti Maalumu ni chombo cha kutupa fursa na kujiandaa, sio tubaki hapo hapo. Mbunge kama Benadeta Mshashu amekomaa sasa kiasi kwamba anayeweza kuwania jimbo bila kutegemea viti maalum, hii itasaidia kutoa fursa kwa wanawake wengine mkoa wa Kagera kuwania viti maalum.

Pamoja na kuangalia yote hayo, watanzania tujitathmini tangu tumeanzisha viti maalumu,

Je, lile lengo letu tunafanikiwa?

Je, wawakilishi wa viti maalumu wanaelewa kwa nini wamepata fursa ya kuwawakilisha watu maalumu katika viti hivyo maalumu?
Andiko zuri kabisa. Naunga mkono.
 
Viti maalum vya wanawake ni utaratibu unaopatikana katika nchi mbalimbali unaolenga kuongeza idadi ya wanawake na makundi yao katika bunge na mabaraza. Kuna nchi nyingi za dunia zilizochukua hatua za kuongeza nafasi za wanawake serikalini kulingana na Mkataba kuhusu ufutaji wa ubaguzi wote wa wanawake (Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women) uliosainiwa na mataifa 189 tangu kuanzishwa mwaka 1981 na kuimarishwa na azimio la Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 2011.

Kwa tafsiri rahisi kabisa ni mpango mahsudi ambao unalenga kuwajengea uwezo kundi maalumu katika kushika nafasi mbalimbali katika ngazi ya maamuzi na uongozi.

Mpango huo unalenga sana katika kupunguza na kutokomeza dhana za ukandamizaji wa kijinsia na makundi maalumu kwa kuwapa fursa ya kupata nafasi za usawia katika maamuzi mbalimbali na uongozi.

Cha ajabu sasa tunawaona baadhi ya wawakilishi wetu kupitia viti maalumu wanaonekana kama hawajaielewa falsafa ya viti maalumu vizuri, maana mbunge anapata fursa ya kuteuliwa zaidi ya mara mbili lakini bado anakuwa hajajiamini na kujijengea dhana ya ushindani wajimbo.

Nashauri Serilikali iweke muda maalumu na kusiwe na fursa ya kujirudia mara mbili, na muwakilishi atayepata fursa ya kuteuliwa viti maalum afanyiwe majaribio baada ya kumaliza huo muda maalumu ili tuone kama dhana ya kumjenga katika kipindi alichopewa imemkaa? Sina maana ya kuvipinga viti maalumu

Viti Maalumu ni chombo cha kutupa fursa na kujiandaa, sio tubaki hapo hapo. Mbunge kama Benadeta Mshashu amekomaa sasa kiasi kwamba anayeweza kuwania jimbo bila kutegemea viti maalum, hii itasaidia kutoa fursa kwa wanawake wengine mkoa wa Kagera kuwania viti maalum.

Pamoja na kuangalia yote hayo, watanzania tujitathmini tangu tumeanzisha viti maalumu,

Je, lile lengo letu tunafanikiwa?

Je, wawakilishi wa viti maalumu wanaelewa kwa nini wamepata fursa ya kuwawakilisha watu maalumu katika viti hivyo maalumu?
Umenikumbusha mama Shaly Raymond. Amegombea mwaka wa 20 na bado ni mbunge wa viti maalum hadi sasa 2022
 
Viti maalum vya wanawake ni utaratibu unaopatikana katika nchi mbalimbali unaolenga kuongeza idadi ya wanawake na makundi yao katika bunge na mabaraza. Kuna nchi nyingi za dunia zilizochukua hatua za kuongeza nafasi za wanawake serikalini kulingana na Mkataba kuhusu ufutaji wa ubaguzi wote wa wanawake (Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women) uliosainiwa na mataifa 189 tangu kuanzishwa mwaka 1981 na kuimarishwa na azimio la Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 2011.

Kwa tafsiri rahisi kabisa ni mpango mahsudi ambao unalenga kuwajengea uwezo kundi maalumu katika kushika nafasi mbalimbali katika ngazi ya maamuzi na uongozi.

Mpango huo unalenga sana katika kupunguza na kutokomeza dhana za ukandamizaji wa kijinsia na makundi maalumu kwa kuwapa fursa ya kupata nafasi za usawia katika maamuzi mbalimbali na uongozi.

Cha ajabu sasa tunawaona baadhi ya wawakilishi wetu kupitia viti maalumu wanaonekana kama hawajaielewa falsafa ya viti maalumu vizuri, maana mbunge anapata fursa ya kuteuliwa zaidi ya mara mbili lakini bado anakuwa hajajiamini na kujijengea dhana ya ushindani wajimbo.

Nashauri Serilikali iweke muda maalumu na kusiwe na fursa ya kujirudia mara mbili, na muwakilishi atayepata fursa ya kuteuliwa viti maalum afanyiwe majaribio baada ya kumaliza huo muda maalumu ili tuone kama dhana ya kumjenga katika kipindi alichopewa imemkaa? Sina maana ya kuvipinga viti maalumu

Viti Maalumu ni chombo cha kutupa fursa na kujiandaa, sio tubaki hapo hapo. Mbunge kama Benadeta Mshashu amekomaa sasa kiasi kwamba anayeweza kuwania jimbo bila kutegemea viti maalum, hii itasaidia kutoa fursa kwa wanawake wengine mkoa wa Kagera kuwania viti maalum.

Pamoja na kuangalia yote hayo, watanzania tujitathmini tangu tumeanzisha viti maalumu,

Je, lile lengo letu tunafanikiwa?

Je, wawakilishi wa viti maalumu wanaelewa kwa nini wamepata fursa ya kuwawakilisha watu maalumu katika viti hivyo maalumu?
Kama ilivyo kiti cha rais, nafasi za ubunge pia ziwe na ukomo wa vipindi viwili !! Iwekwe kwenye katiba
 
mwanamwana ana hoja nzuri sana. Kwanza, ni kweli , Wabunge waliopa sasa hivi ''wote ni wa viti maalumu'' . Kufuatia uchafuzi wa 2020. Magufuli aliwaambia '' kama siyeye nani angerudi bungeni''.

Pili, lazima kuweka ukomo ili kutoa nafasi za fikra mpya. Habari ya Ubunge miaka 20 haifai

Tatu, mleta mada anasema viti maalumu ni kuwajengea uwezo Wanawake waweze kupambana majimboni. Mbunge wa miaka 15 anasubiri uwezo upi kuwania jimboni. Watoto waliopo wanapata fursa gani ya uzoefu ikiwa watu wanakalia viti miaka 15-20!

Nne, maswali ya kujiuliza, viti maalumu wamekuwa na mchango gani wa kudhani tunawahitaji kwa miaka mingine. Miaka 50 ya Uwepo wao imetupa nini cha kuamini tunawahitaji?

Tano, tuna Wanawake; Rais, Spika, Waziri wa mambo ya nje, Waziri wa Ulinzi kwa uchache. Ikiwa tunawaamini katika nafasi hizo, kwanini Wabunge Wanawake waendelee kupewa viti maalumu?

Kwanini siku zijazo tuendelee na utaratibu wa kupata ''Mawaziri'' kwa Ubunge wa kuteuliwa au viti maalimu na si wabunge wa kuchaguliwa?
 
Katiba ndio iweke ukomo wa kugombea Ubunge
Serikali iweke ajira za mikataba miaka 5 iwe hiari kumi iwe lazima
Liwekwe FAO la kujitoa jaman
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom