Kama unaona hakuna umuhimu huo, ungeona pia umuhimu wa kutoandika uliyoandika kwa kutumia mtandao. 'Otherwise, you are not true to yourself'.Hii nchi ina maadui wengi sana wa kiuchumi na kisiasa ambao hawaitakii mema. Hivyo serikali iwe makini.
Hizi ni nyakati mbaya sana maana mitandao inatumika vibaya na mara nyingi hutumika hata kuiba siri za nchi na kueneza propaganda za uongo.
Tumeshuhudia wadukuzi wakifanya udukuzi kwa kueneza propagada za uongo na kusababisha taharuki hasa nyakati za uchaguzi. Mimi binafsi naipongeza Serikali kwa hatua ilizofanya kwa maslahi ya taifa letu.
Hatujui akina Amsterdam na baadhi ya mabeberu walikuwa na mpango gani wa kudukua na kuingilia mawasiliano ya mtandao wa serikali yetu ili kuvuruga uchaguzi.