serikali iwashukuru wanywaji

Ochu

JF-Expert Member
May 13, 2008
975
47
Mbunge wa Moshi Mjini (Chadema) Phillemon Ndesamburo amesema kwamba wanywaji pombe ni watu wazuri kwa serikali kwa kuwa ndio wachangiaji wakuu wa uchumi.

Akichangia bajeti hiyo, Mbunge wa Moshi (Chadema), Phillemon Ndesamburo alisema tangu azaliwe bajeti
zote zinaongeza kodi kwenye pombe na sigara bila kuangalia maeneo mengine ya kutoza kodi.

''Watu wamesifia sana TRA, wanafanya kazi nzuri wanaingiza fedha nzuri. Mimi nasema hapana, ningesema wangetufungulia njia mbadala, njia nyingine nyingi, ningesema wamefanya kazi nzuri,'' alisema Ndesamburo na kuongeza:

''Wanywaji pombe nadhani ni watu wazuri kwa serikali ndio wachangiaji wakuu wa uchumi, siyo hiyo tu tunawafanya wananchi wanakuwa mabega kwa kurudi kwenye piwa (gongo) na hii inakuwa gharama nyingine kwa hospitali kuwahudumia.''

Ndesamburo alisema, hakuna chanzo kipya kilichobuniwa na TRA kupanua wigo wa kodi, lakini wamekuwa wakiendelea kumkamua Mtanzania ambaye amechoka.

Kuhusu kilimo, Ndesamburo alisema sio kila mtu ni mkulima na kutahadharisha kwmba, serikali isifanye makosa kama ilivyofanya kwa wafanyabiashara kuwaita wote Wamachinga.
 
Nchi yetu inapoelekea kwa kweli si pazuri si mbaya sana kama sisi wanywaji tukishukuriwa kwa kazi nzuri tunayofanya ya kuchangia kukua kwa uchumi wa nchi yetu ila ni kweli kwamba serikali ibuni njia nyingi na mbadala kwa ajili ya kuongeza kodi its not good kuwa over dependent mainly one only one source of kodi.hive have you ever thot itakuwaje siku people stoop drinking.my you everything is possible under the sun na hizi pombe watu kila siku tunazudi kuwa aware na aftermath yake.Wana JF from what I learnt yesterday pombe ni chanzo kikubwa cha Hepatitis B.Pliz be on the watch out.
 
inashangaza serikali isivyoona inavyobana watu wachache, ni uvivu wa kufikiri au wako bize kupanga ulaji binafsi?
 
Ni kweli kabisa,can you imagine kabla ya TBL kupewa makaburu ilikuwa inapewa ruzuku na serikali kujiendesha na kuuza bia chafu na za mgawo na hata Tax walikuwa hawalipi sababu walikuwa hasara tupu,lakini nafikiri mlipa kodi mkubwa kwa serikali ni mafuta na payroll ya wafanyakazi...ila ni kweli kuna vyanzo vingi sana ambavyo tungeweza kuweka mikakati na kukusanya pesa za kutosha kuliko sasa njaa inavyotumaliza kwa incompetency ya wachache.
 
Serikali inapaswa ifikirie zaidi ya kila mwaka kifikiria wanywa pombe na wavuta sigara..hivi wote tukiamua 'kuokoka' itakuwaje? ndo serikali itategemea wafanyakazi tu?
 
Ndesamburo is right! They should think of relaxing traffick rules ili wanywa pombe wasiadhibiwa kwa kuendesha gari wakati wakiwa wamelewa! Mimi naamini wangekusanya kodi kwenye madini na utalii, wala kulikuwa hakuna haja ya kubembeleza wafadhili kwa ajili ya bajeti. Na bajeti ingepanda hadi trillion kumi na nne!
 
Ukiangalia wanao buni na kutunga bajeti unaweza kusema ni walokole kwani hawapendi kusikia sigara na pombe kwani kila mwaka ushuru unapanda na haya makampuni moja kwa moja wapo wazawa lakini makampuni ya kigeni yanapeta tu bila kulipa kodi na wanasema wanavutia uwekezaji.Hapa naona tunakalibisha wakoloni kwa kupitia serikali haiwezekani mtu atumie ardhi yetu kila kitu kisha wao wanapata faida kisha wanaondoka zao.
Anaye umia hapa ni mlalahoi huyo huyo.
Angalia bajeti ya ZNZ nayo ni pombe kwa hiyo haya makampuni yakifa gafla watapata wapi chanzo cha mapato????
 
Ukiangalia wanao buni na kutunga bajeti unaweza kusema ni walokole kwani hawapendi kusikia sigara na pombe kwani kila mwaka ushuru unapanda na haya makampuni moja kwa moja wapo wazawa lakini makampuni ya kigeni yanapeta tu bila kulipa kodi na wanasema wanavutia uwekezaji.Hapa naona tunakalibisha wakoloni kwa kupitia serikali haiwezekani mtu atumie ardhi yetu kila kitu kisha wao wanapata faida kisha wanaondoka zao.
Anaye umia hapa ni mlalahoi huyo huyo.
Angalia bajeti ya ZNZ nayo ni pombe kwa hiyo haya makampuni yakifa gafla watapata wapi chanzo cha mapato????


kisha eti 'hawawataki wanywa pombe'......
 
Serikali inatakiwa ibadilike katika kutafuta vianzio vipya vya mapato na kuimarisha vyanzo vya mapato vilivyopo, kupandisha bei ya vinywaji kila mara ni kupunguza idadi ya lita zinazouzwa na viwanda vya soda na bia kila mara.

Ningekuwa waziri wa fedha ningepunguza kwa sh.300 kwenye lita moja ya bia, hatua hii ingeongeza pato la taifa kwa sababu zifuatazo:

1. Unapopunguza bei ya bidhaa kwa bei ndogo, unawezesha wananchi wengi kumudu kuinunua. Kama kiwanda kilikuwa kinatengeneze chupa 1000 kwa siku na mahitaji yakiongezeka, kiwanda kitaongeza uzalishaji maradufu kwa sababu soko la uhakika lipo na bei ya bidhaa ipo chini.

2. Utaondoa kundi kubwa la wanywaji wa pombe za kienyeji ambazo serikali haikusanyi kodi yoyote zaidi ya kuzalisha majeruhi wa afya.

3. Bajeti ya wizara ya afya itapungua kwani afya za wananchi zitaimarika, kwa sasa serikali inaongeza kodi kwenye bidhaa za vileo, lakini pesa hiyohiyo inatakiwa iende kwenye wizara ya afya kutibu majeruhi wa pombe ya gongo.
 
Back
Top Bottom