Serikali itoe pedi(vitaulo) kwa wanafunzi wa kike shule zote za sekondari Tanzania

Marisi schweini

Senior Member
Dec 3, 2018
130
374
Wasalaam wanajukwaa...!! Kulingana na hali ya uchumi wa wananchi walio wengi hasa vijijini ambako wanaishi asilimia zaidi ya 75 kuwa mbaya ambapo walio wengi wanaishi chini ya msitari wa umasikini hivo kushindwa kuhimili hata mahitaji msingi ya binadamu achilia mbali mahitaji mengineyo muhimu kama afya n.k,

Wasichana wengi walio katika umri wa kupevuka wamekuwa wakishindwa kuhimili gharama za kununua vitaulo hivi na kujikuta wakitumia vipande vya khanga n.k ambavyo sio salama kwa afya zao. Wengine wamejikuta wakikosa kujiamini na kuathirika kisaikolojia huku wengine wakishindwa kuhudhuria shule siku ambazo wako kwenye hedhi kutokana na kukosa vitaulo vya kuwasitiri.

Wengine wamejikuta wakidanganyika na kuingia kwenye tabia povu ili kuweza kupata pesa za kustahimili kununua pedo kutokana na hali duni ya kipato cha familia

Naomba serikali iangalie uwezekano wa kupeleka vitaulo hivi shule za sekondari ambapo kila msichana ataweza kupata hitaji hili la msingi. Serikali inaweza kuamua kutafuta vyanzo cha kufund na napendekeza mojawapo iwe makato ya asilimia kadhaa ya mshahara wa wabunge na mawaziri pamoja na kuongeza kodi kwenye vipodozi. Naomba kuwakilisha

Cc: Paschal mayalla ; zitto; Faiza fox;
 
Hili suala halina chama kwasababu linahusu afya za watanzania wote. Kwani hawa wasichana ndo watakuja kuwa wazazi wa taifa
 
Wazazi wapo wapi? Elimu bure inatosha. Mambo mengine tupambane na hali zetu.
Baadae tutaanza kuomba wanunuliwe na chupi!
 
Vipedi viko kwenye kampuni vinawekewa nembo na maandishi ya Hapa Kazi Tu!...ndio visambazwe.
 
Huo ni ushauri mzuri ambao serikali yapaswa kuuchua kama sehemu ya kujali Afya ya mtoto wa kike
 
Hivi Hedhi Ni Ugonjwa!?, Hivi Hedhi Imeanza Miaka Ya Hivi Karibuni Nini? Ikiona Ni Vema Na Ifanye, ! Vya Bure Ni Ghari Mno Kuvimudu, Ni Kheri Waendelee Hivyo Hivyo, Wahimizwe Usafi Tu,.
 
Wakati inafikiria ushauri wako naomba na mimi niongeze ombi lingine kwa serikali yetu kuwa ilete Condoms hapa makambako. Hali ni mbaya sana! Kuna uhaba wa Condom sana hapa ,wiki ya pili sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii serikali iliyishindwa kusambaza hata panadol na kondom tena nyingine za msaada, mnataka na kuitwisha mzigo wa pedi, kweli tuliotumwa na mabeberu tuna tabu.


Kondom zimekuwa adimu watu wanapigana kavukavu maambukizi yanakuwa kwa kasi baada ya mda kadhaa janga maradhi litazidi kupaa, mwishon yale makabur nayo wataita viwanda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi hizo tauro si zilifutiwa kodi kwenye bunge la bajeti mwaka wa fedha 2018/19 au ilikua politksi..? Mi nilitegemea zishuke bei sio kutolewa bure!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom