Serikali itazameni sekta binafsi kama wasaka fursa na faida na sio waunga mkono juhudi katika mipango na mikakati ya serikali.

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,471
46,002
"Nitoe rai kwamba sekta binafsi ilete mpango mahsusi kuhusu namna ambavyo itaunga mkono mipango na mikakati ya Serikali ikiwa ni pamoja na kutengeneza ajira milioni nane katika kipindi cha miaka mitano,"- Waziri Mkuu.

Na mimi nitoe rai kwa serikali na watendaji wake.Katika uchumi wa soko hurua sekta binafsi inaongozwa na mahitaji ya soko la bidhaa au huduma zao pamoja na mazingira wezeshi ya kufanya biashara.

Hata siku moja wafanyabiashara wasije kuwadanganya kwamba wanafanya wanayofanya ili kuunga mkono mipango na mikakati ya serikali yenu au kwa sababu ni wazalendo. Wanachotazama ni fursa na faida tu, hakuna kingine.

Mkitaka sekta binafsi izalishe ajira milioni 8 iwekeeni mazingira wezeshi tu wala hakuna haja ya wao kuwa na mpango mahususi katika uchumi wa soko huria. Nyie serikali ndio mnatakiwa kuwa na mpango mahususi.
 
"Nitoe rai kwamba sekta binafsi ilete mpango mahsusi kuhusu namna ambavyo itaunga mkono mipango na mikakati ya Serikali ikiwa ni pamoja na kutengeneza ajira milioni nane katika kipindi cha miaka mitano,"- Waziri Mkuu.

Na mimi nitoe rai kwa serikali na watendaji wake.Katika uchumi wa soko hurua sekta binafsi inaongozwa na mahitaji ya soko la bidhaa au huduma zao pamoja na mazingira wezeshi ya kufanya biashara.

Hata siku moja wafanyabiashara wasije kuwadanganya kwamba wanafanya wanayofanya ili kuunga mkono mipango na mikakati ya serikali yenu au kwa sababu ni wazalendo. Wanachotazama ni fursa na faida tu, hakuna kingine.

Mkitaka sekta binafsi izalishe ajira milioni 8 iwekeeni mazingira wezeshi tu wala hakuna haja ya wao kuwa na mpango mahususi katika uchumi wa soko huria. Nyie serikali ndio mnatakiwa kuwa na mpango mahususi.
WELL SAID
 
Back
Top Bottom