Bikirajohola
JF-Expert Member
- Jun 11, 2022
- 356
- 632
Ndiyo sifa zote za serikali za kifisadi duniani huwa hazina uwezo wa kukusanya kodi kutoka kwa matajiri ,hivyo hukimbilia kuwatoza kodi za hovyo watu masikini.
Tunatambua makusanyo ya kodi ni lazima kwa kila mwananchi ili kuleta maendeleo ya taifa ila kinachoonekana ni kuwa watawala wanafanya ufahari na kuishi maisha ya isirafu bila kujali, wanatembelea magari ya bei ghali, kulipana mishahara mikubwa na posho za kuzidi kiwango, kupeana incentives kiasi kwamba hawajali kabisa na kutambua kuwa upande wa pili wa shilingi Watanzania wanaoogelea kwenye tope la umaskini.
Mikopo ni karibia kila week sasa kuna mkopo mpya unatangazwa wa mabilioni kama si matrillion ya fedha ila bado wananchi tunakamuliwa vilivyo. Maendeleo yanayomgusa mwananchi yako wapi? Maboresho ya huduma za kumpa unafuu mwananchi mbona hatuyaoni? Kama mtu anaweza akafia hospitali sababu tu Network ya NHIF iko down mna sababu gani ya kuendelea kukamua kodi kwa wananchi?
Miradi haimaliziwi, kazi ya kutengeneza mikataba mipya ya kudokoa 10% ndio inaonekana kushika hatamu awamu hii. Tulishayasahau haya kwanini tunarudishana nyuma?
Hilo ndilo ambalo wananchi waliwatuma huko serikalini? Bila aibu wala soni mnasifia ubadhirifu wa fedha za kodi zetu kwa kuhonga wapinzani na kupalilia udokozi kwa kuita "Kulamba Asali". Hii ni zaidi ya dharau jamani.
Mmeanzisha tozo za miamala juu ya 18% VAT ambayo ilikuwa inachajiwa awali ila bado hamjaridhika..Sahizi mnataka mlete tozo kwenye ving'amuzi. Tupeni basi mchanganuo wa hizo tozo mnazokusanya. Mlidai zinajenga mashule hizo shule hazijaisha tu kwa mabilion mliokwisha kusanya kwa mwaka mzima?
Mmeleta tozo kwenye luku hizo pesa zote zinaenda wapi na mtaani hela hakuna? Huduma za kijamii mbovu kabisa. Toeni malengo na utekelezaji wa kila senti ambayo imekusanywa kwenye tozo za awali kwanini mnaficha ripoti za makusanyo na matumizi?
Msituchukulie poa jamani hii hali inachosha kiukweli tunapoenda watu wanaweza wakawa mbogo tukavuruga ule urithi aliotuachia hayati baba wetu wa Taifa.
Tunatambua makusanyo ya kodi ni lazima kwa kila mwananchi ili kuleta maendeleo ya taifa ila kinachoonekana ni kuwa watawala wanafanya ufahari na kuishi maisha ya isirafu bila kujali, wanatembelea magari ya bei ghali, kulipana mishahara mikubwa na posho za kuzidi kiwango, kupeana incentives kiasi kwamba hawajali kabisa na kutambua kuwa upande wa pili wa shilingi Watanzania wanaoogelea kwenye tope la umaskini.
Mikopo ni karibia kila week sasa kuna mkopo mpya unatangazwa wa mabilioni kama si matrillion ya fedha ila bado wananchi tunakamuliwa vilivyo. Maendeleo yanayomgusa mwananchi yako wapi? Maboresho ya huduma za kumpa unafuu mwananchi mbona hatuyaoni? Kama mtu anaweza akafia hospitali sababu tu Network ya NHIF iko down mna sababu gani ya kuendelea kukamua kodi kwa wananchi?
Miradi haimaliziwi, kazi ya kutengeneza mikataba mipya ya kudokoa 10% ndio inaonekana kushika hatamu awamu hii. Tulishayasahau haya kwanini tunarudishana nyuma?
Hilo ndilo ambalo wananchi waliwatuma huko serikalini? Bila aibu wala soni mnasifia ubadhirifu wa fedha za kodi zetu kwa kuhonga wapinzani na kupalilia udokozi kwa kuita "Kulamba Asali". Hii ni zaidi ya dharau jamani.
Mmeanzisha tozo za miamala juu ya 18% VAT ambayo ilikuwa inachajiwa awali ila bado hamjaridhika..Sahizi mnataka mlete tozo kwenye ving'amuzi. Tupeni basi mchanganuo wa hizo tozo mnazokusanya. Mlidai zinajenga mashule hizo shule hazijaisha tu kwa mabilion mliokwisha kusanya kwa mwaka mzima?
Mmeleta tozo kwenye luku hizo pesa zote zinaenda wapi na mtaani hela hakuna? Huduma za kijamii mbovu kabisa. Toeni malengo na utekelezaji wa kila senti ambayo imekusanywa kwenye tozo za awali kwanini mnaficha ripoti za makusanyo na matumizi?
Msituchukulie poa jamani hii hali inachosha kiukweli tunapoenda watu wanaweza wakawa mbogo tukavuruga ule urithi aliotuachia hayati baba wetu wa Taifa.