Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Wapendwa wanaJF, katika Mkutano wa 16, Kikao cha 44 cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania cha tarehe 1 Agosti, 2009, Spika wa Bunge hilo, Mh Samweli Sitt aliiomba Serikali ihakikishe kwamba suala la Richmond Development Company LLC liwe limefikia mwisho kabla ya kumalizika kwa mwaka huu. "Waheshimiwa Wabunge, sasa imefika hatua Kamati ya Uongozi iliamua kwambasuala hili la RICHMOND tulimalize mwaka huu lisiwe linaendelea kama mengine. Kwahiyo, nilimwandikia Mheshimiwa Waziri Mkuu nikiweka wazi kwamba tunahitaji kwa faida ya Taifa letu jambo hili tuliweke mwisho. Serikali ilete maelezo kwamba mmefikia wapi sasa na hayo mnayotujibu yaturidhishe kwamba ndiyo utekelezaji wa yale tuliyoazimia." Alisema Spika Sita.