Serikali isimamie kutoa fidia kwa wale wanaotoa ardhi kwa ajili ya maendeleo, watu wanalia sana

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,138
Binafsi naiamini na kuiomba Serikali ya sasa jinsi inavyosimamia maendeleo kadhaa isimamie pale wananchi wanapolipwa pesa zao kwa kutoa ardhi kwa ajili ya serikali. Hili naamanisha ama inapovunja nyumba ama kuchukua sehemu ambayo wana haki ya kulipwa. Nimeona wengi wakiteseka hasa wanaposema tumelipa hela.

Wapo wasio waaminifu chini huanza kuleta chokochoko ili Wananchi walio na muamala mkubwa wawakatie mshiko ndipo wapewe haki zao. Wapo waliodiriki hata kukamilisha kila kitu pesa zinapotumwa wanaanza kuulizwa mambo mengine ya ajabu ambayo hawakuwahi kuulizwa hapo ni lazima ukate hela upewe chako.

Naomba waziri husika inapotokea swala la kulipa watu vyema ama wewe ama naibu akasimamia pia akishirikiana na wahusika walioathirika waweze kupata haki zao.

kidumu chama cha mapinduzi
zidumu fikra za mwenyekiti

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI
GODBLESS U
#CCMTANOTENA
#DKJPMTANOTENA
 
Back
Top Bottom