Serikali isaidie kampuni za wazawa walau miradi ya 2.5B kushuka ifanye wazawa tu

Myahudi Jr II

JF-Expert Member
Jan 7, 2016
6,703
8,481
Naandika haya nikiwa na huzuni kubwa sana Moyoni huku nikiona kabisa hakuna “future” yoyote kwa makampuni ya wazawa na ma engineer wetu(civili) wanaozalishwa kila siku kwenye vyuo vyetu vya ndani.

Ndugu zangu nikiwa kama mdau wa sector ya Ujenzi based kwenye majengo (Building Constructions) napenda niseme neno moja tu walau SERIKALI ilisikie isaidie wahandisi wazawa na kampuni zetu za ndani za Ujenzi ili nazo zikue.Kwanza kabisa napenda nipongeze wote wenye kampuni Class 1-3 maana si lele mama kumiliki hizo class inaonyesha kuna kazi ya ziada imefanyika sana, hongereni.

Ndani ya nchi yetu sasa kuna utitiri wa kampuni za wageni hasa wachina, wamekuja kuua soko kabisa la kampuni zetu za ndani, nachosema WAMEUA KABISA KAMPUNI ZETU, ni mjinga tu atakaesifia ujio wa utitiri wa kampuni hizo bila kuelewa chochote, nawaomba CRB itoshe basi kampuni za Kichina zilizopo nchini, zimetosha, zimetosha zimetosha. Tunaua makampuni yetu ya wazawa bila kujua, tunaua mainjinia wtu bila kujua, tunapeleka wapi hili taifa la engineers wenye vyeti wasio na ujuzi??

Makampuni ya kichina ukienda nayo kwenye Tendering, usijidanganye kushinda, narudia tena usijidanganye kushida mradi wowote, wale ni vunja bei (atatoke mtu hapa atasema mlizoea wizi na Magufuli anawakomesha, Usamehewe in advance), sitaki kusema sanaaa maana wanajua wanachofanya kufidia hasara ya hiyo vunja bei, ndio maana ukifanya kazi na mchina 24/7 unatakiwa uwe nae mgongoni ukilala kidogo tu UMEUMIA.
Hizi kampuni za Kichina nyingii sana ni za serikali yao yaan 70% ya serikali huku 30% ya mtu binafsi kwa hiyo wao hawalipi mishahara bali serikali yao ndio inalipa wafanyakazi, equipments zoote ni serikali ndio ina facilitate, pia huwezi kukuta mchina hana equipments wanaazimana maana ni mali ya serikali yaani yeye haangaiki chochote.

Pili hawa jamaa unaweza ukakuta wamebid hata kampuni 3 mradi mmoja usidhani ni wajinga wale, yaani hapo ni mmoja ila kampuni tofauti tu na lazima mmoja apate huku wazawa wanapigwa chini, INAUMIZA SANA.

Naiomba serikali isaidie wazawa hata miradi ya 2.5billions kushuka chini iwe inafanya wazawa tu tuinue kampuni zetu na watoto wetu wapate ajira humo nasema hivo kwa kua mradi wa 2billions mchina atakuta amebid kwa 1.3b wakati lowest bidder wa kibongo ana 1.6b, jamani huyu analipa mishahara, ofisi, mitambo, etc etc akishuka zaidi ni majanga sana, hawezi shindana na mtu aambae anasaidiwa na serikali yake
Naweza nikawa nisiwe mzuri kuwasilisha hoja zangu ila naomba niwasilishe hivo hivo
 
Wazawa kina nani? Hao Delmonte Nyanza Nyakirang"anyi wametufikisha wapi? Wazawa tuwe na "nidhamu" katika kutafuta kazi hasa kwenye kubid na kutekeleza miradi.. Unadhani kwanini Estim anaendelea
 
Wazawa kina nani? Hao Delmonte Nyanza Nyakirang"anyi wametufikisha wapi? Wazawa tuwe na "nidhamu" katika kutafuta kazi hasa kwenye kubid na kutekeleza miradi.. Unadhani kwanini Estim anaendelea

Huyo Estim unaemtaja anapumulia mashine sasa hivi, rudi miaka 5 nyuma miradi aliokua nayo estim na sasa hivi hali ikoje
 
Ulichokizungumza ndugu ni kweli tupu, niongeze jambo hapo kwa macho ndogo. Hawa jamaa tunavyowaona huku wengi wao ni wafungwa ila ni wataalamu wa sekta hizo wanazofanyia kazi na wanaifanyia kazi serikali hivyo wao hawana cha kudai tofauti na posho wanazolipwa. Hakuna maendeleo yatafanyika kwako kwa kumtegemea jirani! Lazima wewe mwenyewe uhusike kuyajenga
 
Kuna kikao cha tender niliwahi kuhudhuria, kampuni za kichina zilikua 3, wao hata swali hawakuuliza tena hawana mbwembwe kwenye vikao ila mwisho wa siku anapata tender

Sent using Jamii Forums mobile app

Ukweli ni kwamba huwezi kushindana na mchina kwenye attachements za bid, atakushinda tu kuanzia equipments na kila kitu, na wao wanajua kuna wabongo wako very well kwenye attachements mchina yeye anavunja bei
 
Ulichokizungumza ndugu ni kweli tupu, niongeze jambo hapo kwa macho ndogo. Hawa jamaa tunavyowaona huku wengi wao ni wafungwa ila ni wataalamu wa sekta hizo wanazofanyia kazi na wanaifanyia kazi serikali hivyo wao hawana cha kudai tofauti na posho wanazolipwa. Hakuna maendeleo yatafanyika kwako kwa kumtegemea jirani! Lazima wewe mwenyewe uhusike kuyajenga

Watu ukiwaeleza wanasema tupo shallow wabongo
 
Kampuni zao mara nyingi hua wanaweka bei ndogo sana, kiasi kwamba anakua hana mpinzani kingine wale jamaa hawalipi kodi kuagiza vitu kwao hivyo inakua nafuu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sasa kama ni hivyo kwanini asipewe kazi mzawa ambae tutafaidika nae?? ila kuna mahali tunashindwa sio sisi bali serikali yetu haiwajali wao wanawaza kupigwa tuuu
 
Kwaio hao wabongo wao wanazo hizo equipments? Ila mara nyingi miradi mingi ya serikali yetu inakua imekopeshwa hela kwaio moja ya sharti la mkopo ni kutumia kampuni za kichina, labda niulize hivi kwa wenye hizo kampuni mlizianzisha ili mpate tenda za serikali au hata tenda za sekta binafsi? Maana huwezi anzisha biashara ukitegemea kupata tenda za serikali
 
Kwaio hao wabongo wao wanazo hizo equipments? Ila mara nyingi miradi mingi ya serikali yetu inakua imekopeshwa hela kwaio moja ya sharti la mkopo ni kutumia kampuni za kichina, labda niulize hivi kwa wenye hizo kampuni mlizianzisha ili mpate tenda za serikali au hata tenda za sekta binafsi? Maana huwezi anzisha biashara ukitegemea kupata tenda za serikali

Chini ya Jua hili linalotoa Mwanga wake kwahabari za ujenzi mwajiri mkuu ni SERIKALI kwa hii Tnzania yetu, Equipments zipo ila zinakodishwa na pesa ya kukodisha inatakiwa itoke humo humo kwwenye pesa za mradi, hivyo kwa kua wachina wao serikali yao inawapa inakua vyepesi zaidi kupata mradi kwa bei ndogo
 
Back
Top Bottom