Serikali iruhusu magari mengine kutumika kama daladala mida ya jioni na usiku mkoani Dar-es-salaam

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,985
Kutokana na adha ya usafiri katika jiji la Dar es salaam hasa kuanzia saa 12 jioni mpaka around saa 3 na saa 4 usiku, nashauri serikali iruhusu magari ambayo yanaweza kubeba abiria(mifano NOAH) yaruhusiwe ili kuondoa mateso na adha kwa abiria.


Ushauri huu ni Kutokana na unwell kuwa katika mida hii, abiria huwa wengi sana vituoni huku daladala zikiwa na capacity ndigo ya kubeba abiria walioko vituoni na hivyo kusababisha watu kugombania magari sometimes karibu ya kuumizana.

Magari yatayokuwa teyari kutumika yanaweza kusajiliwa kwa mashariti na taratibu maalumu kufanya kazi hii.


Option nyingine ni serikali ku-phase out hizi daladala na kuruhusu mabasi makubwa zaidi kutumika kama daladala badala ya kuendelea na hizi daladala zinazoongeza wingi wa magari tu na kuongeza tatizo la foleni jijini Dar es salaam.

Najua wimiliki wa daladala pamoja na madereva na makonda watapinga wazi hili, ill watambue na wao(madereva) wanachangia sana tatizo hili hasa kwa kukatisha root mida ya usiku na kusababisha tatizo kuwa kubwa zaidi.

Tujiongeze.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom