Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,480
- 9,241
Serikali imesema ipo katika mpango wa kupitia utaratibu wa malipo kwa wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu ili wapunguziwe mzigo.
Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano Machi 31, 2021 bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu Omari Kipanga alipokuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalum, Halima Mdee.
Mdee amehoji ni lini Serikali itapeleka bungeni mapendekezo ya sheria ili kuwaondolea mzigo mzito wanaobeba wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu kwani mpango huo umekuwa biashara.
Kwa mujibu wa Mdee Serikali inasema kuwa inawasaidia watoto wa masikini wakati inawaumiza kwa mlolongo wa madeni.
Naibu Waziri amesema tozo zilizotajwa na mbunge huyo hazina uhalisia kwani upo utaratibu mzuri wa namna ya ulipaji mikopo.
Swali la msingi liliulizwa na Atupele Mwakibete na likiibua mjadala mrefu bungeni ambapo wabunge wengi walitaka kuuliza maswali.
Chanzo: Mwananchi
Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano Machi 31, 2021 bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu Omari Kipanga alipokuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalum, Halima Mdee.
Mdee amehoji ni lini Serikali itapeleka bungeni mapendekezo ya sheria ili kuwaondolea mzigo mzito wanaobeba wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu kwani mpango huo umekuwa biashara.
Kwa mujibu wa Mdee Serikali inasema kuwa inawasaidia watoto wa masikini wakati inawaumiza kwa mlolongo wa madeni.
Naibu Waziri amesema tozo zilizotajwa na mbunge huyo hazina uhalisia kwani upo utaratibu mzuri wa namna ya ulipaji mikopo.
Swali la msingi liliulizwa na Atupele Mwakibete na likiibua mjadala mrefu bungeni ambapo wabunge wengi walitaka kuuliza maswali.
Chanzo: Mwananchi