Serikali Ingilieni Huu Ukatili: Hoshi Security Inawanyanyasa vijana wa Kitanzania

Mwingereza

JF-Expert Member
Jan 21, 2014
1,110
2,736
Wanajukwaa, nadhani serikali yetu inabidi iangalie kwa umakini mkubwa haya mambo ya ukatili ndani ya hii nchi. Kuna mambo ya ajabu mno.

Mara kwa mara naenda Mikocheni kumtembelea mchumba wangu anayeishi Mikocheni Baraka Plaza Apartments, na mara nyingi nawakuta vijana wale wale waigwa lindoni. ILa leo ilikuwa tofauti kidogo maana mmoja alikuwa akibubujika machozi. Nililazimika kuingiza gari na kurudi kutaka kujua kulikoni, ndipo nikagundua kwamba, Huyu aliyekuwa akilia alifukuzwa kazi.

Sababu ya kufukuzwa kazi, ni kwa sababu aliomba mshahara wake. Huu ni wezi wa saba tarehe 20, lakini hadi leo hawajalipwa mishahara yao toka mwezi wa sita ya 150,000 (Laki na Nusu) kwa mwezi. Hawa vijana wanakosa hadi nauli wanalizimika kutuembea toka Kimara hadi Mikocheni, wengine wanatokea tegeta, kwa maana hiyo lazima waamke saa 9 usiku kuanza kuttembea ili waripoti kazını saa 1. Hapo hakuna chakula cha mchana wala kifungua kinywa. Wanaokesha nao ni njaa . Pamoja na tabu zote hizo, kosa ni kuomba Mashahara. Wasiongee chochote....!

Kwa pamoja hawa vijana walikaa, wakakubaliana kwamba kiongozi wao atume SMS kwa uongozi kwamba wana hali mbaya na wangeshindwa kuendelea kufanya kazi. Kosa ni hiyo SMS.

Hii kampuni ya ulinzi inaitwa HOSHI Security. Hawa vijana wanalipwa laki na nusu, ila inafika Tarehe 20 hawajalipwa..... Wanakuja kuomba stahiki yao, wanafukuzwa. Nimekuja kuongea na mmoja wa waimiliki wa nyumba, nao wanashangaa, na wamedhamiria kuifikisha hili swala kwa mamlaka.

Mamlaka Tanzania, angalieni huu UKATILI. Kwa nini Watanzania wanyanyaswe kiasi hiki?
 
Hadi hapa bado sijaelewa kwa kuwa hujasema hawajalipwa mshahara wa mwezi gani.
 
Vikampuni vingi hapa Tanzania ndio aina yake ya kufanya biashara hiyo.

hasa hivi vya ulinzi.

at least guardaworld,g4S wanajitambua.
 
Hayo makampuni huwa ya mabos wa polisi au wajeda wakubwa wa staafu kwa ufupi wakikuzungua hauna ujanja sijajua ni katiba inawabeba au haizingatiwi tu
 
Mimi ninefanya sana kazi ya ulinzi kwa miaka 3 sasa.

Hivi mtu unashindwaje kupambania maisha yao mpaka unakuwa mpumbavu hivi?

Mimi siwezi kufanya kazi bila kulipwa. Mshahara ukivuka tu 10 siendi kazini.

Na mara nyingi watu wa hivi huwa hawana vyeti vya kidato cha nne.

Mimi nawashauri wakatafute kazi G1 Security au Simplisafe huko
wanajitahidi kulipa kwa wakati.

Unakuwa msukule kwenye kampuni moja kwani umeambiwa ukiacha kazi hapo unakufa ?

Hapa unaweza kujifanya unawatetea kumbe hata hawana mikataba yoyote ya kikazi.
 
Haya makampuni ya ulinzi ni wanyonyají balaa. Miaka ya 1995 mpaka 2000 nilikuwa na mlinzi wa kampuni fulani hapa Dodoma na huko Dar, nilichokishuhudia, nilliamua kutafuta walinzi binafsi badala ya kampuni.
 
Biashara ngumu mkuu, hata mwenye kampuni anafanya kudunduliza Kwa kusubilia wataje wake walipe. Hivi vikampuni local havina huwezo wa kulipa bila kusuburi wateja walipe Kwanza. Yako mengi siyo hiyo Tu.
 
Wanajukwaa, nadhani serikali yetu inabidi iangalie kwa umakini mkubwa haya mambo ya ukatili ndani ya hii nchi. Kuna mambo ya ajabu mno.

Mara kwa mara naenda Mikocheni kumtembelea mchumba wangu anayeishi Mikocheni Baraka Plaza Apartments, na mara nyingi nawakuta vijana wale wale waigwa lindoni. ILa leo ilikuwa tofauti kidogo maana mmoja alikuwa akibubujika machozi. Nililazimika kuingiza gari na kurudi kutaka kujua kulikoni, ndipo nikagundua kwamba, Huyu aliyekuwa akilia alifukuzwa kazi.

Sababu ya kufukuzwa kazi, ni kwa sababu aliomba mshahara wake. Huu ni wezi wa saba tarehe 20, lakini hadi leo hawajalipwa mishahara yao toka mwezi wa sita ya 150,000 (Laki na Nusu) kwa mwezi. Hawa vijana wanakosa hadi nauli wanalizimika kutuembea toka Kimara hadi Mikocheni, wengine wanatokea tegeta, kwa maana hiyo lazima waamke saa 9 usiku kuanza kuttembea ili waripoti kazını saa 1. Hapo hakuna chakula cha mchana wala kifungua kinywa. Wanaokesha nao ni njaa . Pamoja na tabu zote hizo, kosa ni kuomba Mashahara. Wasiongee chochote....!

Kwa pamoja hawa vijana walikaa, wakakubaliana kwamba kiongozi wao atume SMS kwa uongozi kwamba wana hali mbaya na wangeshindwa kuendelea kufanya kazi. Kosa ni hiyo SMS.

Hii kampuni ya ulinzi inaitwa HOSHI Security. Hawa vijana wanalipwa laki na nusu, ila inafika Tarehe 20 hawajalipwa..... Wanakuja kuomba stahiki yao, wanafukuzwa. Nimekuja kuongea na mmoja wa waimiliki wa nyumba, nao wanashangaa, na wamedhamiria kuifikisha hili swala kwa mamlaka.

Mamlaka Tanzania, angalieni huu UKATILI. Kwa nini Watanzania wanyanyaswe kiasi hiki?
Hoshi Security & Detective Pvt Ltd
5.0 (4) · Security guard service
New Delhi, Delhi, India
Open ⋅ Closes 8PM

Hoshi Guards Private Limited
3.8 (8) · Security guard service
New Delhi, Delhi, India · +91 11 2636 4155
Open now
 
Mbona ni kama ww huyo mlinzi
Ni yeye lakini unajua hapa ni jukwaa sasa pot kaona atumie undercover technique kupata info, alafu kachimba mkwara eti huwa anaenda Kwa demu wake, alafu anasema baada ya kupack gari...... Mlinzi aliyefukuzwa siyo rahisi arudi Lindo analofanyia kazi na kupata access ya kuingia ndani.
 
Vikampuni vingi hapa Tanzania ndio aina yake ya kufanya biashara hiyo.

hasa hivi vya ulinzi.

at least guardaworld,g4S wanajitambua.
Yeah sijui kwa nini hata sisi tumeajiri walinzi wa kutosha kutoka kampuni fulani,mshahara wao tunapeleka tarehe 2 ya kila mwezi ila wao wanawalipa kuanzia tarehe 10 na zaid
 
Yeah sijui kwa nini hata sisi tumeajiri walinzi wa kutosha kutoka kampuni fulani,mshahara wao tunapeleka tarehe 2 ya kila mwezi ila wao wanawalipa kuanzia tarehe 10 na zaid
Mpaka hapo haujaona kuwa tatizo ni wewe kama unapeleka malipo ya kazi ya mlinzi trh 2 unatarajia mwajiri wake atamlipa tarehe ngapi? Mimi Nina kampuni zaidi ya tatu ikiwemo taasisi ya kiserikali ambayo nayo inatoa huduma kwetu na malipo huwa tunafanya tarehe kumi na nane ( 18) kila mwezi ili nao wapate muda wa kuwalipa staff wao. Labda wao ndo wachelewe kuleta invoice lakini wakileta Kwa wakati malipo yetu huwa hayavuki trh 20, na Nina hakikisha walinzi wamelipwa ifikapo trh 30, kinyume na hapo lazima nivaane na service provider. Kwa sababu kadili mishahara inavochelewa walinzi hupoteza morali. Tatizo ni kwamba hizi kampuni ndogo zinalinda maskini ambao hawezi kulipa gharama ya laki 8 mpka milioni moja plus Kwa mlinzi. Hawa ni aina ya wateja ambao wanachukuwa vikampuni vile vinavotoza laki 3 kama gharama ya ulinzi. Akitarajia kumlipa mlinzi laki na nusu ili abaki na laki pia kama hela ya kampuni
 
Mpaka hapo haujaona kuwa tatizo ni wewe kama unapeleka malipo ya kazi ya mlinzi trh 2 unatarajia mwajiri wake atamlipa tarehe ngapi? Mimi Nina kampuni zaidi ya tatu ikiwemo taasisi ya kiserikali ambayo nayo inatoa huduma kwetu na malipo huwa tunafanya tarehe kumi na nane ( 18) kila mwezi ili nao wapate muda wa kuwalipa staff wao. Labda wao ndo wachelewe kuleta invoice lakini wakileta Kwa wakati malipo yetu huwa hayavuki trh 20, na Nina hakikisha walinzi wamelipwa ifikapo trh 30, kinyume na hapo lazima nivaane na service provider. Kwa sababu kadili mishahara inavochelewa walinzi hupoteza morali. Tatizo ni kwamba hizi kampuni ndogo zinalinda maskini ambao hawezi kulipa gharama ya laki 8 mpka milioni moja plus Kwa mlinzi. Hawa ni aina ya wateja ambao wanachukuwa vikampuni vile vinavotoza laki 3 kama gharama ya ulinzi. Akitarajia kumlipa mlinzi laki na nusu ili abaki na laki pia kama hela ya kampuni
Huu ni utaratbu wetu wa malipo na hatujawahi ongeza tarehe au kupunguza labda tungekuwa tunalipa kwa kusuasua ndo ungesema tunawachelewesha point yangu hela tangu tarehe2 mpaka 10 na zaidi inakuwa inasubiri nini?
 
Back
Top Bottom