Serikali ingepata Sh3.2 Billion kama ingeliweza kurudisha mjusi wake!

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,377
58,384
Serikali ya Tanzania inapoteza fedha nyingi kila mwaka kwa kutokuwa na ujasiri wa kumrudisha mjusi aliyepelekwa ujerumani mwaka 1918.

Pamoja na mapato hayo kila mwaka watalii wapatao 500,000 wanaotembelea makumbusho hayo wangeweza kuitembelea Tanzania,kujionea mabaki ya mjusi huyo aliyetokea kusini mwa Tanzania.Maelezo hayo yalitolewa na Membe bungeni,alisema mjusi huyo mwenye urefu wa mita 22,na uzito wa tani 250 amekuwa kivutio kikubwa ujerumani,alisema mchakato wa kumrudisha sio kazi rahisi kwa sababu wajerumani bado hawajaonyesha nia ya kufanya hivyo:

My take;Serikali inashindwa nini kurudisha mabaki ya huyu mjusi(dinosour),ilihali waliweza kurudisha fuvu la Mkwawa?
 
Huu ni ukoloni na ikibidi hata walipe,wamekaa naye mda mrefv sana.
 
kuna siku nilipata bahati ya ku over heard maongezi ya wadau fulani toka makumbusho ya taifa, ni kwamba tatizo linalo kwamisha mjusi huyu kurudishwa ni facilities za kumuweka, maana urefu wake sio mchezo, kwa sasa makumbusho ya taifa hawana jengo lenye uwezo wa kumifadhi mjusi huyo, maana urefu wake kwenda juu ni kama au zaidi ya ghorofa tatu.

napia mtaalamu na fedha za kumsafirisha na kumassemble pia ni ishu..,
 
kuna siku nilipata bahati ya ku over heard maongezi ya wadau fulani toka makumbusho ya taifa, ni kwamba tatizo linalo kwamisha mjusi huyu kurudishwa ni facilities za kumuweka, maana urefu wake sio mchezo, kwa sasa makumbusho ya taifa hawana jengo lenye uwezo wa kumifadhi mjusi huyo, maana urefu wake kwenda juu ni kama au zaidi ya ghorofa tatu.

napia mtaalamu na fedha za kumsafirisha na kumassemble pia ni ishu..,

unajua wizara inaingiza kiasi gani kwa mwaka?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom