Serikali inayobadilisha maamuzi yake kwa kutegemea upepo ni Serikali dhaifu, haifai

Kwamba itakuwa nchi ya kila kitu kitajijua? Bonge la swali.

Nchi ina watu milioni 60, walipa kodi rasmi idadi yao haifiki hata milioni 10 (na walio wengi kati ya hao ni wafanyakazi wanaokatwa over 30% ya mshahara wao kila mwezi kwa kodi tu PAYE).

Then kodi ya miamala ingewagusa walau hao wengine ambao kiukweli ndio walio wengi, but hawajulikani katika vitabu vya kodi vya serikali lakini wanawajibika pia katika kuijenga nchi yao.

Tusitake kuitana majina yasiyo na sababu za msingi, eti watanzania wa chini. Hakuna cha mtanzania wa chini au wa juu wote ni watanzania na hii nchi tuliambiwa ni nchi ya kijamaa.

Hapa kinachokosekana ni kiongozi wa kujenga hoja za ushawishi na kusisimua ili hii kodi ionekane ya kawaida, ya lazima na ya kuleta mabadiliko.
Mwendazake Sikuwahi kumkubali ila kwenye kusimamia maamuzi aliyoamini alikuwa poa.

Sasa tumekosa kiongozi shupavu haiingii akilini unashindwa kusimamia maamuzi,udhaifu mkubwa huu.
 
"Tunataka mambo makubwa wakati hatujakenga miundo mbinu ya kuyafikia hayo makubwa."

JPM alipokuwa akitumia muda mwingi akitetea miradi yake ya miundombinu mlikuwa mnasemaje?

Si mlikuwa mkipiga kelele oh maendeleo ni watu sio vitu?

Sasa nakushangaa leo unasema tena kwamba miundombinu ni muhimu kuyafikia hayo maendeleo. Duh!

Ni hivi hakuna kitu ambacho kiongozi yeyote atafanya/atatekeleza asipigiwe makelele. Mimi namtaka kiongozi anayeamini kwamba kile anachokifanya ni sahihi na awe tayari kukitetea kwa kauli na kwa matendo. Walipokuwa wanaweka hizo kodi walikuwa hawana maono ya nini wanataka kufanya kwa kupitia kodi?
Kwani nikisema miundo mbinu wewe unaelekeza akili kwenye barabara na reli?

Kaa tuliza kichwa utanielewa
 
Mwendazake Sikuwahi kumkubali ila kwenye kusimamia maamuzi aliyoamini alikuwa poa.

Sasa tumekosa kiongozi shupavu haiingii akilini unashindwa kusimamia maamuzi,udhaifu mkubwa huu.
Hakuna jambo zuri or baya 100%, misimamo ni mizuri lakini lazima kushirikisha bongo pia, angalia alivyohandle issue ya corona! So kila aina ya uongozi/utawala una pande chanya na hasi pia! Muhimu hasi zisizidi sana chanya
 
Hizo tozo ni mzigo kulingana na hali ya uchumi wa mtu mmoja mmoja.

Pili sio kupenda kwao. Miamala imeshaanza kudorola imebidi washtuke maana kinachoenda kutokea ni wao kukosa hata kile kidogo walichokua wanakipata kupitia VAT ya ada za miamala

Hivi unadhani kama mzunguko wa miamala ungekua kama zamani wangejari kelele? Si unakumbuka juzi tu mwigulu alisema tutazoea tu? Unafikiri alikurupuka? Alisema kutoka moyoni kuonyesha they don't care hata tukilalamika.....

Ngoma imenoga watu wamegoma kuweka hela ambayo inakatwa mpaka kichwa kinauma. Hela yenyewe unaipata kwa mbinde
The thing is Mwigulu hakuwa mtu sahihi kuzungumzia umuhimu wa kodi hiyo.

Hiyo kodi ni mpya, na hiyo kodi ndio ilikuwa fursa ya mama kutengeneza maono yake na kujibrand kwa watanzania. Huu ndio mwaka mpya wa fedha unaoanza na mama akiwa top na angetumia fursa hii kuja na speech kabambe ya kuimarket hiyo kodi na kuwaaminisha watanzania kwamba zama zimebadilika, ulimwengu umebadilika na nchi yetu imebadilika pia. Angetumia fursa hiyo pia kujiweka kwamba yeye kama mkuu wa serikali ana nia ya kuongeza kasi ya maendeleo ya nchi yetu kwa namna jumuishi lakini yenye ahadi ya kuleta maendeleo jumuishi. Ndio maana amekuja na hii kodi.

Jambo kubwa kama lile anatutumia Mwigulu......!

If you cant be serious kwenye mambo serious watu hawawezi kukuchukulia serious pia, na ndio maana watu wakambeep kupitia kusuasua kwa transactions za mpesa. Naye naona kashabipika. Yote kati ya yoye it matters who says it and how it is being said.
 
The thing is Mwigulu hakuwa mtu sahihi kuzungumzia umuhimu wa kodi hiyo.

Hiyo kodi ni mpya, na hiyo kodi ndio ilikuwa fursa ya mama kutengeneza maono yake na kujibrand kwa watanzania. Huu ndio mwaka mpya wa fedha unaoanza na mama akiwa top na angetumia fursa hii kuja na speech kabambe ya kuimarket hiyo kodi na kuwaaminisha watanzania kwamba zama zimebadilika, ulimwengu umebadilika na nchi yetu imebadilika pia. Angetumia fursa hiyo pia kujiweka kwamba yeye kama mkuu wa serikali ana nia ya kuongeza kasi ya maendeleo ya nchi yetu kwa namna jumuishi lakini yenye ahadi ya kuleta maendeleo jumuishi. Ndio maana amekuja na hii kodi.

Jambo kubwa kama lile anatutumia Mwigulu......!
Tamaa za kutaka hela nyingi kwa wakati mmoja ndio chanzo cha kukosa kabisa. Hebu jiulize, ada ya kutuma Tsh 45,000 ni Tsh 410 ambayo inakatwa na mtandao husika. Serikali imeongeza Tsh 1,500 na kufanya iwe Tsh 1,910. Hilo ni ongezeko la zaidi ya 300%

Kwanini hapo wasingeongeza japo Tsh 90 ili iwe Tsh 500 kwa ujumla. Yaani inakua ni reasonable kwa watumia huduma. Hapo bado kwenye kutoa. Hivi unadhani kuna hela ya kuchezea kiasi hicho wakati hali zenyewe ni ngumu ki-uhalisia
 
Tamaa za kutaka hela nyingi kwa wakati mmoja ndio chanzo cha kukosa kabisa. Hebu jiulize, ada ya kutuma Tsh 45,000 ni Tsh 410 ambayo inakatwa na mtandao husika. Serikali imeongeza Tsh 1,500 na kufanya iwe Tsh 1,910. Hilo ni ongezeko la zaidi ya 300%

Kwanini hapo wasingeongeza japo Tsh 90 ili iwe Tsh 500 kwa ujumla. Yaani inakua ni reasonable kwa watumia huduma. Hapo bado kwenye kutoa. Hivi unadhani kuna hela ya kuchezea kiasi hicho wakati hali zenyewe ni ngumu ki-uhalisia
Hiyo hela si kubwa kihivyo na si kweli kwamba haimuduki.

Hawatetea ipasavyo hizo charges.
 
Hiyo hela si kubwa kihivyo na si kweli kwamba haimuduki.

Hawatetea ipasavyo hizo charges.
Sio kubwa??? Kwa mwenye nayo hiyo hela sio kubwa. Kwa mimi ninayelipwa 4000 kwa siku ni kubwa sana hiyo. Maana unayemtumia ili atoe inatakiwa awe na Tsh 3,850 ya ziada.

Maana yake ukiwa na Tsh 45,000 ukimtumia mtu mpaka kuitoa ni Tsh 39,000....

Sasa nini faida hapo kwa mtumiaji wa huduma hiyo? Yaani 6,000 nzima sio yako tena
 
Hakuna jambo zuri or baya 100%, misimamo ni mizuri lakini lazima kushirikisha bongo pia, angalia alivyohandle issue ya corona! So kila aina ya uongozi/utawala una pande chanya na hasi pia! Muhimu hasi zisizidi sana chanya
Ngoja tuone nyie mnaoshirikisha bongo kama mtakusanya mapato ya kutosha na kutatua changamoto za maendeleo,bahati nzuri saizi si TRA wala halmashauri wanaosisitiza kukusanya mapato ya serikali .Wafanyabiashara na wananchi wanakwepa kodi.Nasubiri nione matokeo ya serikali sikivu
 
Ngoja tuone nyie mnaoshirikisha bongo kama mtakusanya mapato ya kutosha na kutatua changamoto za maendeleo,bahati nzuri saizi si TRA wala halmashauri wanaosisitiza kukusanya mapato ya serikali .Wafanyabiashara na wananchi wanakwepa kodi.Nasubiri nione matokeo ya serikali sikivu
Hizo changamoto ziliwahi kutatuliwa lini? Watu walikalishwa benchi miaka 5, no ajira mpya, no kupandishwa madaraja, no ongezeko la mishahara. Makato ya bodi yakaongezwa kutoka 8% to 15% bila kufuata mkataba, deni la taifa likaongezeka zaidi ya 15 trilions, hamna barabara mpya ya maana imejengwa zaidi ya zile alizoacha jk.

Hela zikakwapuliwa kutoka kwenye accounts za watu, TRA wakawa wanalazimishwa kupika data za mapato, hela za maendeleo kwenye halmashauri na manispaa zikawa hazipelekwi! Nchi imeongozwa kwa propaganda kwa miaka 5, now kila kitu kitakuwa wazi! Tutademka na kutukana sana tu, lakini ndiyo afya ya taifa hiyo!!
 
Chadema 2010 ilipata viti vingi vya ubunge bungeni, kwasbb ya udhaifu wa mkwele katika hoja ya ufisadi, Richmond, IPTL, mwisho wa siku wananchi wakapatwa na hasira na kuihamini Chadema.

Kwa hiyo hata hoja hii ya Tozo na inaweza mende akaangusha kabati.
Na kama sio goli la mkono 2015 Sasa hivi tungekua tunaongea habari nyingine
 
Tulipompigia kelele JK kuhusu safari zake hadi tukamwita Vasco da Gama, serikali yake iliondolewa?

Mlipompigia kelele JPM kuhusu kile mlichokuwa mnakiita udkiteta serikali yake iliondolewa?

Ni kawaida ya raia kutoridhika, uongozi ni kujenga hoja na kuwashawishi watu kwamba maamuzi yako ni sahihi.

Urais ni mgumu, na usipokuwa na uthabiti wa maamuzi hiyo kazi haikufai.
Mkuu hebu tumia akili kidogo ziara za JK hazikuwa zikiwaguza watu wa vijijini moja kwa moja..ila hili la tozo liliwaguza hadi mafukara wa chini kabisa.. linapokuja suala la kukamua wananchi direct linaweza kuiyumbisha Serikali sio umesikia watu wameacha kutumia simu kutuma fedha kwa mamilioni ndani ya siku tatu tu..watu wamegomea maana yake hilo lengo la kupata hizo fedha limeshakufa
 
Chadema 2010 ilipata viti vingi vya ubunge bungeni, kwasbb ya udhaifu wa mkwele katika hoja ya ufisadi, Richmond, IPTL, mwisho wa siku wananchi wakapatwa na hasira na kuihamini Chadema.

Kwa hiyo hata hoja hii ya Tozo na inaweza mende akaangusha kabati.
Kwani chadema ni raia kutoka Urusi? hawana haki ya kuchaguliwa acha akili za kizeee
 
Hizo changamoto ziliwahi kutatuliwa lini? Watu walikalishwa benchi miaka 5, no ajira mpya, no kupandishwa madaraja, no ongezeko la mishahara. Makato ya bodi yakaongezwa kutoka 8% to 15% bila kufuata mkataba, deni la taifa likaongezeka zaidi ya 15 trilions, hamna barabara mpya ya maana imejengwa zaidi ya zile alizoacha jk. Hela zikakwapuliwa kutoka kwenye accounts za watu, TRA wakawa wanalazimishwa kupika data za mapato, hela za maendeleo kwenye halmashauri na manispaa zikawa hazipelekwi! Nchi imeongozwa kwa propaganda kwa miaka 5, now kila kitu kitakuwa wazi! Tutademka na kutukana sana tu, lakini ndiyo afya ya taifa hiyo!!
Hivyo unavyovitaja utatatua kwa kutumia makalio yako au pesa? Maamuzi ya kijinga kama haya ya kuwasikiliza walalamishi,wakulaumu kama wewe na wajuaji wengine wasio na suluhisho ndio vimefanya tuendelee kuwa na changamoto zisizopungua miaka na mikaka.
 
Kwani ukitumia benki kuna shida gani? Cha msingi lazima serikali iwe na msimamo,upuuzi kama huu ndio unatufanya miaka 60 ya uhuru shule zinahangaika na vyoo, watoto wanarundikana hovyo madarasani afu Hali ya maisha Vijijini inazidi kuwa mbaya huku nyie wa mjini mnadwmka tuu eti tozo kubwa .
Unadhani hizo kodi mwigulu alizozipendekeza ndo zitatatua hizo changamoto unajidanganya sana
 
Hivyo unavyovitaja utatatua kwa kutumia makalio yako au pesa? Maamuzi ya kijinga kama haya ya kuwasikiliza walalamishi,wakulaumu kama wewe na wajuaji wengine wasio na suluhisho ndio vimefanya tuendelee kuwa na changamoto zisizopungua miaka na mikaka.
Huwa unatumia makalio kutatua changamoto? Unataka ufanye upupu and watu wasilalamike? Acha ujinga
 
Mbona hujaacha Kazi sasa kama haikulipi? Picha gani ya kuisoma? Huko mtaani unaishi peke yako au wakala ni wewe peke yako?

Kwamba nikitoa 130,000 nikakatwa 6180 nitakuwa nimeathirika Sana na hiyo unayoita Hali halisi ya maisha?

Mbona hao wanaowapa commission sijawahi kukusikia ukitetea wananchi kwamba mnakata wateja pesa nyingi? Kampuni inapata 3650 na Serikali 2530 ,hapo nani anafaidika Kati ya Serikali na Kampuni?

Kama serikali inakubali kusalimu amri basi na huo wizi wa kampuni za simu Ili kulipa mawakala wao ukome.
Then nani atalipa mawakala?
 
Sio ilo tu misimamo ya JPM ilikuwa yakibabe! Hivi ingekuwaje Serikali kama ndiyo ya Samia ingejenga Bwawa la Umeme pale Rufiji na zengwe lote lile? Serikali ya Samia ndo ingekuwa madarakani kipindi corona inaingia umewahi kuwaza tungechezea lockdown mpaka tuishe wote!

Samia hana ubavu wa kukabiliana na pressure sio za nje tu ata ndani ya nchi
Jiwe hakufaa kuongoza hata familia yake na ndiyo maana ilimshinda na Sir God akaingilia kati, hiyo corona ndiyo imepita naye kwa sababu ya kushupaza shingo
 
Nchi za Scandnavia ndizo zinazoongoza kwa kulipa kodi. Kule mtu anapigwa kodi hadi utabaki unashangaa.

Cha kushangaza zaidi wananchi wanafurahia utaratibu wao huo wa kodi kubwa. Kwa nini?

Kwa sababu kila raia anapata huduma ya afya first class bila kujali kipato chao.

Kwa sababu barabara zao ni za kiwango cha lami cha kwanza kuanzia mjini hadi vijijini.

Kwa sababu kila raia ana fursa ya kupata elimu hadi chuo kikuu kwa ruzuku ya serikali.

Labda hawa jamaa wanaoitwa viongozi wetu waliweka hayo makodi bila kuwa na nia ya ndani kabisa ya kuhakikisha kila senti ya kodi ya mtanzania inatumika kuleta tofauti katika sura ya nchi yetu na maisha ya watu wetu. After all JPM alikuwa mtu mmoja tu wa aina yake tofauti kati ya lundo la wanasiasa ambao kwao hawana nia ya dhati ya maono na usimamizi katika kufikia ndoto za nchi yetu.

Ndio maana hawa wakiyumbishwa tu na kelele wanakimbilia shimoni kama panya aliyesikia kelele za nyau.

Kuna mtu mmoja hapo juu amehoji, Hivi kwa uongozi wa aina hii hivi hata SGR, Nyerere Dam vingethubutu hata kuanza?

Uongozi wa aina hii ungeweza kuja na msimamo thabiti na wa aina yake kwamba no lock down?

Demokrasia siyo kuyumba katika maamuzi, huo ni udhaifu. Demokrasia ni kuja na maono na mawazo shirikishi, lakini ikifika wakati wa kutekeleza uthabiti wa maamuzi utahitajika.
Sukuma gang kazin
 
Kwa hiyo wewe kwa uelewa wako mfupi kuumiza wananchi ni kwenye Kodi tuu?

Unapokuwa huna umeme, barabara,shule, hospital,maji nk huumii?

Utatoka vipi kwenye umaskini? Hakuna ku move bila kuumia haipo hiyo na ukiwa maskini ndio unaumia kwenye kila kitu
Kinachokwamisha serikali nyingi za kiafrika kutokusonga mbele ni UFISADI, na matumizi mabovu ya fedha, na ndio maana mwananchi anakuwa mgumu kulipa kodi, leo waziri wa fedha anaulizwa kwanini wasianze wao kupunguza matumizi kwenye misafara ya viongozi, eti ana jibu kwenye misafara ile hasa ya rais wengi wao wanatumia magari yao binafsi kweli?!!yale ya ma V8, ni ya kwao binafsi!!inshu wala sio kukusanya kama hujadhibiti upotevu wa hayo mapato ni bure, huyo mnyonge mtamuua tu, na kile mnachomuahidi kamwe hatakiona!!mfano awamu ya tano tuliaminishwa kuwa makusanyo yanakusanywa kweli kweli, na pesa haipotei!!lipi la maana sana lilifanyika, kama ni deni la taifa lilipaa sio kawaida!!
Hali ya madawa hospitalini haikuwa na unafuu wowote!!
 
Back
Top Bottom