Serikali inajua hiki tunachofanyiwa na Halmashauri ya Wilaya Kibaha

baraka bb

JF-Expert Member
Mar 20, 2016
2,691
3,858
Habari zenu wakuu!

Mimi ni dereva wa fuso ya kubeba mchanga, huwa tunafata mchanga Kibaha na kupeleka Dar es Salaam. Kipindi cha nyuma tulikuwa tunafanya kazi usiku na mchana na huwa tunanunua mchanga sh 10000/= ushuru wa halmashauri Kibaha 3000/= na Kinondon 1000/=

Halmashauri ya Kibaha ikaleta tamko kwamba tuwe tunafanya kazi kuanzia saa 12 asubuh - 12 jioni. Kumbuka tulikuwa tunalipa kodi kwa kila trip 1 na tulikuwa na uwezo wa kupiga trip zaidi ya 10 ila sasa hivi tunaenda trip 3 hadi 4 kutokana na ufinyu wa muda.

Kilichotokea leo hii tunapita hapa kwenye kulipia kibali cha mchanga (ushuru) mtu wa halmashauri anatuzuia anataka tulipe faini 50,000/=. Anasema ilitakiwa saa12 ndo tuingie shamba sio tuwe tunatoka kama tulivyofanya leo.

Je hii ni sahihi kwa nchi inayoendelea kama hii kupangiwa muda finyu wa kufanya kazi? Je Serikali kuu inatambua hili tunalofanyiwa?

Hadi sasa bado tumekaa hapa Kibaha TAMCO tunasubiri muafaka, hatuwezi kulipa faini ya ajabu hivi kwani huu ni uonevu!

ImageUploadedByJamiiForums1482982653.772790.jpg
 
Poleni sana, bila msimamo mtakua mnaonewa kila siku.

amekuja mkurugenz hapa anasema tulipe fain elfu50 alfu yeye atalifanyia kaz ili swala ila elfu50 tulipe daaah nmecheka sana ,, unaweza pata kes ya mauaji hapa
 
Watumishi wa umma hawana huruma na wajasiliamali kwa sababu wao hawajafanya hata biashara ya kuuza karanga wanaona wafanyabiashara wana fedha sana ukilipa elfu 50 utakuwa ushapata hasara ila wao hilo hawalioni wanakuwa na roho mbaya sijui kwa nini.
Ripoti ya benki ya dunia inasema Tanzania ni moja kati ya nchi zenye mazingira magumu ya kufanya biashara lakini wana siasa wetu wanapiga porojo za hapa kazi tu,watu wajiajiri,Tanzania ya viwanda utafikiri hizo ajira au viwanda vinatoka mbinguni hawana ubunifu kabisa yapo yapo tu.
Badala ya kutengeneza mazingira mazuri ili vijana wajiajiri yenyewe yanapiga porojo tu.
 
Nadhani kuna pesa inahitajika idara Fulani haraka aidha kati ya afya na elimu haswa ndio maana wamewashitukiza na jamaa kakazia lipa afanyie kazi komaeni tu
 
Habari zenu wakuu!

Mimi ni dereva wa fuso ya kubeba mchanga, huwa tunafata mchanga Kibaha na kupeleka Dar es Salaam. Kipindi cha nyuma tulikuwa tunafanya kazi usiku na mchana na huwa tunanunua mchanga sh 10000/= ushuru wa halmashauri Kibaha 3000/= na Kinondon 1000/=

Halmashauri ya Kibaha ikaleta tamko kwamba tuwe tunafanya kazi kuanzia saa 12 asubuh - 12 jioni. Kumbuka tulikuwa tunalipa kodi kwa kila trip 1 na tulikuwa na uwezo wa kupiga trip zaidi ya 10 ila sasa hivi tunaenda trip 3 hadi 4 kutokana na ufinyu wa muda.

Kilichotokea leo hii tunapita hapa kwenye kulipia kibali cha mchanga (ushuru) mtu wa halmashauri anatuzuia anataka tulipe faini 50,000/=. Anasema ilitakiwa saa12 ndo tuingie shamba sio tuwe tunatoka kama tulivyofanya leo.

Je hii ni sahihi kwa nchi inayoendelea kama hii kupangiwa muda finyu wa kufanya kazi? Je Serikali kuu inatambua hili tunalofanyiwa?

Hadi sasa bado tumekaa hapa Kibaha TAMCO tunasubiri muafaka, hatuwezi kulipa faini ya ajabu hivi kwani huu ni uonevu!

View attachment 451535

Kaka fikiria upya biashara ya Mchanga fuso imekuwa kichaa, majuzi hapo kulikuwa na watu wa Maturubai, yaani alikuwa anapanda juu ya mchanga na anarukaruka, mchanga ukimwagika kidogo tu barabarani faini LAKI TANO (500,000) na gari linapelekwa yard Tamco, ukishindwa kulipa siku moja penalt inaongezeka

Maana hapo kuna SUMATRA, VIPIMO, MAPATO, TURUBAI, USALAMA, gari linahitaji service, dereva anahitaji posho, kila trip kuna 2000 ya Trafic na kila ijumaa kuna HESABU YA MEZA- Yaani kuna 5000 ya trafiki ambayo ni tofauti na 2000 ya kila siku, we mwenye gari utapata nini

Kama una pesa weka box body au Bomba peleka gari shamba
 
Watumishi wa umma hawana huruma na wajasiliamali kwa sababu wao hawajafanya hata biashara ya kuuza karanga wanaona wafanyabiashara wana fedha sana ukilipa elfu 50 utakuwa ushapata hasara ila wao hilo hawalioni wanakuwa na roho mbaya sijui kwa nini.
Ripoti ya benki ya dunia inasema Tanzania ni moja kati ya nchi zenye mazingira magumu ya kufanya biashara lakini wana siasa wetu wanapiga porojo za hapa kazi tu,watu wajiajiri,Tanzania ya viwanda utafikiri hizo ajira au viwanda vinatoka mbinguni hawana ubunifu kabisa yapo yapo tu.
Badala ya kutengeneza mazingira mazuri ili vijana wajiajiri yenyewe yanapiga porojo tu.

Hao madereva wangekuwa ni wazungu wasingesumbuliwa, shame on them.
 
Je hii ni sahihi kwa nchi inayoendelea kama hii kupangiwa muda finyu wa kufanya kazi?


Sasa hawaeleweki, je tafsiri ya Hapa kazi tu ni nini, watu wakifanya kazi kosa wakienda kwenye pool kosa wakienda kusomba mchanga mapema kosa, au kuna jambo limejificha hamjaliona enyi madereva
 
kuna mambo yanafanyika sehemu mpaka mtu wa 3 unaona aibu ila muhusika macho makavu.

kwa hili mkurugenzi anatakiwa aondoke, mambo ya kusema mlipe faini ndo aje ashughulikie kero hii ni utoto wa hali ya juu.
 
Nimepita nimeliona hili, poleni
Rweye pole haitoshi hebu ongea na wazee wetu Lumumba pale wamkaripie huyo Mkurugenzi..kumbuka kwa sasa Wakurugenzi ni makada wenzetu..wanatengeneza hasira za sisi kunyimwa fursa baadae
 
Mrejesho wakuu,.
Baada ya kumsonga sana Mkugurenz na kugomea kutoa hyo elfu50 had aje Mkuu wa Mkoa akatuambia et ametupunguzia fain kwa hyo tumpe elfu 10 kwa kila gari daaah nmecheka sana had kuna askal nilimuita pemben nikamuuliza iv hawa viongoz huwa hawalipwi mishahara naye akacheka akasema toen tu muende asije watafutia jambo lingine

so kuanzia kesho tuwe tunaamka saa 12 asubuh kwenda shamba kupakia mchanga kumbuka kutoka mbez had kufika Soga ni mwendo wa masaa3 na hili uweze kupata hesabu ya boss ni lazima upige trip 4 ,,.'naona kila dalili ya kurudisha hii gar
 
Back
Top Bottom