Serikali inaendelea kufanya ubaguzi kwenye ajira. Kama una div 1&2 au bachelor degree jua upo kwenye risk ya kutoajiriwa

Tangu ile moment wakati tupo chuo nilipoona wanaCCM ambao hawana mkopo wanaambiwa waandike majina ishu zao za mikopo zishughulikiwe na ukweli walikuwa wanashughulikiwa, sijawahi kuwa na na hawa so called serikali. Ubaguzi hautakaa uishe....
 
Ukweli mtupu asilimia kubwa ya watu tuliosoma kwa bidii ndo tuna hustle sana kwenye sekta ya kutafuta ajira, failure wote wanamaisha mazuri, ila tuliokuwa tunafuhuru tu ajira zinatupiga chenga, Mana saiz ajira zinaishia veta na diploma, Kwenda form six ni kupoteza mda , hakuna professional yoyote unayopata ndani ya hiyo miaka miwili.
 
Suluhisho ni kupunguza muda kustaafu kutoka 60 hadi 50 serikalini.

Pia serikali kuweka mazingira rafiki ili makampuni binafsi yawe mengi, maana ndio wazalishaji wa ajira.

Bila kusahau mazingira rafiki kwa wafanyabiashara ili raia wajiajiri kupitia biashara.
Nimesema suala hili kwa muda mrefu.mimi napendekeza kustaafu iwe hata 45yrs.tatizo litakwisha.Au iwe ajira za mkataba wa miaka 10-15tu.
 
Umeongea vizuri kiongozi.Mimi huwa nashangaa matangazo ya kazi wanahitaji watu wenye cheti cha atec 1 ya nbaa wakati kimsingi nbaa hawatoagi cheti cha atec 1.!!nbaa wanatoa cheti kwa atec 2 na CPA tu.Sasa jiulize ina maana watu wa serikali hawajuhi kuwa nbaa hawatoi cheti cha atec 1???
 
Iko hivi,polisi wanawataka waliofeli maana hawawezi kuhoji chochote. Akiambiwa piga,anapiga. Lipua,analipua. Ajiri mtu mwenye masters yake sasa,lazima ahoji. After all,msomi siku zote Ana exposure yakutosha. Ndio maana ukiangalia vikosi vvyetu,utagundua Kuna tatizo kubwa Sana.
 
waziri simbachawene amesema wana ajiri wenye division zero ili wakashike silaha na kulinda benki kwahiyo ww na One yako kaa kwa kutulia hizi ajira ni special kwa failures tu
 
Nilikomaa kusoma hadi varsity huko nitatoka na GPA 3.8 but job niliyopata ni ya kisenge.Niliomba chance huko jeshini (JW,Magereza hadi Polisi) hata nafasi ya kuitwa kwenye interview sikuipata.

Rafiki yangu tuliyekuwa naye Form 6 na akaishia hapo,yeye alichukuliwa JW huku mimi nikiachwa.Sasa jamaa ni Luteni na anakula maisha ile mbaya kiasi kwamba ananitimulia vumbi kwa mbali mno.

Sisi wenye nyota za kunguni tumeshakoma!
 
Suluhisho ni kupunguza muda kustaafu kutoka 60 hadi 50 serikalini.

Pia serikali kuweka mazingira rafiki ili makampuni binafsi yawe mengi, maana ndio wazalishaji wa ajira.

Bila kusahau mazingira rafiki kwa wafanyabiashara ili raia wajiajiri kupitia biashara.
Hadi 45
 
Serikali mara kwa mara imekuwa ikiwahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kufaulu lakini jambo la kusikitisha unapofika wakati wa ajira serikali hiyo hiyo inawabagua tena.

Tumeona kwenye ajira za polisi wanaotakiwa ni wale ambao hawakufanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne. Yaani waliopata divisheni Four ila waliofaulu vizuri kwa kupata divisheni one na Two hawatakiwi.

Sanjari na hilo, kuna ubaguzi mkubwa unafanywa na serikali kwenye utoaji wa ajira hasa kwa wahitimu wenye elimu ya juu i.e bachelor degree holders kulinganisha na level zingine za kielimu kama vile diploma na certificate.

Mfano mimi nimehitimu kidato cha nne mwaka 2011. Kwakuwa nilikuwa na ndoto ya kufika mbali kielimu kama serikali inavyosisitiza, nilisoma kwa bidii na kufanikiwa kuendelea na elimu ya kidato cha tano na sita.

Sikuishia hapo, niliendelea kukazana kwa nguvu zote na maarifa yote na hatimaye nikafanikiwa kuendelea na elimu ya juu na sasa ni mhitimu wa moja ya chuo kikubwa hapa nchini

Lakini katika yote, wenzangu niliomaliza nao kidato cha nne wakapata ufaulu wa divisheni Four kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti leo hii ni waajiriwa wa serikali wanakula keki ya Taifa.

Niliomaliza nao kidato cha sita wakakosa sifa (qualifications) za kujiunga chuo kikuu wakaenda kusomea ualimu ngazi ya diploma tayari wote wameajiriwa serikalini

Lakini mimi niliyefuata ushauri wa serikali wa kusoma kwa bidii na kufaulu kwa kufikia kiwango cha elimu ya juu leo naonekana sina thamani kwani serikali ile ile iliyonihamasisha kusoma kwa bidii ndio ile ile imeniweka mtaani kwa takribani miaka minne sasa. Kwa maana nyingine kiherehere changu cha kusoma kwa bidii na kufaulu leo hii ndio kinaniponza kwa sababu kama ningefeli kidato cha nne au sita leo ningekuwa ni miongoni mwa wanaofaidi keki ya Taifa.

Mwisho wa yote kama serikali haina mpango wa kuajiri wahitimu wenye bachelor degree tunaomba itamke hadharani ilikusudi vijana tujue moja kwani hata ajira zinapotangazwa wenye bachelor degree wanaoajiriwa ni wachache sana tena nafikiri ni katika jitihada za serikali kuficha dhambi ya ubaguzi wanayoifanya isijulikane kirahisi.
Taratibu zakazi huwa haziangalii daraja ya masomo ya juu huwa unatangaza kuanzia hapa.
Kama kazi inahitaji kijana waelimu ya chini hutangazi.
Unaweza kusema sifa ni mtu kuwa na certificate ya Form IV
watakao kuja unafanya usaili>
Wewe una degree jee huoni kazii itakuwa umeover qualified na mshahara utakao pata utaku wachini sana?
Kwanini uka apply hii kazi na msuali mengine lakini hutangazi kuwa nataka watu daraja gani tuu.
 
Nina division four yangu safi ya form four, sasa hivi nipo ofisi nyeti ya serikali napiga kazi😏
 
Serikali mara kwa mara imekuwa ikiwahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kufaulu lakini jambo la kusikitisha unapofika wakati wa ajira serikali hiyo hiyo inawabagua tena.

Tumeona kwenye ajira za polisi wanaotakiwa ni wale ambao hawakufanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne. Yaani waliopata divisheni Four ila waliofaulu vizuri kwa kupata divisheni one na Two hawatakiwi.

Sanjari na hilo, kuna ubaguzi mkubwa unafanywa na serikali kwenye utoaji wa ajira hasa kwa wahitimu wenye elimu ya juu i.e bachelor degree holders kulinganisha na level zingine za kielimu kama vile diploma na certificate.

Mfano mimi nimehitimu kidato cha nne mwaka 2011. Kwakuwa nilikuwa na ndoto ya kufika mbali kielimu kama serikali inavyosisitiza, nilisoma kwa bidii na kufanikiwa kuendelea na elimu ya kidato cha tano na sita.

Sikuishia hapo, niliendelea kukazana kwa nguvu zote na maarifa yote na hatimaye nikafanikiwa kuendelea na elimu ya juu na sasa ni mhitimu wa moja ya chuo kikubwa hapa nchini

Lakini katika yote, wenzangu niliomaliza nao kidato cha nne wakapata ufaulu wa divisheni Four kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti leo hii ni waajiriwa wa serikali wanakula keki ya Taifa.

Niliomaliza nao kidato cha sita wakakosa sifa (qualifications) za kujiunga chuo kikuu wakaenda kusomea ualimu ngazi ya diploma tayari wote wameajiriwa serikalini

Lakini mimi niliyefuata ushauri wa serikali wa kusoma kwa bidii na kufaulu kwa kufikia kiwango cha elimu ya juu leo naonekana sina thamani kwani serikali ile ile iliyonihamasisha kusoma kwa bidii ndio ile ile imeniweka mtaani kwa takribani miaka minne sasa. Kwa maana nyingine kiherehere changu cha kusoma kwa bidii na kufaulu leo hii ndio kinaniponza kwa sababu kama ningefeli kidato cha nne au sita leo ningekuwa ni miongoni mwa wanaofaidi keki ya Taifa.

Mwisho wa yote kama serikali haina mpango wa kuajiri wahitimu wenye bachelor degree tunaomba itamke hadharani ilikusudi vijana tujue moja kwani hata ajira zinapotangazwa wenye bachelor degree wanaoajiriwa ni wachache sana tena nafikiri ni katika jitihada za serikali kuficha dhambi ya ubaguzi wanayoifanya isijulikane kirahisi.
Hivi kama unamchukuwa kijana wa dv4 una mpa kaz anaifanya vizuri alafu una mchukia wa dv1 anafanya kama darasa la Saba wewe unge muajiri nani? Elimu imeimgiliwa mm naona sawa tu.
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom