Wakuu nimeona nililete hapa ili tujadiliane na pengine kuishauri serikali kuchukua hatua madhubuti wanafunzi wanaoongoza matokeo mbalimbali ya mitihani ya kitaifa. Mathalani, kuna wanafunzi wameongoza mitihani ya kidato cha nne yaliyotoka juzi kwa kupata alama za juu sana kuliko wenzao, top ten etc.
Nadhani ni wakati muafaka sasa kwa wizara husika kuona umuhimu wa kuwapa motisha vijana hawa na wale wanaoendelea na masomo yao kwa kuwatafutia program nzuri either nje ya nchi au ndani na kuwafuatilia kwa karibu maendeleo yao huenda wakatufaa sana hasa kwa Tanzania hii mpya ya viwanda.
Nadhani ni wakati muafaka sasa kwa wizara husika kuona umuhimu wa kuwapa motisha vijana hawa na wale wanaoendelea na masomo yao kwa kuwatafutia program nzuri either nje ya nchi au ndani na kuwafuatilia kwa karibu maendeleo yao huenda wakatufaa sana hasa kwa Tanzania hii mpya ya viwanda.