Ndugu wanabodi nashangazwa sana kwa msimamo wa kampuni ya Multichoice ambayo inatoa huduma ya kuonyesha chanel za TV za digitali nchini kwa kupitia DSTV.
Kampuni hii haijaonyesha nia au tuseme imekataa kuweka chanel za kitaifa za hapa nyumbani ambazo ndizo zinatupa habari za hapa nyumbani.
Nashangazwa sana na msimamo huu pamoja na ukimya wa serikali hasa kupitia TCRA na wizara husika ambao ndio wanapaswa kulinda maslahi ya wananchi wake.
Inavyoelekea baadhi ya viongozi wa serikali wana maslahi binafsi kwenye kampuni hii. Iweje kampuni zingine kama Star time na Zuku waweze kuingiza chanel zetu za kitaifa kama ITV na Star Tv kwenye bundle zao lakini DSTV wakatae? Hakuna mantiki yoyote ya kutoziingiza hizi chanel kwani ni chanel ambazo si za kulipia.
Hii ina maana watu tulio na DSTV baada ya tarehe 31 mwezi huu hatutaweza kuona chanel zetu labda kama utanunua king'amuzi kingine ambacho nacho uwe unakilipia. Na kama TV yako haiwezi kuchukua ving'amuzi viwili basi itakubidi ununue TV nyingine! Au uondoe deki nk
Pia ingawa hawa jamaa wanatoa huduma kibiashara lakini bei zao ni kubwa mno tofauti hata ukiwa huko kwao SA na hata huwezi ukalinganisha na watu wanavyotozwa huko ulaya au marekani ambako wao ndio wenye kipato kikubwa. Huduma za TV ni chanzo cha taarifa na elimu (information & education) kwa karne hii kama ilivyo simu za mkononi si anasa tena Bali ni huduma muhimu kwa wananchi.
Pamoja na kwamba hawa Multichoice wana miaka 15 wakitoa hii huduma ya DSTV na sasa hivi wana wateja wengi ambapo ingewezekana kupunguza bei kwa kiwango kikubwa lakini bei zao zimebaki kuwa za kiwizi. Sasa hivi wanatudanganya kwa kupunguza asilimia 10!
Pamoja na kwamba kujiunga na DSTV ni hiari kama ilivyo kujiunga na makampuni ya simu za mkononi hii haihalalishi wizi kwa mteja na kichwa ngumu kukataa kuingiza TV zetu za kitaifa za kitanzania na serikali yetu ikiwaangalia na kuendelea kutoza gharama ya wastani wa 120,000 kwa mwezi ambayo ni sawa na elfu 4 kwa siku!
Kampuni hii haijaonyesha nia au tuseme imekataa kuweka chanel za kitaifa za hapa nyumbani ambazo ndizo zinatupa habari za hapa nyumbani.
Nashangazwa sana na msimamo huu pamoja na ukimya wa serikali hasa kupitia TCRA na wizara husika ambao ndio wanapaswa kulinda maslahi ya wananchi wake.
Inavyoelekea baadhi ya viongozi wa serikali wana maslahi binafsi kwenye kampuni hii. Iweje kampuni zingine kama Star time na Zuku waweze kuingiza chanel zetu za kitaifa kama ITV na Star Tv kwenye bundle zao lakini DSTV wakatae? Hakuna mantiki yoyote ya kutoziingiza hizi chanel kwani ni chanel ambazo si za kulipia.
Hii ina maana watu tulio na DSTV baada ya tarehe 31 mwezi huu hatutaweza kuona chanel zetu labda kama utanunua king'amuzi kingine ambacho nacho uwe unakilipia. Na kama TV yako haiwezi kuchukua ving'amuzi viwili basi itakubidi ununue TV nyingine! Au uondoe deki nk
Pia ingawa hawa jamaa wanatoa huduma kibiashara lakini bei zao ni kubwa mno tofauti hata ukiwa huko kwao SA na hata huwezi ukalinganisha na watu wanavyotozwa huko ulaya au marekani ambako wao ndio wenye kipato kikubwa. Huduma za TV ni chanzo cha taarifa na elimu (information & education) kwa karne hii kama ilivyo simu za mkononi si anasa tena Bali ni huduma muhimu kwa wananchi.
Pamoja na kwamba hawa Multichoice wana miaka 15 wakitoa hii huduma ya DSTV na sasa hivi wana wateja wengi ambapo ingewezekana kupunguza bei kwa kiwango kikubwa lakini bei zao zimebaki kuwa za kiwizi. Sasa hivi wanatudanganya kwa kupunguza asilimia 10!
Pamoja na kwamba kujiunga na DSTV ni hiari kama ilivyo kujiunga na makampuni ya simu za mkononi hii haihalalishi wizi kwa mteja na kichwa ngumu kukataa kuingiza TV zetu za kitaifa za kitanzania na serikali yetu ikiwaangalia na kuendelea kutoza gharama ya wastani wa 120,000 kwa mwezi ambayo ni sawa na elfu 4 kwa siku!