Serikali Imewekwa Mfukoni na Kampuni ya Multichoice!

blueray

JF-Expert Member
Sep 15, 2012
2,217
423
Ndugu wanabodi nashangazwa sana kwa msimamo wa kampuni ya Multichoice ambayo inatoa huduma ya kuonyesha chanel za TV za digitali nchini kwa kupitia DSTV.

Kampuni hii haijaonyesha nia au tuseme imekataa kuweka chanel za kitaifa za hapa nyumbani ambazo ndizo zinatupa habari za hapa nyumbani.

Nashangazwa sana na msimamo huu pamoja na ukimya wa serikali hasa kupitia TCRA na wizara husika ambao ndio wanapaswa kulinda maslahi ya wananchi wake.

Inavyoelekea baadhi ya viongozi wa serikali wana maslahi binafsi kwenye kampuni hii. Iweje kampuni zingine kama Star time na Zuku waweze kuingiza chanel zetu za kitaifa kama ITV na Star Tv kwenye bundle zao lakini DSTV wakatae? Hakuna mantiki yoyote ya kutoziingiza hizi chanel kwani ni chanel ambazo si za kulipia.

Hii ina maana watu tulio na DSTV baada ya tarehe 31 mwezi huu hatutaweza kuona chanel zetu labda kama utanunua king'amuzi kingine ambacho nacho uwe unakilipia. Na kama TV yako haiwezi kuchukua ving'amuzi viwili basi itakubidi ununue TV nyingine! Au uondoe deki nk

Pia ingawa hawa jamaa wanatoa huduma kibiashara lakini bei zao ni kubwa mno tofauti hata ukiwa huko kwao SA na hata huwezi ukalinganisha na watu wanavyotozwa huko ulaya au marekani ambako wao ndio wenye kipato kikubwa. Huduma za TV ni chanzo cha taarifa na elimu (information & education) kwa karne hii kama ilivyo simu za mkononi si anasa tena Bali ni huduma muhimu kwa wananchi.

Pamoja na kwamba hawa Multichoice wana miaka 15 wakitoa hii huduma ya DSTV na sasa hivi wana wateja wengi ambapo ingewezekana kupunguza bei kwa kiwango kikubwa lakini bei zao zimebaki kuwa za kiwizi. Sasa hivi wanatudanganya kwa kupunguza asilimia 10!

Pamoja na kwamba kujiunga na DSTV ni hiari kama ilivyo kujiunga na makampuni ya simu za mkononi hii haihalalishi wizi kwa mteja na kichwa ngumu kukataa kuingiza TV zetu za kitaifa za kitanzania na serikali yetu ikiwaangalia na kuendelea kutoza gharama ya wastani wa 120,000 kwa mwezi ambayo ni sawa na elfu 4 kwa siku!
 
Si nilisikia kuwa kuna tbc kwa dstv?
Kuhusu suala la bei maybe kwakuwa wanatumia W4 Eutelsat satellite with Ku-band services lazima gharama za uendeshaji ziwe juu
 
aiseeee babaangu kwanza elewa itv and star tv si channel za kitaifa channel ya taifa ni tbc pekee ndio maana wapo dstv swala la itv kuwa kwenye dstv ni swala gumu sana coz itv haina vipindi au uchambuzi wa vitu muhimu we angalia habari zake za kimataifa wanataja vichwa vya habari bila maelezo ya kina ,,na swala la itv kuwa kwenye dstv ni swala la mmiliki kuongea na dstv na si serekali mkuu

karibu mkuu rombo upate mbege
 
Si nilisikia kuwa kuna tbc kwa dstv?
Kuhusu suala la bei maybe kwakuwa wanatumia W4 Eutelsat satellite with Ku-band services lazima gharama za uendeshaji ziwe juu

Mkuu ni kweli wameweka TBC lakini kwa nini na wao wasiweke vituo vingine vya kitaifa ambavyo tumekuwa tukivipata bure. Kampuni zingine za Star Time Na Zuku pamoja na kwamba nao wanafanya biashara kama ya Multichoice chini ya uangalizi mmoja wa TCRA wameweka hivi vituo Au wao wana masharti tofauti.

Bei za DSTV zimekuwa juu tangu ianzishwe miaka 15 iliyopita. Makampuni yote yanapokuwa wamepata wateja wengi hupunguza gharama lakini hawa jamaa wako kiuchumaji na wanacharge kwa dola kinyume na keseni yao ya biashara. Ukienda kulipia wanakupigia mahesabu ya dola!
 
Mkuu ni kweli wameweka TBC lakini kwa nini na wao wasiweke vituo vingine vya kitaifa ambavyo tumekuwa tukivipata bure. Kampuni zingine za Star Time Na Zuku pamoja na kwamba nao wanafanya biashara kama ya Multichoice chini ya uangalizi mmoja wa TCRA wameweka hivi vituo Au wao wana masharti tofauti.

Bei za DSTV zimekuwa juu tangu ianzishwe miaka 15 iliyopita. Makampuni yote yanapokuwa wamepata wateja wengi hupunguza gharama lakini hawa jamaa wako kiuchumaji na wanacharge kwa dola kinyume na keseni yao ya biashara. Ukienda kulipia wanakupigia mahesabu ya dola!

blueray hapo kwenye dola ni uzembe wa moja kwa moja wa serikali,sijui hadi lini tutaendelea kutumia dola hapa bongo,na sijui ni kwanin wahusoka huishia kupiga stori tu pasipo kutekeleza,,,,viongozi wetu wanaitumia Dstv kwanini hawakemei matumizi ya dola?maana kwenye matangazo yao inaonesha nigeria wanatumia naira na s.a wanatumia RAND,
 
Last edited by a moderator:
aiseeee babaangu kwanza elewa itv and star tv si channel za kitaifa channel ya taifa ni tbc pekee ndio maana wapo dstv swala la itv kuwa kwenye dstv ni swala gumu sana coz itv haina vipindi au uchambuzi wa vitu muhimu we angalia habari zake za kimataifa wanataja vichwa vya habari bila maelezo ya kina ,,na swala la itv kuwa kwenye dstv ni swala la mmiliki kuongea na dstv na si serekali mkuu

karibu mkuu rombo upate mbege

Asante Mkuu rombo naona sasa hivi utakuwa kwenye supu baada ya mbege ya jana. Ila Mkuu mbona watu Wa Zuku Na Srar Time wameweka hizo Chanel kwenye bundle zao, Au wao wana masharti tofauti?
Pamoja na kwamba hizi Chanel zetu hazina vipindi vingi vya uchambuzi lakini zinatupasha matukio mengi yanayotokea nchini. Na DSTV kutoweka hizi tv kwenye bundle zao ni kuwanyima haki watenzania wenye DSTV. Cha msingi zaidi Kama ilivyo tbc hizi ni free Chanel
 
Asante Mkuu rombo naona sasa hivi utakuwa kwenye supu baada ya mbege ya jana. Ila Mkuu mbona watu Wa Zuku Na Srar Time wameweka hizo Chanel kwenye bundle zao, Au wao wana masharti tofauti?
Pamoja na kwamba hizi Chanel zetu hazina vipindi vingi vya uchambuzi lakini zinatupasha matukio mengi yanayotokea nchini. Na DSTV kutoweka hizi tv kwenye bundle zao ni kuwanyima haki watenzania wenye DSTV. Cha msingi zaidi Kama ilivyo tbc hizi ni free Chanel

me nimekuelewa,hapo unachomaanisha ni kwamba tukiwa kwenye digitali utakosa habari kwakua utakua upo dstv,so ili nawe upate habar na usiwe na ving'amuz zaid ya kimoja ungependa Dstv wawe na channel za kitanzania huko,
ok labda watalifanyia kazi
 
Ngoja zuku, star times na wengine wajikite vilivyo kwenye channel za mpira, dstv ndio watajua kwanini watu wananunua ving'amuzi vyao!!
 
Ndugu wanabodi nashangazwa sana kwa msimamo wa kampuni ya Multichoice ambayo inatoa huduma ya kuonyesha chanel za TV za digitali nchini kwa kupitia DSTV.

Kampuni hii haijaonyesha nia au tuseme imekataa kuweka chanel za kitaifa za hapa nyumbani ambazo ndizo zinatupa habari za hapa nyumbani.

Nashangazwa sana na msimamo huu pamoja na ukimya wa serikali hasa kupitia TCRA na wizara husika ambao ndio wanapaswa kulinda maslahi ya wananchi wake.

Inavyoelekea baadhi ya viongozi wa serikali wana maslahi binafsi kwenye kampuni hii. Iweje kampuni zingine kama Star time na Zuku waweze kuingiza chanel zetu za kitaifa kama ITV na Star Tv kwenye bundle zao lakini DSTV wakatae? Hakuna mantiki yoyote ya kutoziingiza hizi chanel kwani ni chanel ambazo si za kulipia.

Hii ina maana watu tulio na DSTV baada ya tarehe 31 mwezi huu hatutaweza kuona chanel zetu labda kama utanunua king'amuzi kingine ambacho nacho uwe unakilipia. Na kama TV yako haiwezi kuchukua ving'amuzi viwili basi itakubidi ununue TV nyingine! Au uondoe deki nk

Pia ingawa hawa jamaa wanatoa huduma kibiashara lakini bei zao ni kubwa mno tofauti hata ukiwa huko kwao SA na hata huwezi ukalinganisha na watu wanavyotozwa huko ulaya au marekani ambako wao ndio wenye kipato kikubwa. Huduma za TV ni chanzo cha taarifa na elimu (information & education) kwa karne hii kama ilivyo simu za mkononi si anasa tena Bali ni huduma muhimu kwa wananchi.

Pamoja na kwamba hawa Multichoice wana miaka 15 wakitoa hii huduma ya DSTV na sasa hivi wana wateja wengi ambapo ingewezekana kupunguza bei kwa kiwango kikubwa lakini bei zao zimebaki kuwa za kiwizi. Sasa hivi wanatudanganya kwa kupunguza asilimia 10!

Pamoja na kwamba kujiunga na DSTV ni hiari kama ilivyo kujiunga na makampuni ya simu za mkononi hii haihalalishi wizi kwa mteja na kichwa ngumu kukataa kuingiza TV zetu za kitaifa za kitanzania na serikali yetu ikiwaangalia na kuendelea kutoza gharama ya wastani wa 120,000 kwa mwezi ambayo ni sawa na elfu 4 kwa siku!

Wewe ulizaliwa nayo hiyo DSTV? kama wanazingua achana nao kwani lazima? au wewe ndio wale wanaoishi kwa misifa?
 
Wewe ulizaliwa nayo hiyo DSTV? kama wanazingua achana nao kwani lazima? au wewe ndio wale wanaoishi kwa misifa?

CHIEF...YOU NAILED IT WELL...jamaa kangangania dstv..dstv..utadhani ndio baba na mama yake.

hao majambazi walishatuibia kiasi cha kutosha na njia sahihi ni kutowapa ushirikiano kwa kutojiunga na huduma zao mpaka washushe bei ifikie tsh 9000 kwa mwezi kama wenzao...kama hawawezi wafungashe virago wasepe..

tanzania bila dstv...inawezekanaaaaaaaaa.
 
Asante Mkuu rombo naona sasa hivi utakuwa kwenye supu baada ya mbege ya jana. Ila Mkuu mbona watu Wa Zuku Na Srar Time wameweka hizo Chanel kwenye bundle zao, Au wao wana masharti tofauti?
Pamoja na kwamba hizi Chanel zetu hazina vipindi vingi vya uchambuzi lakini zinatupasha matukio mengi yanayotokea nchini. Na DSTV kutoweka hizi tv kwenye bundle zao ni kuwanyima haki watenzania wenye DSTV. Cha msingi zaidi Kama ilivyo tbc hizi ni free Chanel

aiseeeeeee babaangu umenena vema napata supu kukata mbege ya jana,,mi nadhani kunavigezo vinavyotumika mpaka channel iwekwe dstv kwa tz hakuna channel yenye hadhi ya kuwa dstv wakiweka tv za mbongo sito lipia tena dstv
ngoja niagize mbege nizimue
 
Nchi ya wafanyabiashata. Bei Zao zinabadilika kutokana na kupanda na kushuka kwa dola na serikali imekaa kimya tuendelee kunyonywa tu! Wao si wamewekewa Bure na wanalipiwa na serikali kama entertainment, hawajui gharama zake mpaka pale wanapostaafu ndo wanashtuka, na wenginee wamewekeza humo
 
Mi nimefunga zangu easy tv for local channels na nafunga abudhabi sports soon kwa ajili ya mpira.. Nimeshawachoka multichoice na ufisadi wao
 
Mi nimefunga zangu easy tv for local channels na nafunga abudhabi sports soon kwa ajili ya mpira.. Nimeshawachoka multichoice na ufisadi wao

Kwa kweli Mkuu itabidi namimi nianze mikakati ya kuondokana na hawa multichoice ni wezi wakuu! hawa makaburu yanatuibia sana. Watu tulivyo busy na ujenzi wa taifa wakati mwingine hupati hata muda wa kuangalia tv lakini kila siku elfu 4 inakwenda!

Hebu Mkuu nisaidie kati ya hao jamaa wa easy tv, Zuku Na Star time ni wepi wenye quality nzuri zaidi. Na
hiyo abudhabi sports unafunga dishi ya aina gani
 
Nchi ya wafanyabiashata. Bei Zao zinabadilika kutokana na kupanda na kushuka kwa dola na serikali imekaa kimya tuendelee kunyonywa tu! Wao si wamewekewa Bure na wanalipiwa na serikali kama entertainment, hawajui gharama zake mpaka pale wanapostaafu ndo wanashtuka, na wenginee wamewekeza humo

Hii ni kweli kabisa. kwa kweli watanzania tuna safari ndefu, mafisadi wametubana kila mahali!
 
Wewe ulizaliwa nayo hiyo DSTV? kama wanazingua achana nao kwani lazima? au wewe ndio wale wanaoishi kwa misifa?

Mkuu nimekuelewa. mimi niko kwenye mchakato wa kuachana nao.

Ila nimeleta hii topic ikiwezekana tuwe kitu kimoja tuwakatae hawa makaburu wezi.
Pia vile vile hawa wenzetu tuliowapa mamlaka ya kulinda maslahi yetu waamke na wafanye kazi kwa manufaa ya watanzania.
 
aiseeeeeee babaangu umenena vema napata supu kukata mbege ya jana,,mi nadhani kunavigezo vinavyotumika mpaka channel iwekwe dstv kwa tz hakuna channel yenye hadhi ya kuwa dstv wakiweka tv za mbongo sito lipia tena dstv
ngoja niagize mbege nizimue

Ni kweli unachosema Mkuu lakini chetu ni chetu tusikidharau sana, tuwape moyo kwa mategemeo kwamba baadae wanaweza kuboresha.
Sasa ukiangalia hii tv ya serikali TBC ndio utaona vichekesho. Wanaonyesha hadi reception za harusi tena full!
 
me nimekuelewa,hapo unachomaanisha ni kwamba tukiwa kwenye digitali utakosa habari kwakua utakua upo dstv,so ili nawe upate habar na usiwe na ving'amuz zaid ya kimoja ungependa Dstv wawe na channel za kitanzania huko,
ok labda watalifanyia kazi

Sawa kabisa Mkuu, ila haionekani kama wana nia hiyo Na TCRA inaonekana kwa DSTV hawana meno
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom