Wizara ya Habari kupitia Idara yake ya Maelezo imesimamisha Usajili wa magazeti kwa sababu ambazo mpaka sasa hivi hatuzijui.
Tofauti na Kenya ambako unaweza kuanzisha gazeti halafu baadaye kuliandikisha kibiashara hapa Tanzania huwezi kuanzisha gazeti bila kusajiliwa na Idara ya Maelezo.
Hii ni mojawapo ya sheria ambazo haifurahiwi na wawekezaji katika sekta ya habari -wa ndani na wa nje.
Huu ni msimu wa watu wengi wenye uchu na uroho wa ukubwa nchini kuanzisha magazeti uchwara ambayo muda wake wa kuishi ni kati ya kabla kidogo tu ya uchaguzi mkuu na mwisho wa uchaguzi mkuu.
Tofauti na Kenya ambako unaweza kuanzisha gazeti halafu baadaye kuliandikisha kibiashara hapa Tanzania huwezi kuanzisha gazeti bila kusajiliwa na Idara ya Maelezo.
Hii ni mojawapo ya sheria ambazo haifurahiwi na wawekezaji katika sekta ya habari -wa ndani na wa nje.
Huu ni msimu wa watu wengi wenye uchu na uroho wa ukubwa nchini kuanzisha magazeti uchwara ambayo muda wake wa kuishi ni kati ya kabla kidogo tu ya uchaguzi mkuu na mwisho wa uchaguzi mkuu.