Serikali ilijipanga kuongeza mishahara, ila covid19 imeharibu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,007
9,873
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman amesema serikali ilikuwa tayari imejipanga kuongeza viwango vya mishahara kwa watumishi wa umma, lakini kutokana na janga la corona, utekelezaji wa mpango huo umesitishwa kutokana na nchi kuyumba kiuchumi

Alisema serikali imejipanga kuimarisha maslahi bora ya watumishi wote, ikiwemo kuongeza mishahara kwa kadri wakati unaporuhusu

Katika kujali maslahi ya watumishi wa umaa Waziri Suleiman amesema walimu wote waliokuwa wakifanya kazi kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, wataajiriwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021

Waziri Suleiman alisema kutokana na uhaba wa walimu vijijini kuna baadhi ya watu waliosomea uwalimu walikuwa wanajitolea katika vijiji mbalimbali nchini kwa kulipwa ujira wa kujikimu na wanakijiji

Suleiman alisema hayo wakati akijibu hoja za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliotaka kupata ufafanuzi kwa nini wapo walimu wengi wanajitolea bila ya kuajiriwa hadi sasa

----
PIA WALIMU WALIOJITOLEA WAULA MWAKA WA FEDHA 2020/2021

WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman amesema walimu wote waliokuwa wakifanya kazi kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, sasa wataajiriwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021.

Suleiman alisema hayo wakati akijibu hoja za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliotaka kupata ufafanuzi kwa nini wapo walimu wengi wanajitolea bila ya kuajiriwa hadi sasa.

Akifafanua, alikiri kuwepo kwa suala hilo, ambalo limekuja kutokana na tatizo kubwa la uhaba wa walimu katika maeneo mengi ya vijijini. Alisema walimu hao walikuwa wakijitolea kufundisha wanafunzi bila ya kuajiriwa na kulipwa fedha kidogo za kujikimu zinazotolewa na wanavijiji.

“Spika napenda kuthibitisha kwamba walimu wote waliokuwa wakisomesha kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, sasa serikali itawaajiri katika kipindi hichi cha mwaka wa fedha 2020/2021,” alisema.

Alisema serikali imejipanga kuimarisha maslahi bora ya watumishi wote, ikiwemo kuongeza mishahara kwa kadri wakati unaporuhusu. Kwa mfano, alisema serikali ilikuwa tayari imejipanga kuongeza viwango vya mishahara kwa watumishi wa umma, lakini kutokana na janga la corona, utekelezaji wa mpango huo umesitishwa kutokana na nchi kuyumba kiuchumi.

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walipitisha makadirio, mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na kuidhinisha jumla ya Sh 15,617,500,000. Kati ya fedha hizo Sh 14,217,500,000 ni kwa kazi za kawaida na Sh 1,400,000,000 kwa kazi za maendeleo.


HABARI LEO
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman amesema serikali ilikuwa tayari imejipanga kuongeza viwango vya mishahara kwa watumishi wa umma, lakini kutokana na janga la corona, utekelezaji wa mpango huo umesitishwa kutokana na nchi kuyumba kiuchumi

Alisema serikali imejipanga kuimarisha maslahi bora ya watumishi wote, ikiwemo kuongeza mishahara kwa kadri wakati unaporuhusu

Katika kujali maslahi ya watumishi wa umaa Waziri Suleiman amesema walimu wote waliokuwa wakifanya kazi kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, wataajiriwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021

Waziri Suleiman alisema kutokana na uhaba wa walimu vijijini kuna baadhi ya watu waliosomea uwalimu walikuwa wanajitolea katika vijiji mbalimbali nchini kwa kulipwa ujira wa kujikimu na wanakijiji

Suleiman alisema hayo wakati akijibu hoja za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliotaka kupata ufafanuzi kwa nini wapo walimu wengi wanajitolea bila ya kuajiriwa hadi sasa

----
PIA WALIMU WALIOJITOLEA WAULA MWAKA WA FEDHA 2020/2021

WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman amesema walimu wote waliokuwa wakifanya kazi kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, sasa wataajiriwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021.

Suleiman alisema hayo wakati akijibu hoja za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliotaka kupata ufafanuzi kwa nini wapo walimu wengi wanajitolea bila ya kuajiriwa hadi sasa.

Akifafanua, alikiri kuwepo kwa suala hilo, ambalo limekuja kutokana na tatizo kubwa la uhaba wa walimu katika maeneo mengi ya vijijini. Alisema walimu hao walikuwa wakijitolea kufundisha wanafunzi bila ya kuajiriwa na kulipwa fedha kidogo za kujikimu zinazotolewa na wanavijiji.

“Spika napenda kuthibitisha kwamba walimu wote waliokuwa wakisomesha kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, sasa serikali itawaajiri katika kipindi hichi cha mwaka wa fedha 2020/2021,” alisema.

Alisema serikali imejipanga kuimarisha maslahi bora ya watumishi wote, ikiwemo kuongeza mishahara kwa kadri wakati unaporuhusu. Kwa mfano, alisema serikali ilikuwa tayari imejipanga kuongeza viwango vya mishahara kwa watumishi wa umma, lakini kutokana na janga la corona, utekelezaji wa mpango huo umesitishwa kutokana na nchi kuyumba kiuchumi.

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walipitisha makadirio, mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na kuidhinisha jumla ya Sh 15,617,500,000. Kati ya fedha hizo Sh 14,217,500,000 ni kwa kazi za kawaida na Sh 1,400,000,000 kwa kazi za maendeleo.


HABARI LEO
Tangu mwaka 2015 hadi 2019 kulikuwa na covid 19? Mbona mishahara haikuongezwa? Kazi ya utumishi wa Umma ni wito.
 
Tanzania olive na waandishi uchwara wa habari kesho wataandika "JPM amwaga ajira kwa walimu wanaojitolea"
Najiuliza tu, hivi kuna mpumbavu alikuwa anajitolea zaidi ya miaka 10 huku anawaona wenzake wakikopa bank na kununua pikipiki na kujenga huku yeye akisubiri zari?
Hakuna hao watu waache uzushi.
 
WAZIRI WA UTUMISHI NI GEORGE H. MKUCHIKA

NAIBU WAZIRI NI DR. MARY M. MWANJELWA

Sa huyu Haroun Ali Suleiman unayemtaja ni wa nchi gani??
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman amesema serikali ilikuwa tayari imejipanga kuongeza viwango vya mishahara kwa watumishi wa umma, lakini kutokana na janga la corona, utekelezaji wa mpango huo umesitishwa kutokana na nchi kuyumba kiuchumi

Alisema serikali imejipanga kuimarisha maslahi bora ya watumishi wote, ikiwemo kuongeza mishahara kwa kadri wakati unaporuhusu

Katika kujali maslahi ya watumishi wa umaa Waziri Suleiman amesema walimu wote waliokuwa wakifanya kazi kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, wataajiriwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021

Waziri Suleiman alisema kutokana na uhaba wa walimu vijijini kuna baadhi ya watu waliosomea uwalimu walikuwa wanajitolea katika vijiji mbalimbali nchini kwa kulipwa ujira wa kujikimu na wanakijiji

Suleiman alisema hayo wakati akijibu hoja za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliotaka kupata ufafanuzi kwa nini wapo walimu wengi wanajitolea bila ya kuajiriwa hadi sasa

----
PIA WALIMU WALIOJITOLEA WAULA MWAKA WA FEDHA 2020/2021

WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman amesema walimu wote waliokuwa wakifanya kazi kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, sasa wataajiriwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021.

Suleiman alisema hayo wakati akijibu hoja za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliotaka kupata ufafanuzi kwa nini wapo walimu wengi wanajitolea bila ya kuajiriwa hadi sasa.

Akifafanua, alikiri kuwepo kwa suala hilo, ambalo limekuja kutokana na tatizo kubwa la uhaba wa walimu katika maeneo mengi ya vijijini. Alisema walimu hao walikuwa wakijitolea kufundisha wanafunzi bila ya kuajiriwa na kulipwa fedha kidogo za kujikimu zinazotolewa na wanavijiji.

“Spika napenda kuthibitisha kwamba walimu wote waliokuwa wakisomesha kwa njia ya kujitolea kwa zaidi ya miaka kumi, sasa serikali itawaajiri katika kipindi hichi cha mwaka wa fedha 2020/2021,” alisema.

Alisema serikali imejipanga kuimarisha maslahi bora ya watumishi wote, ikiwemo kuongeza mishahara kwa kadri wakati unaporuhusu. Kwa mfano, alisema serikali ilikuwa tayari imejipanga kuongeza viwango vya mishahara kwa watumishi wa umma, lakini kutokana na janga la corona, utekelezaji wa mpango huo umesitishwa kutokana na nchi kuyumba kiuchumi.

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walipitisha makadirio, mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na kuidhinisha jumla ya Sh 15,617,500,000. Kati ya fedha hizo Sh 14,217,500,000 ni kwa kazi za kawaida na Sh 1,400,000,000 kwa kazi za maendeleo.


HABARI LEO
FAKE NEWS
 
Back
Top Bottom