Serikali ilichapisha fedha bila mpangilio?

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,319
Inasemekana kupungua kwa thamani ya Tsh, kunakoakisiwa na kupanda kwa bei ya bidhaa siku za karibuni kumetokana na serikali kuchapisha fedha nyingi bila kujali tija ya taifa katika kipindi hiki cha uchaguzi. Inasemekana kuwa fedha hizo zilichapishwa ili CCM iweze kupata fedha kwa ajili ya kukisaidia kushinda, lakini pia ili serikali iweze kugbharamia matumizi mengine ikiwemo mishahara na posho mbalimbali za watendaji wake. Hali hii imesababisha mwangwi mkubwa wa mfumuko wa bei hasa baada ya uchaguzi kutokana na kupungua thamani ya shilingi pale inahitajika kwa ajili ya kuagiza bidhaa na malighafi kutoka nje.

Wataalamu wa uchumi wanatabiri ugumu mkubwa wa maisha wakati seriakali ikijitahidi kujitoa katika hali hii, na inasemekana kuwa benki zitaathirika zaidi endapo watanzania na watu wengine waliopo nje ya nchi wataamua kuweka fedha za kigeni benki na kuzibadilisha kuwa shilingi, kwani kwa wakati huu shilingi itakuwa na thamani ndogo, hali ambayo itaathiri benki pale shilingi itakapopanda thamani (Hii ina maana kuwa kwa mfano kama ukiweka uro moja benki kwa sasa itahesabiwa kama labda tsh 2000. Miezi michache ijayo pengine shilingi itapanda bei na kuwa tsh 1800 kwa uro 1, then benki itakuwa na hasara ya tsh 200 kwa kila uro ambayo itakuwa imepokea kwa sasa).
 
Back
Top Bottom