Tallmfupi
JF-Expert Member
- Dec 1, 2015
- 240
- 78
Salam kwenu wakuu,
Kama mkereketwa wa masuala ya elimu, Nina imani serikali inaitambua vyema shule hii yenye historia maridhawa.
Ikiwa imeanzishwa Mwaka 1929 na ikijulikana kama st.Thomas more kipindi hicho, imeweza kuzalisha watu wenye upeo mkubwa na dhamana mahususi hapa nchini.
Lakini ni jambo kubwa la kushangaza kusikia shule hii ikiwa ni miongoni mwa shule zenye migomo ya Mara kwa Mara na mazingira mabovu sana kwa mwanafunzi kuweza kupata elimu bora.
Chakula kisicho bora, walimu wachache na miundombinu iliyozeeka hasa vyoo na mabweni na ikikumbukwa kuwa imeanzishwa Mwaka 1929. Hii yote hupelekea shule hii iliyobeba historia ya bukoba na mkoa wa kagera kutokufanya vizuri.
Hivyo ni jukumu la serikali kuitilia maanani shule hii ya "advance" na kuweza kuondoa kero zinazowakabili wanafunzi na walimu katika utoaji wa elimu bora.
Mwisho napenda kuwahamasisha wale wote waliopitia katika shule hii na wale wenye mapenzi na elimu ya nchi yetu kuweza kuichangia kwa chochote walichonacho ili kuweza kuboresha hali ya shule hiyo. Ahsanteni..
Kama mkereketwa wa masuala ya elimu, Nina imani serikali inaitambua vyema shule hii yenye historia maridhawa.
Ikiwa imeanzishwa Mwaka 1929 na ikijulikana kama st.Thomas more kipindi hicho, imeweza kuzalisha watu wenye upeo mkubwa na dhamana mahususi hapa nchini.
Lakini ni jambo kubwa la kushangaza kusikia shule hii ikiwa ni miongoni mwa shule zenye migomo ya Mara kwa Mara na mazingira mabovu sana kwa mwanafunzi kuweza kupata elimu bora.
Chakula kisicho bora, walimu wachache na miundombinu iliyozeeka hasa vyoo na mabweni na ikikumbukwa kuwa imeanzishwa Mwaka 1929. Hii yote hupelekea shule hii iliyobeba historia ya bukoba na mkoa wa kagera kutokufanya vizuri.
Hivyo ni jukumu la serikali kuitilia maanani shule hii ya "advance" na kuweza kuondoa kero zinazowakabili wanafunzi na walimu katika utoaji wa elimu bora.
Mwisho napenda kuwahamasisha wale wote waliopitia katika shule hii na wale wenye mapenzi na elimu ya nchi yetu kuweza kuichangia kwa chochote walichonacho ili kuweza kuboresha hali ya shule hiyo. Ahsanteni..