Serikali ikomeshe huu utaratibu wa wanafunzi kukusanyika kushangilia wasanii wanapotembelea mashuleni kutoa misaada

kishegheni

Member
Mar 6, 2012
21
85
Nina kitu kinanishangaza,. kunsikitishai na kushindwa kuelewa sababu za serikali kuruhusu wanafunzi kusitisha masomo ili kuwasubiri na kuwashangilia wasanii wa muziki au filamu wanapofika mashuleni kutoa misaada.

Huu utaratibu umeendelea kwa.kipindi kirefu mpaka sasa. Hii leo tumeona kwenye Mitandao watoto wa shule wakiimba wimbo wa "Nyegezi" uliofungiwa na BASATA mbele ya Mkuu wa Wilaya na Diamond na team yake ya Wasafi wakati walipotembelea shule moja huko Iringa..

Mbona watu wengi wanatoa misaada mikubwa mikubwa kusaidia mashule na sehemu mbalimbali lakini hatuoni watotkowakitoka madarasani na kukusanyika ili kuwasubiri watoa misaada 'na wala hawajitangazi kwenye mitandao wala magazeti ka.wasanii. Hii tabia imekithiri kwa wasanii zaidi na sielewi wanafanya hivi kwa nia gani. Misaada yenyewe haijulikani ni misaada ya aina gan wanayotoa. Sana sana wanatafuta umaarufui.

Hata matamasha wanayofanya wasanii mikoani ndio kabisaaa shughuli zote ndio zinasimama kuanzia mkoani mpaka wilayani. Utasikia wanakutana na Mkuu wa Mkoa mara Mkuu wa Wilaya. Mbona watu wengine wakitembelea mikoani hawafanyi hivi.

Waziri wa Elimu na Waziri wa TAMISEMI tunaomba.mkomeshe tabia hii kwani inawadhalilisha viongozi, wazazi, walimu na kuwapotezea watoto wetu muda wa kusoma.

Kwa kweli jambl hili linatukera sisi wazazi.
 
Matamasha ya muziki ni fursa kwa wakazi wa eneo husika, kwa mfano sasa hivi yaani muda huu wakazi wa iringa wenye bodaboda, wauza maji,vyoda, vyakula vyepesi, pombe n.k wanapiga pesa mbayaaa kwa ujio wa hao wasanii unaowaona wanafanya upuuzi.
.
Kuhusu wanachokifanya kwa wanafunzi kinafanyika kwa mtindo huo kwa sababu wao ni kioo cha jamii ni brand sio kama wewe hujulikani hata na panzi uitishe press si itakuwa kituko?
.
Acha chuki
 
Lengo ni kuhamasisha wanafunzi wapende kuimba mashairi darasani kuliko kusoma maana hata sylabus inatambua mziki ni muhimu kuliko Bunsen banner.

Pia kuwahamasisha wanafunzi wakitoka shule waende kushangilia mziki uwanjani usiku kucha.

Kuna tatizo kwani?
 
Matamasha ya muziki ni fursa kwa wakazi wa eneo husika, kwa mfano sasa hivi yaani muda huu wakazi wa iringa wenye bodaboda, wauza maji,vyoda, vyakula vyepesi, pombe n.k wanapiga pesa mbayaaa kwa ujio wa hao wasanii unaowaona wanafanya upuuzi.
.
Kuhusu wanachokifanya kwa wanafunzi kinafanyika kwa mtindo huo kwa sababu wao ni kioo cha jamii ni brand sio kama wewe hujulikani hata na panzi uitishe press si itakuwa kituko?
.
Acha chuki
Nafikiri sio vyema kutazama kila kitu katika fursa tu za kiuchumi na kupuuza pande nyinginezo mfano muda wa kusoma katika hili.

Mleta mada anauliza kuna ulazima gani wa kukatisha vipindi vya masomo na kuwaruhusu wasanii waonane na wanafunzi? Hamna namna nyingine ya wao kuwafikia wanafunzi mpaka waende wakati wa masomo?

Uchumi unaotegemea matamasha ya wasanii kwa watu kuingiza kipato cha kueleweka ni uchumi usio imara kwa sababu haujawahakikishia wananchi ajira za kiwaletea vipato vya kueleweka.
 
Nafikiri sio vyema kutazama kila kitu katika fursa tu za kiuchumi na kupuuza pande nyinginezo mfano muda wa kusoma katika hili.

Mleta mada anauliza kuna ulazima gani wa kukatisha vipindi vya masomo na kuwaruhusu wasanii waonane na wanafunzi? Hamna namna nyingine ya wao kuwafikia wanafunzi mpaka waende wakati wa masomo?

Uchumi unaotegemea matamasha ya wasanii kwa watu kuingiza kipato cha kueleweka ni uchumi usio imara kwa sababu haujawahakikishia wananchi ajira za kiwaletea vipato vya kueleweka.
Mkuu siamini kama kuna vipindi vinakatishwa, kampeni ya kipepeo inapotembelea shule yoyote wanaenda muda usio wa vipindi vya darasani kwa mfano kuna kipindi cha dini n.k
.
Diamond na crewe yake wamefika kwenye ile shule muda ambao vipindi vimekwisha vipindi vinaisha saa 5-6 siku ya ijumaa inategemea na shule ilivyojipangia.
.
Kwa kumalizia hakuna njia nyingine kabisa ya celebrity kuwasilisha michango yake pasina kufanya mnachokiona tazama hata U.S Oprah winfrey, future, bill gates, jay z n.k wakitoa hata I pad lazima wafanye kilichofanya watambulike kwa umma wa dunia ujue.
 
Acha wivu mzee baba, na wewe kama una surplus katoe msaada na ni ruksa kuita hata CNN au BBC na kama ni famous watachoma hata shule moto kwa furaha ya kukuona live (just kidding)..
 
Nina kitu kinanishangaza,. kunsikitishai na kushindwa kuelewa sababu za serikali kuruhusu wanafunzi kusitisha masomo ili kuwasubiri na kuwashangilia wasanii wa muziki au filamu wanapofika mashuleni kutoa misaada.

Huu utaratibu umeendelea kwa.kipindi kirefu mpaka sasa. Hii leo tumeona kwenye Mitandao watoto wa shule wakiimba wimbo wa "Nyegezi" uliofungiwa na BASATA mbele ya Mkuu wa Wilaya na Diamond na team yake ya Wasafi wakati walipotembelea shule moja huko Iringa..

Mbona watu wengi wanatoa misaada mikubwa mikubwa kusaidia mashule na sehemu mbalimbali lakini hatuoni watotkowakitoka madarasani na kukusanyika ili kuwasubiri watoa misaada 'na wala hawajitangazi kwenye mitandao wala magazeti ka.wasanii. Hii tabia imekithiri kwa wasanii zaidi na sielewi wanafanya hivi kwa nia gani. Misaada yenyewe haijulikani ni misaada ya aina gan wanayotoa. Sana sana wanatafuta umaarufui.

Hata matamasha wanayofanya wasanii mikoani ndio kabisaaa shughuli zote ndio zinasimama kuanzia mkoani mpaka wilayani. Utasikia wanakutana na Mkuu wa Mkoa mara Mkuu wa Wilaya. Mbona watu wengine wakitembelea mikoani hawafanyi hivi.

Waziri wa Elimu na Waziri wa TAMISEMI tunaomba.mkomeshe tabia hii kwani inawadhalilisha viongozi, wazazi, walimu na kuwapotezea watoto wetu muda wa kusoma.

Kwa kweli jambl hili linatukera sisi wazazi.
Anapotembelea rais je na zaidi mwenge? Yote ni upotezaji muda wa wanafunzi na waalimu wao.
 
Back
Top Bottom