Serikali ikajifunze toka St. Francis Sekondari Mbeya kuboresha ufaulu wa kidato cha nne

Huu ndio ukweli hata serikali ikiboresha mazingira vipi bado itaendelea kutoa zero tu.

Mkuu hiyo shule ina mchujo mkali sana. Unataka serikali nayo ipitishe mchujo kwenye shule zake hao wanaochujwa watamalizia wapi kidato cha nne endapo serkali itafanya jambo kama hilo??

Serikali inachukua wanaofanya vizuri, wastani na low performers. Wakati hiyo st francis wanachukua cream tupu.

Sent using Jamii Forums mobile app



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jiulize tangu hio shule ianze kupata matokeo hayo zaidi ya miaka 10 iliyopita hao wanafunzi wameleta impact ipi kwa taifa?
Ni rahisi kumkuta kijana wa Taboraboys aliyepata one ya 16 akifanya vizuri chuo hadi mtaani na carrier yake,kuliko hao wa Francis wa 7.
Au kijana wa Zanzibar/Pemba aliyepata zero ni rahisi sana kuwa na kiwanda cha juisi ya miwa/duka la vitu used,ama duka la engine pale kariakoo.......ni rahisi mno kufanikiwa..........kuliko huyo wa St Francis kuja kuzunguka na bahasha akiwa na degree yake ya marketing.
Nafananisha na african countries unazaa matoto yenye afya yanakuja kua omba omba

Sent using Jamii Forums mobile app
Naona umeweka mpira kwapani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeandika vizuri ila yote hayo ni ndoto, hakuna hata moja ambalo serikali inaweza kutekeleza hata kwa asilimia 10 tu. Kuna shule huko vijijini zina wanafunzi 1000 na walimu ni watano tu akiwemo mkuu na msaidizi wake. Hakuna maktaba wala maabara, madawati ni kitendawili na maeneo mengi hakuna tena hata uji
Given time, Magufuli yupo atarekebisha, hilo sina wasiwasi nalo hata chembe. Tatlizo kubwa la msingi ni kuwa Magufuli hana uwezo wa kurekebisha matatizo ya Nchi yetu yote kwa wakati mmoja kwa mkupuo. Aliahidi atarekebisha hiyo ni sawa kabisa, lakini hakusema kuwa ana uwezo wa kuyarekebisha yote kwa mkupuo, na wala hana uwezo huo, na wala hakuna mtanzania mwenye uwezo huo KWA SABABU NCHI YETU BADO HAIJAFIKIA UWEZO HUO, ILA MAGUFULI NDIYO ANAFANYA MKAKATI WA KUIIPELEKA KWENYE UWEZO HUO, AU KARIBU KABISA NA UWEZO WA AINA HIYO!
 
unasema "Given time" Kama unataka JPM mwenyewe arekebishe basi ana miaka kama 5 tu ya kufanya hayo marekebisho, ungesema serikali ningekuwa na imani kidogo sababu itaendelea kuwepo hata baada ya JPM.

Sent using Jamii Forums mobile app
Uko sahhi kabisa ndugu yangu. Kwa maana nyingine nilimaanisha kuwa by 2025, tatizo hili litakuwa Historia, Serikali itakuwa imerekebisha, ambayo ni ya JPM. Serikali itakayoingia baada ya hii, haitaliwahi tena tatizo hili, halitakuwepo kwa sababu halina nafasi tena ya kuvuka 2025
 
Uko sahhi kabisa ndugu yangu. Kwa maana nyingine nilimaanisha kuwa by 2025, tatizo hili litakuwa Historia, Serikali itakuwa imerekebisha, ambayo ni ya JPM. Serikali itakayoingia baada ya hii, haitaliwahi tena tatizo hili, halitakuwepo kwa sababu halina nafasi tena ya kuvuka 2025
Haya Mkuu. Tutegemee 2025 shule zote zitakuwa na mazingira na ufaulu kama St.Francis.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapi nimesema nikosa?
Hata hivyo unadhani ulichoandika ni sahihi sana ?

Kwanza selection ya kupata wenye uwezo wa kusoma inafanyika na shule zote ambazo unafanya interview ukitaka kusoma sio St. Francis peke yake.

Maana imeandikwa kama wao wana a particular selection criteria ambayo wengine hawatumii. Hapo ndio mnapindisha kwa kujua au kutokujua.

Pale unapokelewa na mtihani uliotungwa palepale.

Waombaji ni wengi sana na nafasi ni kama 100 tu. Darasani moja pale sisi nakumbuka tulikuwa @45 tu sijui siku hizi.

Pale mwanafunzi hapokelewi kwa nguvu ya hela .Hata Marian sidhani.

Shule nyingi binasi vibosile wanalazimisha kwa pesa. Ndio maana Kifungilo ilisumbua sana, sasa hivi sijui kama bado ipo.

Mi nimesoma pale na sio kweli eti ukitoka pale uko mbele wanafunzi wanasota wanakuwa mbumbumbu kabisa hizo data sijui wanazitoa wapi.

Kwa mfano mwaka huu wamefaulu ni kama 70 tu nani atafiatlia wote hao. Wazee wengi wanaopeleka watoto pale ni wenye uelewa mkubwa wa elimu na wengi uchumi uko vizuri. Wengine wakitoka pale ni scholarship ya kujilipia moja kwa moja.

Wengi wanaandika mambo ya kufikirika sijui kumfurahisha nani, na inaweza kuwakatisha tamaa watu wasipeleke watoto wao pale.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Given time, Magufuli yupo atarekebisha, hilo sina wasiwasi nalo hata chembe. Tatlizo kubwa la msingi ni kuwa Magufuli hana uwezo wa kurekebisha matatizo ya Nchi yetu yote kwa wakati mmoja kwa mkupuo. Aliahidi atarekebisha hiyo ni sawa kabisa, lakini hakusema kuwa ana uwezo wa kuyarekebisha yote kwa mkupuo, na wala hana uwezo huo, na wala hakuna mtanzania mwenye uwezo huo KWA SABABU NCHI YETU BADO HAIJAFIKIA UWEZO HUO, ILA MAGUFULI NDIYO ANAFANYA MKAKATI WA KUIIPELEKA KWENYE UWEZO HUO, AU KARIBU KABISA NA UWEZO WA AINA HIYO!
Nimesema ni ndoto kwa sababu hakuna mkakati wowote ule wa makusudi leo wala kesho
 
Kwa hiyo hujaona chochote kilichofanyika mpaka sasa si ndiyo?
Kinachofanyika bado ni non significant kama kweli tunahitaji elimu bora. Siasa zimekuwa nyingi kuliko mikakati, we mpaka leo kila mwaka wanafunzi wanachelewa kujiunga kidato cha kwanza kwa sababu ya upungufu wa vyumba vya madarasa. Yaani wanajua kabisa idadi ya watakaomaliza std 7 mwakani na wanaweza kuproject ufaulu lakini wanakaa bila mipango yoyote mpaka matokeo yanatoka. Kiufupi hali ya elimu ni duni sana kama unataka kuyaona mambo kwa uhalisia wake
 
Huwezi kufananisha St Francis na shule za Kata.
Waanze na hili Moja kila shule iwafanyishe mtihani wa usaili wanafunzi Kabpa ya Kuanza kidato cha Kwanza.
Shule za kata zinapelekewa mpaka watoto Hawajui kusoma jmn watafaulu vipi?
Taratibu za shule za serikali ni ngumu hata wakihamishwa watoto washule Moja ya Kata wakapelekwa St Francis bila mchujo watafeli tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Namna ya kuingia St Francis, wanafanya mtihani watoto zaid ya 1000 af wanachukua 100 tu ila huko shule za kata darasa la saba zima linahamia secondary moja. Wanafunzi hao hawalingani kiuwezo tusizilaumu tu shule za serikali, Kuna watoto wana uwezo mdogo jaman huwez kumfundisha akafaulu. Mbona matokeo ya kidato cha sita shule za serikali huongoza. Kwasababu watoto wengi wanaofaulu na kupangiwa shule za serikali huwa wanaripoti.

Wazazi wa watoto wanaosoma st Francis wengi ni waelewa wanajua umuhimu wa elemu, wanashirikiana vzr kufatilia maendeo ya watoto wao. Huwez kufananisha na wazaz wa watoto shule za kata. Yan wakiambiwa mchango wa buku moja kwa mwez watoto wao wapikiwe uji wazaz wanagoma.

Sikatai Kuna tofauti kubwa za kimazingira ktk shule hizi za private na serikali. Lakini kufaulisha vzr sababu zake ni multidimensional, hatupaswi kuangalia upande mmoja wa walimu peke yao. Zipo sababu nyingi nje ya walimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kipindi kile Elimu na michango mlikua mnafurahia kweli wanafunzi kuja kwa wingi secondary, na sana sana mlikua mnafurahia hiyo michango na sikingine

Hii Leo serikali imeondoa michango mnawaona ni mizigo na hawana akili

Ujue nyinyi walimu ndiyo maana mnashia kuwa walevi wagongo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gabbage IN Gabbage OUT.

Vijana wao wa Form I wanapatikanaje? Ukishajua hilo basi hata serikali haina haja ya kwenda kujifunza chochote kwani malengo yao ni tofauti kabisa. Lengo la serikali ni kila mwanafunzi asome bila kujali uwezo wake wa akili; St Francis wao lengo lao ni kupokea wale wanafunzi waliofanya vizuri sana darasa la saba ili na matokeo ya Form IV wafanye vizuri.
Lakini tambua kila kitu kinahitaji maandalizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nani kakwambia Mimi mwalimu na siku hizi michango hakuna? Acha kukurupuka.
Kipindi kile Elimu na michango mlikua mnafurahia kweli wanafunzi kuja kwa wingi secondary, na sana sana mlikua mnafurahia hiyo michango na sikingine

Hii Leo serikali imeondoa michango mnawaona ni mizigo na hawana akili

Ujue nyinyi walimu ndiyo maana mnashia kuwa walevi wagongo.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom